Mume wa mtu ananilazimisha nizae naye

Mume wa mtu ananilazimisha nizae naye

Status
Not open for further replies.
Habari wana JF

Mimi ni mama wa mtoto mmoja wa miaka 5. Nipo kwenye mahusiano na mume wa mtu

Awali alinidanganya hana mke kwamba waliachana, niligundua ana mke baada ya kuwa nae kwenye mahusiano kwa miaka miwili. Tulizama kwenye penzi zito kila mtu alinogewa na penzi. Toka tunaanza mahusiano wimbo wake ni kuwa nizae na mimi kutokana na maamuzi yangu nikaona baadae itanikosti kuwa double mother

Kinachonisumbua ni hivi karibuni aliniambia kama sitaki kuzaa nae tuachane. Mimi nikamwambia tuendelee kuwa wapenzi ila kuzaa atafute mtu mwingine azae nae kwa sababu kwetu wanahitaji sana niolewe kwa process zote japo sijapata wa kunioa

Ushauri nifanyeje katika mahusiano ya namna hii
Wakati wewe unataka kuolewa na ubaki na mme wako pekeyake ,,,hakika kuna akina dada watatembea na mmeo kama wewe unavyotembea na mme wa mtu
 
uwww Una Chura? kama unae tufanye tumalizane tu hata mimi sitaki mtoto, weka pembeni huyo.
 
Huu Uzi una wahukumu wengi!!! Kana Kwamba ni malaika hawajawahi kosea😂😂😂..Kama dini inaruhusu mwambie akuoe mke wa pili ndipo uzae..Kama hairuhusu wewe Ni mtu mzima na wajua kila Jambo Lina tokeo..eiza zuri au baya..ni wewe sasa kuamua.
 
Usijaribu kufanya huo ujinga wanaume wengi hudaganya wanawake wazae, siku ukizaa hutamuona tena
Siyo hivyo bali ni ulimbukeni wa mapenzi. Inaonesha mwanaume anampenda sana huyo dada na hataki kumpoteza. Kwa bahati mbaya hajui mapenzi ni suala la muda tu hasa kama mtu hamuishi chumba kimoja. Mkianza kuishi chumba kimoja, mapenzi hayoooo
 
Wanaishiaga pabaya sana hawa , ogopa machozi ya mwanamke mwenzio wewe kama umeamua kuwa mtumwa wa ngono kuwa tu lakini usilete chuki ndani ya familia za watu.
Soma uelewe comment yangu mkuu, ukikurupuka hutaielewa. Nimesema, kwa kukusaidia, mwanaume ni ulimbukeni wa mapenzi na anadhani akamzalisha ndipo atammliliki. Kwa bahati mbaya maisha hayako hivyo, pindi akiibeba mimba, mwanamke ataanza kumtandika kiboko cha mimba. Hapo ndipo mategemeo ya mwanaume yatakapofifia. Akijifungua hapo ndo kabisa na gharama za kulea, mwishowe kama alivyosema cariha atamkimbia.

Kwa mwanaume anayejitambua hawezi kulazimisha kuzaa na mwanamke maana mateso mbele ya safari ni makubwa ajabu. Hata uwe na hela kama Jeff wa Amazon, bado viboko utatlchapwa na kuomba dunia ipasuke.
 
Soma uelewe comment yangu mkuu, ukikurupuka hutaielewa. Nimesema, kwa kukusaidia, mwanaume ni ulimbukeni wa mapenzi na anadhani akamzalisha ndipo atammliliki. Kwa bahati mbaya maisha hayako hivyo, pindi akiibeba mimba, mwanamke ataanza kumtandika kiboko cha mimba. Hapo ndipo mategemeo ya mwanaume yatakapofifia. Akijifungua hapo ndo kabisa na gharama za kulea, mwishowe kama alivyosema cariha atamkimbia.

Kwa mwanaume anayejitambua hawezi kulazimisha kuzaa na mwanamke maana mateso mbele ya safari ni makubwa ajabu. Hata uwe na hela kama Jeff wa Amazon, bado viboko utatlchapwa na kuomba dunia ipasuke.
Nadhani lugha zimegongana , namaanisha huyo mtoa mada kama ameamua kuwa mtumwa aendelee na utumwa wake , samahani mkuu kwa kukukanganya kidogo.
 
Siibi mume wa mtu coz awali wakati tunaanza mahusiano alinidanganya hana mke.
Baada ya kujua hilo hayo mahusiano unataka yaendelee ugundue nn sasa?? Ushajua ana mke na familia anakuambia kabisa kama hutaki muachane si uachane nae utafute wako? Utajisikiaje na ww ukiibiwa mumeo huko mbeleni? Nilichogundua unamchuna huyo jamaa anakupa sana hela so unataka kumtumia kww malengo yako ila kama kweli unataka kuolewa achana nae tafuta wako.
 
Baada ya kujua hilo hayo mahusiano unataka yaendelee ugundue nn sasa?? Ushajua ana mke na familia anakuambia kabisa kama hutaki muachane si uachane nae utafute wako? Utajisikiaje na ww ukiibiwa mumeo huko mbeleni? Nilichogundua unamchuna huyo jamaa anakupa sana hela so unataka kumtumia kww malengo yako ila kama kweli unataka kuolewa achana nae tafuta wako.
Huyo shori ni njaaa ndo inamsumbua tu , anajua anapata vipesa hapo sasa ataachaje ? NJAAAA MBAYA SANA
 
Nadhani lugha zimegongana , namaanisha huyo mtoa mada kama ameamua kuwa mtumwa aendelee na utumwa wake , samahani mkuu kwa kukukanganya kidogo.
Barikiwa mkuu, wengine tuna uchungu maana ni wahanga wa hii kitu
 
Siibi mume wa mtu coz awali wakati tunaanza mahusiano alinidanganya hana mke.
Kwa sasa unafahamu tayari na unaendelea kuwa nae, unaiba mme wa mtu. Fanya maamuzi ya kuachana nae.

Bahati mbaya sana viwango vyetu vya kimaadili vimeshuka mno na ndo maana unaona sawa kuwa nae plus kumruhusu atafute mwanamke mwingine muongezeke kwenye chain. Si sawa. Leave him.
 
Habari wana JF.

Mimi ni mama wa mtoto mmoja wa miaka 5. Nipo kwenye mahusiano na mume wa mtu.

Awali alinidanganya hana mke kwamba waliachana, niligundua ana mke baada ya kuwa nae kwenye mahusiano kwa miaka miwili. Tulizama kwenye penzi zito kila mtu alinogewa na penzi. Toka tunaanza mahusiano wimbo wake ni kuwa nizae na mimi kutokana na maamuzi yangu nikaona baadae itanikosti kuwa double mother.

Kinachonisumbua ni hivi karibuni aliniambia kama sitaki kuzaa nae tuachane. Mimi nikamwambia tuendelee kuwa wapenzi ila kuzaa atafute mtu mwingine azae nae kwa sababu kwetu wanahitaji sana niolewe kwa process zote japo sijapata wa kunioa.

Ushauri nifanyeje katika mahusiano ya namna hii
Mwambie akuoe
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom