mhhhm itabidi sasa avalishwe condom time analala :biggrin1:
muheshimiwa rafiki yangu nkadabwi nashauri aende hospitali afanye uchunguzi wa hayo magonjwa aliyoainisha mya kaka horsepower then ikiwa hana dalili au huo ugonjwa aende akaombewe kwa jinsi na mnamna anavyoamini yeye
sio tatizo dogo hilo ila for the time being kabla ya kupata tiba ya kudumu awe anategeshea alarm usiku kila baada ya saa 1 anaamka kukojoa labda itasaidia.
amesema KOLANI sio Qur'an..Jpange!
Asante AshaDii kwa ufafanuzi mzuri. Tunajaribu kuexplore njia mbali mbali kuiokoa hiyo ndoa. Hilo angalizo lako ni zuri, sikulifikiria kabla. Cha msingi huyo dada asikate tamaa. Kama laiweza kumvumilia kwa miaka kadhaa, si vibaya akaendelea kumvumilia huku wakitafuta njia mbali mbali za kusolve tatizo.
Mhhhm itabidi sasa avalishwe condom time analala :biggrin1:
sina uhakika sana ila nafahamu kuna baadhi ya magonjwa ambayo yanaweza kuchangia hili tatizo likiwepo
1. Diabetes
2. Urinary tract infection
3. Urinary tract stones
4. Prostate enlargement
5. Bladder cancer
6. Obstructive sleep apnea
7. Neurological disorders
na saa nyingine, acute anxiety or other emotional disorders (matatizo ya kisaikolojia). Lakini kama kuna mashaka ya imani za kishirikina ni vyema kuwaona viongozi wa dini kwa maombezi na ushauri zaidi.
Sidhani kama suala la kukojoa kitandani ni sababu tosha ya kupeana talaka. Anaweza kumfundisha mumewe kuwa msafi, na kuepuka kunywa vitu vya maji maji usiku kupunguza hatari ya kukojoa usiku. Huyo mume anaweza kutumia muda mwingi kufanya kazi zake usiku ili akichelewa kulala apunguze hatari ya kukojoa kitandani. Anaweza kuvaa hata pampas za wakubwa na akisha kojoa usiku avue na kuendelea kulala bila pampas.
Kumbuka kuwa huyo kaka hakuomba kuugua huo ugonjwa, na kuvunja ndoa kwa sababu ya hilo tatizo la ugonjwa ambalo linavumilika na linaweza kutibika ni kutomtendea haki. Mtie moyo na nenda au mshauri aonane na wataalam wa afya mara kwa mara kwa msaada zaidi.
sawa mkuu
mitihani migumu sana hii,tena mbaya zaid kwenye kutokea kwenye mahusiano ya ndoa
kwa mujibu wake anasema tatzo hili miaka kadhaa iliyopita mume wake hakua nalo
na ndio maana wanapata was was je kuna uwezekano pia kukawa na mambo ya ushirikina ndani yake?
aende kwa maombi; ni tatizo linalohitaji divine intervention hilo.
kama wamehangaika hivyo.. Nashauri wamwimbie kindumbwe ndubwe ataacha tu...
siamini kama hospitali wameshindwa kumsaidia.
Anyways, afanye kama alivyoshauriwa hapo. Kuweka alarm ya kuenda toilet hata kama kila baada ya masaa mawili, kuchelewa kulala na kuepuka pombe na vimiminika usiku.
Kuna zoezi la muscles linaitwa kegel's exercise. Anakojoa na kuubana mkojo kabisa kwa sekunde tano na kuuchia tena kidogo. Anarudia hivyo hadi amalize. Mwanzoni ni ngumu lakini akizoea itakuwa kawaida tu kwake. Hii itaimarisha misuli ya kibofu (sphincter muscles) na kumsaidia kwa mengineyo.
Ni mtihani lakini mkiwa wasafi wala haitawapa shida.
mhh! Jamani kweli kukojoa ndio iwe sababu ya ndoa kuwa mashakani? Kama ni mimi wala nisingemuhadithia mtu mambo ya ndani ya mume wangu, zaidi tungeshughulika kutatua sisi wawili na ingeshindikana ningekaa nae karibu zaidi nimuonyeshe mapenzi zaidi ili ajawe na amani maisha ya upendo yaendelee. Hivi yako wapi mapenzi siku hizi???