Mume wa mtu ananipa wakati mgumu

Mume wa mtu ananipa wakati mgumu

Mtu anajisifu kabisa kufanya zinaa na watu wanashangilia:
9 Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,
10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.
1 WAKORINTHO 6
Haswaaa hiyo ni darsa tosha tu
 
Na atakayekuja kukuoa akawa anatoa matumizi kama hayo kwa kimada utafurahia? Malipo ni hapa duniani
 
Kama umegundua jamaa Ana ndoa yake Tafadhali acha ndoa ya watu Dada,Wanaume wengi humu wamekutia moyo kua endelea Na huyo jamaa Ila unajipa laana amini usiami kama wewe ni mkristo lazima haya kuna siku yatakurudia.
Ni jinsi gani huyo Dada mwenye mme ameumia hebu fikiria ulivyoumia wewe alivyokwambia Ana Mke hadi wivu ukakukaba si zaidi ya Mama watoto wake alivyotoa jozi baada ya kuambiwa ukweli juu yako?
Alichokiunganisha Mungu binadamu asikitenganishe hivyo usiwe mmojawapo ya wavunja ndoa za watu,mliyoyatenda yatosha sasa tubu Mungu atakupa aliye wako achia ndoa ya watu nakusihii ktk jina la Yesu.
Nimeshikwa Na huzuni Nakuhisi maumivu ya huyo Mke Na watoto,usipo mwacha naomba Mungu aje Akugeuzie hiki kibao uje uyahisi haya maumivu kabla hujafa.
 
Wasukumua mwanaume kuwa na wake wawili au zaidi ni culture
so anajua anachokifanya
wewe tulia muache yeye ndo ata handle kila kitu
i am sure mkewe hattakusumbua hasa kama ni msukuma pure...

uko kwenye polygamy
kama Jacob Zuma na wake zake
its just life here in africa
nothing new
Kwahiyo wasukuma kua na wake wawili ni kawaida? Duuh
 
Jamani tuwe na huruma yani umkalize mtu miaka saba ndio uamue kuoana nae?kweli jamani??[emoji25]
 
Pole sana...haya mambo huwa hayashauriki ww fuata moyo wako tu
 
Niko kwenye mahusiano na mtu Kwa muda wa miaka 5 sasa. Mwanzoni aliniambia hajaoa na alikuwa anaishi hotel Kwa Sababu alihamishiwa mkoa nilipo Kikazi akitokea mikoa ya kanda ya ziwa.

Sana Sana katika mapenzi yetu niligundua Ni mtu anayejiheshimu Sana hata Kama alikuwa anapretend basi alipretend Kwa kipindi kirefu mno
Baadae alipata nyumba na tukaendelea yeye kwake na Mimi nikiwa kwangu na Mara moja moja tulilala kwake naye kulala kwangu miaka mitatu style ilikuwa hii

Nilimwambia wazi kuwa sina mpango wa kuolewa tangu nilipozalishwa mtoto na baba mtoto wangu kula kona si kutaka tena kuolewa Kwa sasa hivyo awe anajua kuwa siko katika mambo ya mipango na ndoa nayeye

Tulipendana Sana na heshima juu yetu ilishamiri. Mwaka wa nne wa mahusiano yetu alikuja kwangu siku moja akaniambia weekend twende Zanzibar me nikamwambia siwezi Kwa kuwa nitakuwa kazini akasema no no lazima niwe Nawe Zanzibar fanya uwezavyo

Ikabidi ofisini niwapelekee Report fake nikaenda Zanzibar huko jamaa yangu alionekana mkimya na mwenye mawazo Sana

Akatoa Pete mfukoni akaiweka mezani me tena macho yakanitoka Pete yandoa wala sio engagement akasema unaona hii Pete Ni yangu Mimi Ni Mume wa mtu samahani nimekaa Nawe sikuwahi kusema haya Kwa Sababu nakupenda Sana tens Sana sitaki kukukosa na sitakubali kukukosa maishani mwangu

Niliganda Kama nusu hasira zikanipanda wivu ukanikaba japo sikuwa na mpango wa kuolewa lakini Kwa jinsi trend ilivyokuwa inakwenda nilianza kufikiria tukifika miaka 7 ya mahusiano hakika atanibadili mawazo na naweza kuwa mkewe

Ndugu zangu na hata wazazi wangu wameshamuona kukitokea matukio ya mkusanyiko kwetu na upande wao pia Mara kadhaa nimeshaenda japo sio Mara nyingi ila kuna misiba na sherehe Fulani tulishiriki pamoja japo anabeba tabia zile za private life so nimemzoea hivyo hata wakati wa sherehe na misiba ya kwao hatukuwa jirani saana kiasi cha watu kuunga dots me niliona Ni kawaida yake na vile huwa simind kukabana na mtu Kama watoto wadogo mapenzini so sikuweza kugundua kuwa yeye anaprevent nini.

Turudi Zanzibar sasa pale alinibembeleza Sana kiukweli simkumsikiliza maombi yake kawa laingia kushoto lachomokea kulia
Kauli yake ilinifanya kufa ganzi Ni kuniambia mkewe anakuja kuishi nae hapa na ameona Ni vema atafute nyumba ingine Kwa Sababu pale itakuwa Ni picha tofauti Kwa majirani waliotuzoea Kama wapenzi

Nikamwambia sawa nashukuru nakutakia maisha mema he started crying na kubembelezaaa weee nikamwambia nipe muda maana akili yangu haiko sawa kabisa

Tukarudi Safari yetu kweli ilikuwa ya simanzi huku moyoni nikijiambia Mimi na yeye basi japo naumia ila Ni bora nimuache tu Kwa kweli

Nikakaa week moja huku nimeacha mawasiliano yawe upande mmoja wa yeye kunitafuta Mimi. Akaja kwangu one evening ameshakonda na kupungua ya kutosha kabisa akaniambia week ijayo mkewe anakuja nikamwanbia sawa akawa Kama anaishiwa maneno maana me jibu langu lilibaki sawa . Hata Mimi nilikonda pia Kwa Sababu jambo hili lilikuwa sio je je pesi kabisa.

Akaendelea kuja kwangu Sana hata baada ya mkewe kufika na tuakenda hivyo hivyo Hadi ukiingia mwaka huu wa tano . Ila Ni mapenzi tofauti na mwanzo . Akaanza kujitahidi kugharamia assets akaninunulia viwanja viwili na gari yangu akaniambia niuze niagize ingine aka ongeza pesa juu nikaagiza akaenda kulipa ada ya mtoto wangu shuleni Kwa miaka mitatu mbele vitu ambayo hajawahi kufanya kabisa tena Kwa majina yangu hizo asset amezinunua na kunikabadhi nyaraka zote na nilikuwa nazifuatilia mwenyewe . Ni hivi juzi tu nimetoka kuchukua nyaraka ya kiwanja kimoja wapo

Last week alikuja kwangu jioni Mimi nilichelewa kutoka kazini basi nikamkuta kakaa na mwanangu anamsaidia kumalizia home works baadae akapokea simu akaongea kilugha kisha akamaliza akaweka simu pembeni tukaendelea na mazungumzo yetu Mimi na yeye akaaga na kuondoka alisema mke hajisikii vema hivyo amemwambia ende hospital atamkuta huko ikawa bye

Kesho yake asubuhi akapiga simu saa 11 asubuhi akasema kuna tatizo Kumbe Jana alipo malizia kuongea na simu hakuikata so mke wake amefaidi mazungumzo yetu tano yake Kwa hiyo bomu baya limelipuka on my side nikaona haya mambo Ndio siyataki kabisa hii Ni Sababu muafaka ya Mimi kuachana nae for good

Mwanaume akasema usiwa na wasiwasi I'll handle situation me nikabaki na hasira moyoni mwangu cause I need a free man sio Mume wa mtu kila napofikiria kuachana limoyo langu linanisaliti . Nikaacha kupokea simu zake na nikablock namba yake kabisa Kwa kuanzia tu

Akaja akabembeleeza Sana akalia akasema yale yale Maneno ya Zanzibar kuwa hakubali kunikosa. Nikamwambia anipe nafasi na muda wa miezi miwili hivi ili nifikirie akasema miezi miwili mingi nikamwambia msimamo wangu Ni huo akaondoka zake Kwa makubaliano ya mawasiliano ya Mara moja moja Kwa simu ila asije kwangu wala sitaki kukutana nae popote . Nilichofanya nika unblock namba yake ili aweze kupiga na kutuma text

Wana JF Leo nimeamka asubuhi Ni siku 7 tu tangu tukwaruzane na kupeana time and space nakutana na message

"Hello baby , nimemwambia wife everything about us Kwa Sababu sitaki kukukosa please baby don't panic"

Jamani wanaJF hii message yaleo asubuhi imegeuza ulimwengu totally completely nifanyejeee
Pole sana Dada. Huyu kaka kwanza amekudangsnys sana kwa kupretend hana mke kumbe anaye. Imagine the pain. However, he will cheat again with you with another women. He knows that you will put up with his cheating ways. It is painful either way, but always time will heal all wounds. GOD BLESSING UPON YOU. HE KNOWS YOUR COMING AND YOUR GOING. HE WILL HEAL YOU AND MAKE YOU A NEW CREATURE.
 
Assets zake unazipokea kwa mikono miwili tena kwa kumsifia kabisa ila yeye mwenyew kuwa nae ati moyo unasita sababu ana mke...subiri tu revenge upande wa pili ndo ujue dunia si ya mduara...
 
Yani dunia hii tena kibongobongo akununulie viwanja viwili nina imani atakujengea, akununulie gari, alipe ada ya mwanao tena na miaka ya ziada lol!
Halafu bado unajishauwa tu,kwangu mie hayo mapenzi sina, kweli jamaa kafa kaoza, any way maamuzi ni yako, isijekuwa ndo unapishana na msimu wa maisha,
Mbona baba yangu alikuwa na wanawake 3 japo ni marehemu kwa sasa na tuliishi vzr? Sembuse wewe?
 
Pole sana Dada. Huyu kaka kwanza amekudangsnys sana kwa kupretend hana mke kumbe anaye. Imagine the pain. However, he will cheat again with you with another women. He knows that you will put up with his cheating ways. It is painful either way, but always time will heal all wounds. GOD BLESSING UPON YOU. HE KNOWS YOUR COMING AND YOUR GOING. HE WILL HEAL YOU AND MAKE YOU A NEW CREATURE.
Wengine hatujui kidhungu jamani, hata mleta uzi umeandikwa kiswazi
 
Angalia furaha ya moyo wako. Kama unahisi ukimuacha huyo mwanaume utaumia then usimuache, ila kama unahisi unachokifanya si sahihi na moyo hauna amani muache huyo mwanaume.
 
Kama umegundua jamaa Ana ndoa yake Tafadhali acha ndoa ya watu Dada,Wanaume wengi humu wamekutia moyo kua endelea Na huyo jamaa Ila unajipa laana amini usiami kama wewe ni mkristo lazima haya kuna siku yatakurudia.
Ni jinsi gani huyo Dada mwenye mme ameumia hebu fikiria ulivyoumia wewe alivyokwambia Ana Mke hadi wivu ukakukaba si zaidi ya Mama watoto wake alivyotoa jozi baada ya kuambiwa ukweli juu yako?
Alichokiunganisha Mungu binadamu asikitenganishe hivyo usiwe mmojawapo ya wavunja ndoa za watu,mliyoyatenda yatosha sasa tubu Mungu atakupa aliye wako achia ndoa ya watu nakusihii ktk jina la Yesu.
Nimeshikwa Na huzuni Nakuhisi maumivu ya huyo Mke Na watoto,usipo mwacha naomba Mungu aje Akugeuzie hiki kibao uje uyahisi haya maumivu kabla hujafa.
Watu mmechukua majukumu ya Mungu kuadhibu wengine. We msafi kiasi gani hadi utake kuona binadamu mwenzio akipata mabaya?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom