Mume wa mtu ananipa wakati mgumu

Mume wa mtu ananipa wakati mgumu

Wengine hatujui kidhungu jamani, hata mleta uzi umeandikwa kiswazi
Nimesema kwamba atakuja kutoka na mwanamke mwingine tena hata akibi naye. Cha maana ni kwamba inauma sana ila tu namuombea kwa Mungu ampe Baraka zake na baada ya muda huzuni yake itaisha tu. Mungu wetu ni mwema.
 
  • Thanks
Reactions: nao
Kwa tamaa zako na kukosa maarifa utaikosa mbinguu wewe..
 
Kama umewahi cheza chess board basi ujue jamaa alikuwa anakusukumia kete ule(gari viwanja) akijua ana force King, in fact hii game keshakuzidi maana king inakula kwa dharau sana, Na tayari amekaa equator, wewe kuja hapa ni dalili tosha, muombe tu muanze game mpya hii keshashinda.
 
Lol! sikiliza moyo wako, mwambie achague mmojawapo kati wako na mkewe.
 
Ni bora huyo ana mke lakini amekupenda na wewe pia tena kakupenda sana we kuwa nae tu mapenzi yaendelee coz we si umeshaamua kuwa bachelor forever so what?acha kumliza mshikaji.
 
Baki mchepuko hivyohivyo kama ulivyokuwa unaringa kuolewa. Mwenzako alichukua fursa. Tena yawezekana aliolewa wakati unamzungushazungusha. Halafu cha ajabu wewe ni single mother na bado unadengua kama kigoli!!! Khaaa…
 
Wasukumua mwanaume kuwa na wake wawili au zaidi ni culture
so anajua anachokifanya
wewe tulia muache yeye ndo ata handle kila kitu
i am sure mkewe hattakusumbua hasa kama ni msukuma pure...

uko kwenye polygamy
kama Jacob Zuma na wake zake
its just life here in africa
nothing new
Asante kumbe sukuma ndio tabia yao. Uhiii
 
Kama umegundua jamaa Ana ndoa yake Tafadhali acha ndoa ya watu Dada,Wanaume wengi humu wamekutia moyo kua endelea Na huyo jamaa Ila unajipa laana amini usiami kama wewe ni mkristo lazima haya kuna siku yatakurudia.
Ni jinsi gani huyo Dada mwenye mme ameumia hebu fikiria ulivyoumia wewe alivyokwambia Ana Mke hadi wivu ukakukaba si zaidi ya Mama watoto wake alivyotoa jozi baada ya kuambiwa ukweli juu yako?
Alichokiunganisha Mungu binadamu asikitenganishe hivyo usiwe mmojawapo ya wavunja ndoa za watu,mliyoyatenda yatosha sasa tubu Mungu atakupa aliye wako achia ndoa ya watu nakusihii ktk jina la Yesu.
Nimeshikwa Na huzuni Nakuhisi maumivu ya huyo Mke Na watoto,usipo mwacha naomba Mungu aje Akugeuzie hiki kibao uje uyahisi haya maumivu kabla hujafa.
nao umeandika kwa huruma sana. Hivi ndivyo dunia ilivyo kwa sasa, so sad! Kama upo kwenye ndoa unaujua uchungu na wivu wa kuchukuliwa mtu wako.

Bahati mbaya wengi hawasikii wala kuona.
 
  • Thanks
Reactions: nao
Usiharibu ndoa ya mwanamke mwenzio. Fikiria yale machozi; lazima ujifunze upendo; na mojawapo ya upendo na kujitoa hata kama wew unaumia Mungu atakutia nguvu. Hawa wanaume wanakwambia nakupenda sana na yule mwanamke wangu nilimuoa tu bt sikumpenda hata; lakin kuna kitu ukijiuliza je akienda kwake anaweza chat na ww zile txt za love? Au akienda kwake unaweza mpigia cm muda wowote unao utaka? Au ndio ile mwanaume anakwambia nipo nyumbani tayar usipige simu wala usinitxt.Hapo sasa utajua kuwa bado anamuheshimu mkewe na anampenda sema akija kwako anataka pumziko sababu kule ukute wife ana makwazo mengi lakin hata akiwa na mwakwazo mengi bado anampenda ndio maana hamuachi na hii ndio inayoitwa ndoa kuvumiliana ktk shida na raha.

Anakuona ww asali sababu hajakaa na ww miaka yooote na mkajuana vzr; sababu umesema kila mtu anaishi kwake. Kuna tofaut ya kumuona mtu dakika au siku moja halafu akaondoka na akarud kwa muda mwngne na mtu kukaa naye kila siku yaan kakukera yupo kakufurahisha yupo tu had unahitaj space ya kupumua bt ndio mume hawez ondoka. Ila kwako akikuudh ataondoka baadaye akirud hasira zimeisha mapenz yanaendelea.

Na je akiwa kwako? Mkewe akimpigia simu huwa hapokei simu ya mkewe? Bila shaka anapokea na hatak kumis call wa txt lazima ajibu zote hata kama akiwa yupo na ww karibu sababu ana muheshimu mkewe na hatak kumuumiza; na ukute hata txt za mkewe hazifut ktk simu yake ila za kwako ww mchepuko lazima azifute ili mkewe asizione na hebu kapekue simu kakusave vip ukute ni dada au hajakusave kabisaaaa.

Halafuuuu kwanini hutak kuolewa? Hayo maneno yako umejifunga. Kumbuka ktk kinywa zinatoka baraka na laana. Sasa ww umejinenea laana hebu futa hayo maneno kuwa hutak kuolewa; sema sasa nataka kuolewa na yale maneno ya mwanzo yafute kabisaa usimpe shetan nafas akakufunga kwa maneno yako ndio maana hata Mungu anashindwa hata kukusaidia hata akileta mume huon sababu ulisha funga mlango wa ndoa. Na kingineeeee kuzalishwa ni nini? Huyo aliyekupa mtoto ndio akufanye usiolewe.?
Jiulize hiv ?
Huyo aliyekuzalisha sa hiz anafanya nn; ukute ameshaoa na yupo happy na family yake hata memory na ww hanaaa.

Hebu kung'uta mavumbi move on woman move on. Sio wanaume wote wabaya ; nakuhakikishia wapo best husband in da word choic ni yako; ukiamua kuwa mshikio wenzio wanapakua sawa. Bt ukiamua ww ni mpish na bado unapakua na unakula mwenyew ni maamuz yako. Move on utapata mume tena mzuri had watu washangae; acha kung'ang'ana na mume wa mtu unakosa baraka za kupata wako peke yako. Tena tubu hiyo dhambi ili ukiolewa mume wako asifanye hayo kwa wengine ; ziba huo mlango shetan asiingilie na asiutumie bt yakupasa kujutia dhambi uliyo ifanya na urud kwa Mungu.

Halafuuuuuu wanaume kukupa pesa hawaonag shida tena akiwa nazo na akiwa na mkono wa kutoa; hata ukitaka nini lazima akupe; mapenz sio pesa though sikatai ina chukua nafasi bt hapa naongelea ule upendo wetu uleee halis wa kina dada au mama ambao Mungu katupatia ule huwa haungalii pesa hata kidogo tunapenda from moyon. Lakin mwanaume anaweza kukupa pesa ukahis anakupenda; hakuna hicho kitu wapo humu ngoja wataeleza vzr; mwanaume anaweza akagawa pesa lakin anajua kabisaaa my heart mwanamke fulan ndiye anaye deserve; anakuja kwako atue mzigo tuu . kulala kwa mkewe hata akiwa kamuudh vip lazima arud kwake.

We need strong woman and ua a strong woman;stand up talk to God; speak to Him and tel Him that God help me; am doing this just for u ( God) utaona kama Mungu hatakuacha; lazima akutie nguvuu; Mungu anatusikiliza sana sisi wamama or wadada or mabinti sababu tuna something special inside ; evry drop of ua tears Mungu anahesabu. Simama plzzzz.

Ooh Mungu Linda mume wangu popote alipo macho yake yawe kwangu tu hata akifumba macho. Amen
 
Aiseeee.....kweli mapenzi ni mapezi....mahaba niue....sasa shemeji uwe muangalifu sana, aidha hama mji kabisa, jamaa kawekeza kwako ujue, upende usipende umenasa, ulitakiwa pale alipokwambia pale pale umwage mboga, ukaendelea kwa raha zako mwana kwetu.....
 
Nimesema kwamba atakuja kutoka na mwanamke mwingine tena hata akibi naye. Cha maana ni kwamba inauma sana ila tu namuombea kwa Mungu ampe Baraka zake na baada ya muda huzuni yake itaisha tu. Mungu wetu ni mwema.
Aaah!!
Sawa hizi lugha za kuja na ndege bana, kule kwenye shule zetu za st kayumba hii lugha haikufika[emoji3] [emoji3]
 
Niko kwenye mahusiano na mtu Kwa muda wa miaka 5 sasa. Mwanzoni aliniambia hajaoa na alikuwa anaishi hotel Kwa Sababu alihamishiwa mkoa nilipo Kikazi akitokea mikoa ya kanda ya ziwa.

Sana Sana katika mapenzi yetu niligundua Ni mtu anayejiheshimu Sana hata Kama alikuwa anapretend basi alipretend Kwa kipindi kirefu mno
Baadae alipata nyumba na tukaendelea yeye kwake na Mimi nikiwa kwangu na Mara moja moja tulilala kwake naye kulala kwangu miaka mitatu style ilikuwa hii

Nilimwambia wazi kuwa sina mpango wa kuolewa tangu nilipozalishwa mtoto na baba mtoto wangu kula kona si kutaka tena kuolewa Kwa sasa hivyo awe anajua kuwa siko katika mambo ya mipango na ndoa nayeye

Tulipendana Sana na heshima juu yetu ilishamiri. Mwaka wa nne wa mahusiano yetu alikuja kwangu siku moja akaniambia weekend twende Zanzibar me nikamwambia siwezi Kwa kuwa nitakuwa kazini akasema no no lazima niwe Nawe Zanzibar fanya uwezavyo

Ikabidi ofisini niwapelekee Report fake nikaenda Zanzibar huko jamaa yangu alionekana mkimya na mwenye mawazo Sana

Akatoa Pete mfukoni akaiweka mezani me tena macho yakanitoka Pete yandoa wala sio engagement akasema unaona hii Pete Ni yangu Mimi Ni Mume wa mtu samahani nimekaa Nawe sikuwahi kusema haya Kwa Sababu nakupenda Sana tens Sana sitaki kukukosa na sitakubali kukukosa maishani mwangu

Niliganda Kama nusu hasira zikanipanda wivu ukanikaba japo sikuwa na mpango wa kuolewa lakini Kwa jinsi trend ilivyokuwa inakwenda nilianza kufikiria tukifika miaka 7 ya mahusiano hakika atanibadili mawazo na naweza kuwa mkewe

Ndugu zangu na hata wazazi wangu wameshamuona kukitokea matukio ya mkusanyiko kwetu na upande wao pia Mara kadhaa nimeshaenda japo sio Mara nyingi ila kuna misiba na sherehe Fulani tulishiriki pamoja japo anabeba tabia zile za private life so nimemzoea hivyo hata wakati wa sherehe na misiba ya kwao hatukuwa jirani saana kiasi cha watu kuunga dots me niliona Ni kawaida yake na vile huwa simind kukabana na mtu Kama watoto wadogo mapenzini so sikuweza kugundua kuwa yeye anaprevent nini.

Turudi Zanzibar sasa pale alinibembeleza Sana kiukweli simkumsikiliza maombi yake kawa laingia kushoto lachomokea kulia
Kauli yake ilinifanya kufa ganzi Ni kuniambia mkewe anakuja kuishi nae hapa na ameona Ni vema atafute nyumba ingine Kwa Sababu pale itakuwa Ni picha tofauti Kwa majirani waliotuzoea Kama wapenzi

Nikamwambia sawa nashukuru nakutakia maisha mema he started crying na kubembelezaaa weee nikamwambia nipe muda maana akili yangu haiko sawa kabisa

Tukarudi Safari yetu kweli ilikuwa ya simanzi huku moyoni nikijiambia Mimi na yeye basi japo naumia ila Ni bora nimuache tu Kwa kweli

Nikakaa week moja huku nimeacha mawasiliano yawe upande mmoja wa yeye kunitafuta Mimi. Akaja kwangu one evening ameshakonda na kupungua ya kutosha kabisa akaniambia week ijayo mkewe anakuja nikamwanbia sawa akawa Kama anaishiwa maneno maana me jibu langu lilibaki sawa . Hata Mimi nilikonda pia Kwa Sababu jambo hili lilikuwa sio je je pesi kabisa.

Akaendelea kuja kwangu Sana hata baada ya mkewe kufika na tuakenda hivyo hivyo Hadi ukiingia mwaka huu wa tano . Ila Ni mapenzi tofauti na mwanzo . Akaanza kujitahidi kugharamia assets akaninunulia viwanja viwili na gari yangu akaniambia niuze niagize ingine aka ongeza pesa juu nikaagiza akaenda kulipa ada ya mtoto wangu shuleni Kwa miaka mitatu mbele vitu ambayo hajawahi kufanya kabisa tena Kwa majina yangu hizo asset amezinunua na kunikabadhi nyaraka zote na nilikuwa nazifuatilia mwenyewe . Ni hivi juzi tu nimetoka kuchukua nyaraka ya kiwanja kimoja wapo

Last week alikuja kwangu jioni Mimi nilichelewa kutoka kazini basi nikamkuta kakaa na mwanangu anamsaidia kumalizia home works baadae akapokea simu akaongea kilugha kisha akamaliza akaweka simu pembeni tukaendelea na mazungumzo yetu Mimi na yeye akaaga na kuondoka alisema mke hajisikii vema hivyo amemwambia ende hospital atamkuta huko ikawa bye

Kesho yake asubuhi akapiga simu saa 11 asubuhi akasema kuna tatizo Kumbe Jana alipo malizia kuongea na simu hakuikata so mke wake amefaidi mazungumzo yetu tano yake Kwa hiyo bomu baya limelipuka on my side nikaona haya mambo Ndio siyataki kabisa hii Ni Sababu muafaka ya Mimi kuachana nae for good

Mwanaume akasema usiwa na wasiwasi I'll handle situation me nikabaki na hasira moyoni mwangu cause I need a free man sio Mume wa mtu kila napofikiria kuachana limoyo langu linanisaliti . Nikaacha kupokea simu zake na nikablock namba yake kabisa Kwa kuanzia tu

Akaja akabembeleeza Sana akalia akasema yale yale Maneno ya Zanzibar kuwa hakubali kunikosa. Nikamwambia anipe nafasi na muda wa miezi miwili hivi ili nifikirie akasema miezi miwili mingi nikamwambia msimamo wangu Ni huo akaondoka zake Kwa makubaliano ya mawasiliano ya Mara moja moja Kwa simu ila asije kwangu wala sitaki kukutana nae popote . Nilichofanya nika unblock namba yake ili aweze kupiga na kutuma text

Wana JF Leo nimeamka asubuhi Ni siku 7 tu tangu tukwaruzane na kupeana time and space nakutana na message

"Hello baby , nimemwambia wife everything about us Kwa Sababu sitaki kukukosa please baby don't panic"

Jamani wanaJF hii message yaleo asubuhi imegeuza ulimwengu totally completely nifanyejeee
Kwenye thread ya single mother umetokwa povu hapa unatoa ushetani wako nyie mliozaa ni wakuogopa km ebolaa..
 
Kutaka mtu ambae hajaoa alafu huna mpango wa kuolewa ni kutaka mume wa mtu indirect ili ufanye uzinzi kitu ambacho dini zote haziruhusu.Tena unasema ulitaka ukae nae kama miaka 7 mnatafuta PhD?Wewe hujui unataka nini na huna malengo na maisha yako.Machozi ya mke wa mtu ni sumu kali.Huyo mke wa ndoa akianza kusali na kufunga jiandae kibao kitageuka na utaaibika sana.Tafuta mumeo huyo bado sio wako hata akimuacha mkewe.
 
  • Thanks
Reactions: nao
nao umeandika kwa huruma sana. Hivi ndivyo dunia ilivyo kwa sasa, so sad! Kama upo kwenye ndoa unaujua uchungu na wivu wa kuchukuliwa mtu wako.

Bahati mbaya wengi hawasikii wala kuona.
Huyo dada hana makosa jamaa ndiyo mwenye makosa kwanini hakumwambia huyo mwanamke kuwa ni mme wa mtu? Chukulia mfano demu ndiyo kakuficha hvyo miaka yote halafu mwisho wa picha anakuambia yeye ni mke wa mtu? We utakubali kirahisirahisi tu kumwacha bila moyo kuridhia? Big no mim namsapport dada wa watu asimwache jamaa
 
NGUMU KUMEZA HIYO NAE MKE WAKE ATAFUTA JAMAA =MAGONJWA.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom