Mume wa mtu ananilazimisha nizae naye

Mume wa mtu ananilazimisha nizae naye

Status
Not open for further replies.
Mme wa mtu atakuoaje sasa. ?

Yaani uolewe na Mme wa mtu?

Mme wa mtu akuoe wewe ndo unasubilia?

Kabisa unasubili Mme wa mtu akuoe halafu mkewe iweje ?

Mme kabisa Mme wa mtu.?

Yani wewe Dada Mme wa mtu yani?

Hivi umekaa ukisubili Mme wa mtu akuoe?
 
Habari wana jf. Mimi ni mama wa mtoto mmoja wa miaka 5. Nipo kwenye mahusiano na mme wa mtu.

Awali alinidanganya hana mke kwamba waliachana, niligundua ana mke baada ya kuwa nae kwenye mahusiano kwa miaka miwili. Tulizama kwenye penzi zito kila mtu alinogewa na penzi. Toka tunaanza mahusiano wimbo wake ni kuwa nizae na mimi kutokana na maamuzi yangu nikaona baadae itanikosti kuwa double mother.

Kinachonisumbua ni hivi karibuni aliniambia kama sitaki kuzaa nae tuachane. Mimi nikamwambia tuendelee kuwa wapenzi ila kuzaa atafute mtu mwingine azae nae kwa sababu kwetu wanahitaji sana niolewe kwa process zote japo sijapata wa kunioa.

Ushauri nifanyeje katika mahusiano ya namna hii.
Kasha kwambia Kama huhitaji kuzaa nae muachane wewe unang'@ng'nia nini?mchezea wembe acha umkate,Wanaume ambao hawajaoa wapo wengiii tulia tu utapata
 
Noma sana kiongozi, nainjoi jina lake
Unaweza fikiri hapo alifikiria nini hadi kutunga huo mjina na ukakosa jibu na hapo ndo utajua watu tunavichwa tofauti..😂

Angalia usije tungiwa nawe mjina wa aina hiyo..🤣
Kwakweli sijui alifikiria nini ngoja atujibu mwenyewe akina_baba_kabwela
Jina lina kiima na kiarifu
Mkuu unamuita tena..🙄

Kwa huo mjina aliojipa yeye usikute ni mzuri akivunja kibubu chake cha majina tutaweka wapi sura zetu..
Ngoja tuje tuone tutakimbiana hapa..🤣
 
Siibi mme wa mtu coz awali wakati tunaanza mahusiano alinidanganya hana mke.
WEWE NI MWIZI.
Hapo mwanzo hukujua kama ni mume wa mtu, sasa umejua. Ushauri unataka wa nini? Unataka tukushauri namna ya kuachana nae au kitu gani. Usingekuwa mwizi ungemuacha bila kuuliza.

Na kwa nini unataka azae kwingine kisha aje kwako. Yani unataka single mother mwingine kama wewe aibuke kisha upige maisha na mume wa huyo single mother.
 
Mme wa mtu atakuoaje sasa. ?

Yaani uolewe na Mme wa mtu?

Mme wa mtu akuoe wewe ndo unasubilia?

Kabisa unasubili Mme wa mtu akuoe halafu mkewe iweje ?

Mme kabisa Mme wa mtu.?

Yani wewe Dada Mme wa mtu yani?

Hivi umekaa ukisubili Mme wa mtu akuoe?
Bwana wee mbona unamfokea? Si anaweza kuolewa mke wa pili?
 
Bwana wee mbona unamfokea? Si anaweza kuolewa mke wa pili?
Kweli kabisa. Mdada anatakiwa aweke sharti la kuolewa (mke wa pili) kabla ya kukubali kumzalia mtoto baba huyo.

Tamaduni zetu nyingi na baadhi ya dini huruhusu ndoa za wake wengi.

Kumshauri huyo mwanaume azae na mtu mwingine sio sahihi.
 
S
Siibi mme wa mtu coz awali wakati tunaanza mahusiano alinidanganya hana mke.
Huibi kisa awali alikudanganya Hana mke! Baada ya kujua anaye unaendelea kwasababu huo sio wizi.Jamani acha tu huyo mnigeria aliyewamimba wanawake sita halafu kwa raha kabisa wanafoleni wapige picha wanaminywa matumbo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom