Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Kuna wanaume ambao hawataki kabisa kuona mke akiwa na uhusiano wa karibu na ndugu zake (mwanamke). Hataki kabisa kuona mkewe akionyesha kuwa na mshikamano mkubwa sana na ndugu zake. Inawezekana mara nyingi ni hofu ya mwanaume huyu kwamba mshikamano huo unaweza kumvurugia uhusiano wake na mkewe. Hakuna sababu inayoweza kuelezwa wazi kwamba ndio matokeo ya jambo hili.
Kutokana na hofu hiyo, mume hutunga sheria na kanuni ngumu akijaribu kuvunja uhusiano huo na ndugu zake. Lakini tabia hi huambatana pia na mume kutotaka mkewe kuwa na marafiki wa kike. Kila wakati atakuwa anawakosoa marafiki hao na mwisho atamkataza mkewe kufuatana nao bila kutoa sababu ya maana kuhusu kuwakataza kwake huko.
Kumbuka katika kupinga kwake uhusiano wa karibu kati ya mkewe na ndugu zake na marafiki atakuwa anajaribu kutumia kauli zisizofaa, na hata nguvu. ‘Ndugu zako wenyewe hawaeleweki, wanaonekana watu wa majungu tu,' atasema, au ' siku nikikuona tena na yule rafiki yako, utanitambua .' Na kweli anapomuona naye humtambua. Ni kweli kuna wanaume ambao hujaribu sana kadiri wanavyoweza kuwadhibiti wake zao.
Hufanya hivyo kwa kujigeuza kuwa mabosi badala ya kuwa waume. Unakuta mwanaume ndiye mwenye kauli ya mwisho kwenye kila jambo bila kuomba ushauri wala kuusikiliza, utakuta kazi yake ni kutoa amri bila kujali upande wa pili, yaani kujali kuhusu hisia za mkewe, atakuwa ndiye mwenye kufanya maamuzi yote yanayohusu familia bila kujali au kusikiliza upande wa pili. Mume wa namna hii huwa hayuko tayari kusikiliza maoni ya mwenzake wala ushauri.
Kutokana na hofu hiyo, mume hutunga sheria na kanuni ngumu akijaribu kuvunja uhusiano huo na ndugu zake. Lakini tabia hi huambatana pia na mume kutotaka mkewe kuwa na marafiki wa kike. Kila wakati atakuwa anawakosoa marafiki hao na mwisho atamkataza mkewe kufuatana nao bila kutoa sababu ya maana kuhusu kuwakataza kwake huko.
Kumbuka katika kupinga kwake uhusiano wa karibu kati ya mkewe na ndugu zake na marafiki atakuwa anajaribu kutumia kauli zisizofaa, na hata nguvu. ‘Ndugu zako wenyewe hawaeleweki, wanaonekana watu wa majungu tu,' atasema, au ' siku nikikuona tena na yule rafiki yako, utanitambua .' Na kweli anapomuona naye humtambua. Ni kweli kuna wanaume ambao hujaribu sana kadiri wanavyoweza kuwadhibiti wake zao.
Hufanya hivyo kwa kujigeuza kuwa mabosi badala ya kuwa waume. Unakuta mwanaume ndiye mwenye kauli ya mwisho kwenye kila jambo bila kuomba ushauri wala kuusikiliza, utakuta kazi yake ni kutoa amri bila kujali upande wa pili, yaani kujali kuhusu hisia za mkewe, atakuwa ndiye mwenye kufanya maamuzi yote yanayohusu familia bila kujali au kusikiliza upande wa pili. Mume wa namna hii huwa hayuko tayari kusikiliza maoni ya mwenzake wala ushauri.