Mume wa mama mdogo ananirubuni anioe, nifanyeje?

Mume wa mama mdogo ananirubuni anioe, nifanyeje?

Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 21. Nilianza kuwasiliana na mwanaume nisiyemjua tangu mwaka 2013. Mwanaume huyu anadai ananipenda na nikimuomba hela ananitumia na anaponiambia tuonane moyo wangu unasita.

Nimemchunguza mpaka nimemjua kumbe ni mume wa mama yangu mdogo. Mimi sijawahi kwenda kwa mama mdogo. Nikimwambia ukweli kuwa wewe ni baba yangu mdogo na mkeo ni mama yangu mdogo anakubali ukweli huo.

Lakini ananiambia eti ananipenda na hayuko tayari kunikosa na kuwa yupo tayari kumuacha mama mdogo ili anioe na mimi nimetokea kumpenda nifanyeje?Tangu tuanze kuwasiliana sijawahi kuonana naye ila tunatumiana tu picha kwenye simu.

Naombeni ushauri.


Hii sasa chai jamani khaaa. Huyo siku akikumega tu, ndoa utaisikia radioni!
 
miaka 21 we ni msichana mdogo sana...zigatia masomo mdogo wangu,mapenzi utayakuta mbeleni ukisha maliza na kama husomi nipm phone number yako nikusaidie mtaji kidogo wa biashara maana naona unataka kuvuruga doa ya mama yako mdogo. naomba usimsariti mama yako mdogo laana itakuandama mpaka siku ya mwisho....muombe mungu akuepushie na dhambi hiyo.
 
Mbona fresh,olewa tu!...mtaani tumebaki masela tu,hakuna waoaji!
 
Kaolewe tu mdada..

Ukaendeleze kula raha za dunia, mahali mama yako mdogo alipoishia........

Mambo ya Walawi 18: 6-23


walawi 18:6? ?Hakuna mtu awaye yote atakayemsogelea ndugu wa karibu ili kukutana naye kimwili. Mimi ndimi BWANA.
7?? ?Usimvunjie heshima baba yako kwa kukutana kimwili na mama yako. Yeye ni mama yako, usiwe na mahusiano kama hayo naye.
8? ?Usikutane kimwili na mke wa baba yako, hiyo itamvunjia heshima baba yako.
9? ?Usikutane kimwili na dada yako, wala binti wa baba yako, au binti wa mama yako, awe amezaliwa katika nyumba hiyo au mahali pengine.
10? ?Usikutane kimwili na binti wa mwanao ama binti wa binti yako, utajivunjia heshima.
11? ?Usikutane kimwili na binti wa mke wa baba yako, aliyezaliwa na baba yako, huyo ni dada yako.
12? ?Usikutane kimwili na dada wa baba yako, ni ndugu wa karibu wa baba yako.
13? ?Usikutane kimwili na dada wa mama yako, kwa sababu ni ndugu wa mama yako wa karibu.
14? ?Usimvunjie heshima ndugu wa baba yako, kwa kukutana kimwili na mke wake, yeye ni shangazi yako.
15? ?Usikutane kimwili na mkwe wako, yeye ni mke wa mwanao, usiwe na mahusiano kama hayo naye.
16? ?Usikutane kimwili na mke wa kaka yako, utamvunjia heshima kaka yako.
17? ?Usikutane kimwili na mwanamke kisha na binti yake. Usikutane kimwili na binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, huo ni uovu.
18?? ?Usimchukue dada wa mke wako kuwa mke mwenza na kukutana naye kimwili wakati bado mke wako anaishi.
19?? ?Usimsogelee mwanamke ili kukutana naye kimwili wakati wa unajisi wa siku zake za mwezi.
20?? ?Usikutane kimwili na mke wa jirani yako na kujitia naye unajisi.
21?? ?Usimtoe mtoto wako ye yote awe kafara kwa mungu Moleki, kamwe usilinajisi jina la Mungu wako. Mimi ndimi BWANA.
22?? ?Usikutane kimwili na mwanaume kama mtu akutanaye na mwanamke, hilo ni chukizo.
23? ?Usikutane kimwili na mnyama na kujitia unajisi kwake. Mwanamke asijipeleke kwa mnyama ili kukutana naye kimwili, huo ni upotovu.'
 
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 21. Nilianza kuwasiliana na mwanaume nisiyemjua tangu mwaka 2013. Mwanaume huyu anadai ananipenda na nikimuomba hela ananitumia na anaponiambia tuonane moyo wangu unasita.

Nimemchunguza mpaka nimemjua kumbe ni mume wa mama yangu mdogo. Mimi sijawahi kwenda kwa mama mdogo. Nikimwambia ukweli kuwa wewe ni baba yangu mdogo na mkeo ni mama yangu mdogo anakubali ukweli huo.

Lakini ananiambia eti ananipenda na hayuko tayari kunikosa na kuwa yupo tayari kumuacha mama mdogo ili anioe na mimi nimetokea kumpenda nifanyeje?Tangu tuanze kuwasiliana sijawahi kuonana naye ila tunatumiana tu picha kwenye simu.

Naombeni ushauri.

Hivi unamsalimiaje mume wa mamako mdogo ? Haya kaolewe naye sijui utabadili hiyo salaam !! Au je, Mamako mdogo akija kukusalimia unamwita vile ?
 
We unaona sawa?

Mimi haiwezi ikanitokea ujinga km huo. Nikijua ni mume wa ndugu yangu nampiga chini fasta. Yeye kasema anampenda so atajua mwenyewe. Tunaweza tukaumiza kichwa kumshauri na asifate hata ushauri mmoja mzuri.
Ukimpenda mtu unachanganyikiwa na hakuna ushauri tofauti na akili yako inavyokutuma unaweza ukaukubali kiurahisi.
So mimi sina cha kumshauri
 
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 21. Nilianza kuwasiliana na mwanaume nisiyemjua tangu mwaka 2013. Mwanaume huyu anadai ananipenda na nikimuomba hela ananitumia na anaponiambia tuonane moyo wangu unasita.

Nimemchunguza mpaka nimemjua kumbe ni mume wa mama yangu mdogo. Mimi sijawahi kwenda kwa mama mdogo. Nikimwambia ukweli kuwa wewe ni baba yangu mdogo na mkeo ni mama yangu mdogo anakubali ukweli huo.

Lakini ananiambia eti ananipenda na hayuko tayari kunikosa na kuwa yupo tayari kumuacha mama mdogo ili anioe na mimi nimetokea kumpenda nifanyeje?Tangu tuanze kuwasiliana sijawahi kuonana naye ila tunatumiana tu picha kwenye simu.

Naombeni ushauri.
copy and paste...
Makala hii ipo kwenye gazeti la Nipashe la Jumapili
ya tarehe 08/11/2015
 
Una miaka 21 na umeanza kutaka kuchukua mume wa mama yako mdogo ivi mume wa jirani au shemeji yako utaweza kumuacha? maadili gani ulio lelewa? hukufundishwa kua mama yako mdogo ni mama yako pia? huyo ni sawa na Baba yako
sasa unaweza kulala na mzee wako? mtoto usikate tamaa mapema na jiamini kua atatokea atakae kua wako wa maisha...
 
Back
Top Bottom