Mulugo: Division Five haipo na sifuri ipo palepale

Mulugo: Division Five haipo na sifuri ipo palepale

Habari wanajopo!

Napenda sana na nifuraha yangu kukutana na mtanzania ambaya yuko wazi kwa mambo yake yanayopaswa kuwa wazi.hapo mwanzo niliandika andiko la hoja 15 za kujibu kwa yeyeto anayetaka urais wa tanzania 2015,

Hoja hii ilihusu ustawi wa elimu yetu,huwezi kuwa na elimu ambayo hailingani na mazingira ya ya taifda lako,kuna msuguano ambao hauna msingi wowote mara division 5 mara division 0,na mgongano huu unatokea kati ya watendaji wa chama kimoja na selikali moja-hii ni hatari kwa taifa.

Bwana jakaya hii inadhihilisha kwamba watendaji wako hawana umoja katika utendaji wao inawezekana vipi waziri apingane na katibu mkuu wa wizara yake?

Wananchi wa tanzania tunachotaka ni elimu inayotufundisha kuyamudu mazingira yetu ili tukapambane na kuendeleza taifa letu,hizo division zenu hazitusaidie sisi chochote,tunachotaka elimu ifanane na maisha yetu siyo,alama za juu kichwani ziro,alama za chini lakini kichwa iko sawa na anaishi maisha ya division one.

NB;ELIMU YETU HII KAMA IKIRUHUSIWA KILA ANAYE KUJA ANAKUJA NA MIPANGO YAKE TUTAJIKUTA SIKU HATUNA WALIMU WALA MADAKTARI MAANA WOTE WATAKUWA WA KUCHAKACHULIWA


Hoja inaendelea.......wadau endelezeni
 
Nadhani kiwango cha ufaulu ni kuchaguliwa kuendelea na masomo ya juu kama credits zinaruhusu ndio utaratibu unaotakiwa, vinginevyo mpango wa elimu ulivyobuniwa sasa ni bora zaidi kuwa na kifuta jacho cha wanafunzi kuwepo shuleni vinginevyo ni maumivu tupu wakati mtoto amahenya miaka minne hata mahudhurio tu ni sifuri wakati alikuwepo shuleni muda wote.

Mafanikio ya mwanafunzi shuleni si zile alama za masomo tu, kuna mengi ikiwemo ukomavu kiakili, kiutambuzi nk, sisi tunaona alama za asilimia tu.


Kwa mfumo wa kutoa vifuta jasho hatutafika.

Vyuo vikuu kusiwe na kufeli. Kuna wanafunzi mwaka wa tatu ama wa nne anafeli, anaondoka hapati hata cheti. Hapo inawezekana kafeli somo moja tu.

Na si lazima wote walioenda shule wafaulu. Wengine wanaenda shule kwa ajili ya kukuza mtaji wa kijamii (Social capital) tu.
 
Wanawachanganya tu wananchi na lazima 2jiulize ni kwanini hawa viongoz we2 wanafanya haya?
 
Nadhani kiwango cha ufaulu ni kuchaguliwa kuendelea na masomo ya juu kama credits zinaruhusu ndio utaratibu unaotakiwa, vinginevyo mpango wa elimu ulivyobuniwa sasa ni bora zaidi kuwa na kifuta jacho cha wanafunzi kuwepo shuleni vinginevyo ni maumivu tupu wakati mtoto amahenya miaka minne hata mahudhurio tu ni sifuri wakati alikuwepo shuleni muda wote.

Mafanikio ya mwanafunzi shuleni si zile alama za masomo tu, kuna mengi ikiwemo ukomavu kiakili, kiutambuzi nk, sisi tunaona alama za asilimia tu.
huo ukomavu wa akili uko wapi kama kashindwa mtihani. unadhani mtoto mwenye 'utambuzi na ukomavu kiakili' atashindwa kupata 50+% kwenye mtihani ambao kausomea 4yrs??

kuhusu credit; bado mwanafunzi atahitaji kuclear masomo yote ndio apate cheti
 
Kwa mfumo wa kutoa vifuta jasho hatutafika.

Vyuo vikuu kusiwe na kufeli. Kuna wanafunzi mwaka wa tatu ama wa nne anafeli, anaondoka hapati hata cheti. Hapo inawezekana kafeli somo moja tu.

Na si lazima wote walioenda shule wafaulu. Wengine wanaenda shule kwa ajili ya kukuza mtaji wa kijamii (Social capital) tu.

Nchi kama Marekani vyuo vikuu kuna program ya wanaoenda kusoma kwa ajili ya kupanua wigo wa uelewa na hiyo unayosema social capital na wengine kupata upambanuzi wa kitaalamu kwa shughulizao za kiuchumi, teknolojia na maisha ambapo mhitimu hutunukiwa cheti cha uhitimu bila mchanganuo wa credits, utaratibu ambao unasaidia wengi kwenda kujiendeleza, hata kuna wanaosoma wako above 50 years old.
  • Kwa vyo vyote hata siku moja vigumu uwezo wa watu darasani ukawa sawa,
  • Kufaulu katika masomo mashuleni au vyuoni si uwezo wa wafaulu katika maisha
  • Mahudhurio ya darasani pengine wanashindwa mitihani kiakili huwa wameelimika zaidi
  • Tukubali kusoma mafanikio si kupata alama za juu tu
  • Kusoma kunamkuza mtu katika mengi na tuna ushahidi wengi wasiopata alama za juu wabadili maisha kuliko walioonekana wana uwezo sana madarasani
Anayehitaji kusoma zaidi hasa baada ya degree ya kwanza ni kwa wale ambao wanahitaji zaidi kusaidiwa kuwapanua ubongo ndio maana huko yanayomsaidia mwanafunzi si kama shule ya msingi, sekondari au bachela, bali ni majadiliano na kushindana kwa hoja kitu kinachomsaidia mtu kupanua wigo wa kufikiri, kuchanganua mambao, kupambanua mambo, kutofautisha mambo, kujenga utetezi, uwezo wa kufikiri kupima na kuamua, kuelewa yaliyopo na kupima ayatumieje katika maisha kujenga future nk.

Tumeshuhudia wataalamu na wabunifu mbalimbali kama yule aliyefariki karibuni mmoja wa waanzilishi wa apple hayati Steve alienda chuo akaamua kuacha na kurudi kufanya mambo yake, maana aliona anachojifunza chuoni ni kumpotezea muda alipolinganisha na alicho nacho ubongoni mwake. Nadra sana kupata watu kama Thomas Edson au Steve waliohitimu hadi PHD. Ajabu wamefanya makubwa na sisi tunasomea mambo yao hadi tunakuna vichwa vibaki upara tu na kubakiza chache karibu na masikio kushikiza miwani.

Kuna mada naiandaa kuhusu suala hili la elimu inakuja kuelezea watu wanaofikiria CV ndizo zinafanyakazi badala ya uwezo wa mtu, maana haya tunayohangaikia shuleni na vyuoni waliovianzisha wahakupitia shule ila toka bongoni mwao, hivyo tujue tunao watu wa aina hiyo siku zote maishani mwetu.
 
huo ukomavu wa akili uko wapi kama kashindwa mtihani. unadhani mtoto mwenye 'utambuzi na ukomavu kiakili' atashindwa kupata 50+% kwenye mtihani ambao kausomea 4yrs??

kuhusu credit; bado mwanafunzi atahitaji kuclear masomo yote ndio apate cheti

Tulia kwanza jifunze maisha kabla ya kuanza kuwalaumu watoto wanaoshindwa kupata alama za juu.

Shule zetu hazina kitengo cha wataalamu wa saikolojia, wanafunzi wengi hushindwa kwa woga, kutojiamini na labda baadhi bongo lao halijajikita katika uchanganuzi wa mambo ya darasani. Mitihani yetu haitungwi kwa alengo ya kuwafaulisha watoto bali kuwakomoa na tungali na mfumo ule wa wachache wafaulu kama enzi zile tulipokuwa na shule chache.

Ukitaka kujua hilo, angalia hawa waliojiona wamesoma wenyewe wanapopewa kazi wanavyovulunda kuliko wale ambao hawakufikiwa kiwango chao, tatizo tunaona alama za darasani bila kupima uwezo wao kiakili wamekomaaje, wanawezaje. Nchi zilizoendelea licha ya hizo CV kuna qualifying test kupima uwezo wa mtu hata utendaji wake, sisi tumejaza wenye CV mambo ovyo kabisa.

Kwanza pima mwenyewe uliyoshindwa katika maisha yako na uliyofaulu, kwa nini mengine umeshindwa? Yalipokushinda ukajaribu mengine. Hata darasani kuna masomo ambayo hayakupanda ukaamua kuchukua mchepua ambao unaona kutakuwa na mtiririko mzuri.

Binadamu tuna maumbile ya ubongo unaofanana lakini kila mmoja anapishana na mwenzake jinsi uwezo wa ubongo huo navyoweza kufanya kazi. Hata hapa tunapoandika majadiliano uwezo wa kuandika na kuchanganua mada hii tofauti kiwango chako na changu inayotokana na uwezo wa ubongo wa kila mmoja na ndio maana kila mmoja anakuja na lake.
 
huo ukomavu wa akili uko wapi kama kashindwa mtihani. unadhani mtoto mwenye 'utambuzi na ukomavu kiakili' atashindwa kupata 50+% kwenye mtihani ambao kausomea 4yrs??

kuhusu credit; bado mwanafunzi atahitaji kuclear masomo yote ndio apate cheti
2010-11-06-Kikwete-Obama-01.jpg Obama VS Kikwete View attachment 119872
Hakujipanga kabla ya kuzungumza na kiogozi mwenzake
hadi asome karatasini mstari kwa msitari?
Jibu: uwezo wa kila mtu unavyoruhusu ndicho kinachoendelea

Angalia picha ya hao wawili Obama na Kikwete wote wamepitia vyuo vikuu, Obama anamimina ya kwake toka ubongoni kama manyunyu ya mvua wakati Kikwete pamoja na kusoma tu karatasini anapata kigugumizi cha kutamka hadi Obama anashika tama na kujaribu kujikaza kumsoma apate kumwelewa. Wote hao wameelimika na wanavyeo vya juu vinavyofanana lakini uwezo wa ubongo wanatofautiana, kumbuka ubongo wao unafana licha ya kutofautiana uwezo.
 

Attachments

  • images.jpg
    images.jpg
    9.1 KB · Views: 53
Hii Wizara kweli inaendeshwa na wendawazimu......Hadi prof kaingia kichawa kichwa sasa naona washamwingiza choo cha kike. .........Nadhani kuanzia sasa atakua amejifunza kuwa siasa hazina darasa.
 
Kwa mtazamo wangu naona kama hawa walikuwa wameshakubaliana kama wizara then wakaona watu wanapinga / wanaponda sana huo uamuzi.. Katika kuua soo wakakosea tena; badala ya kumwambia Prof akakanushe / akarekebishe mwenyewe, wakaamua kumtuma Mlugo akalikoroge zaidi... Hii kwa mtazamo wangu ni aibu kwa wizara na inashusha morale ya watu walioko kwenye wizara. Kama mmekubaliana hata kama ni utumbo then, mkamtuma mmoja wenu akatoe tamko, then mnakuja kulipinga tena kwenye press sidhani kama ni sahihi....

Ni maoni yangu tu.
 

Shule zetu hazina kitengo cha wataalamu wa saikolojia, wanafunzi wengi hushindwa kwa woga, kutojiamini na labda baadhi bongo lao halijajikita katika uchanganuzi wa mambo ya darasani.


Sasa hayo ndiyo mambo yaliyopaswa kutiliwa mkazo na siyo kuja na mfumo upya wa alama! Hayo mambo uliyoyasema ndiyo chachu ya kuiinua elimu yetu. Pia kitengo cha career guidance ni muhimu kuwa nacho katika shule zetu za msingi na sekondari. Hivyo kutamfanya mwanafunzi atambue mapema yeye uwezo wake umejikita katika fani/taaluma ipi. Hapo ndipo atakaongeza bidii zaidi katika hiyo fani/taaluma. Huwezi kumlazimisha kila mwanafunzi awe injinia, wengine ni wachoraji!!


Hayo pamoja na mengi (walimu, maabara, vifaa vya ufundishaji, vitabu n.k.) yaliyosemwa juu ya kuboresha elimu yetu, ndiyo ya kutiliwa mkazo. Na si alama na madaraja mapya.

Mitihani yetu haitungwi kwa malengo ya kuwafaulisha watoto bali kuwakomoa na tungali na mfumo ule wa wachache wafaulu kama enzi zile tulipokuwa na shule chache.

Chifu, sidhani kuwafaulisha wanafunzi ndiyo sababu ya kuwepo kwa mitihani. Mitihani ipo kwa ajili ya kupima uelewa wa mwanafunzi kwa kile alichofundishwa darasani na kile kinachofanyika kwa uhalisia katika maisha ya mwanadamu.

Chifu watoto hawawezi kufaulu kama hakuna mazingira katika shule zao, ya kuwafanya wafaulu.

Mitihani haiwezi kutungwa kwa kukomoa; wanataka kumkomoa nani? Kwa watungaji hao hao, wana watoto, ndugu zao na watoto wa ndugu zao wanaofanya mitihani hiyo hiyo!! Sasa mzazi anaweza kumkomoa mwanaye?!? Hii ni sababu itolewayo na wanafunzi waliosoma katika mazingira yasiyowawezesha kufaulu. Mitihani inatungwa bila kuangalia kama mada zilizotungiwa mitihani zilifundishwa ama la! Sasa mwanafunzi akikutana na maswali kutoka kwenye mada kama hizo, ndipo anapoanza kusema amekomolewa!! Kumbe ni udhaifu wa mfumo wa ufundishaji!!
 
Tulia kwanza jifunze maisha kabla ya kuanza kuwalaumu watoto wanaoshindwa kupata alama za juu.

1] Shule zetu hazina kitengo cha wataalamu wa saikolojia, wanafunzi wengi hushindwa kwa woga, kutojiamini na labda baadhi bongo lao halijajikita katika uchanganuzi wa mambo ya darasani. Mitihani yetu haitungwi kwa alengo ya kuwafaulisha watoto bali kuwakomoa na tungali na mfumo ule wa wachache wafaulu kama enzi zile tulipokuwa na shule chache.

2] Ukitaka kujua hilo, angalia hawa waliojiona wamesoma wenyewe wanapopewa kazi wanavyovulunda kuliko wale ambao hawakufikiwa kiwango chao, tatizo tunaona alama za darasani bila kupima uwezo wao kiakili wamekomaaje, wanawezaje. Nchi zilizoendelea licha ya hizo CV kuna qualifying test kupima uwezo wa mtu hata utendaji wake, sisi tumejaza wenye CV mambo ovyo kabisa.

3] Kwanza pima mwenyewe uliyoshindwa katika maisha yako na uliyofaulu, kwa nini mengine umeshindwa? Yalipokushinda ukajaribu mengine. Hata darasani kuna masomo ambayo hayakupanda ukaamua kuchukua mchepua ambao unaona kutakuwa na mtiririko mzuri.

Binadamu tuna maumbile ya ubongo unaofanana lakini kila mmoja anapishana na mwenzake jinsi uwezo wa ubongo huo navyoweza kufanya kazi. Hata hapa tunapoandika majadiliano uwezo wa kuandika na kuchanganua mada hii tofauti kiwango chako na changu inayotokana na uwezo wa ubongo wa kila mmoja na ndio maana kila mmoja anakuja na lake.
1]i used to panic, so i asked my class teacher kwa ushauri na akaniambia jinsi ya kutulia kwenye mtihani na ilinisaidia.
2] hiyo ni lack of practical experience, hata miye nilipoanza kazi kuna mengi sikujua ambayo waliosoma chini yangu wanayafahamu. pia mindset ilikuwa tofauti since nilikuwa najaribu ku-copy/paste vya darasani to the office. hii iliisha baada ya muda mfupi. issue ya QT iwekwe kazini/vyuoni sio mashuleni.

3] i can't do everything, i'm just human.

4] nakuunga mkono hapo. ingekuwa vizuri if we had various methods of examination/assessment.
 
Zuzu moja alikuta kinyesi barabarani, aksema kile si kinyesi kweli? Akasema ngoja nionje nione kama nichenyewe, basi akaonja akagundua nichenyewe akasema AFADHALI SIKUKANYAGA
 
Mh Mulugo, a.k.a Mr #Tan_Zimbabwe , amekuwa akinukuliwa mara kwa mara akijitetea kwamba wao (Wizara ya Elimu) hawajashusha viwango vya ufaulu bali walichofanya ni 'kuongeza wigo wa ufaulu'. Mimi sijamuelewa kabisa na wala simuamini huyu mtu. Kwanza kauli zake nyingi ni tata--juzi wamefuta division 0 na kuanzisha division 5 lakini jana bwana TanZimbambwe ameibuka na kukanusha kwamba hawajawahi kuanzisha division 5. Maajabu ya Musa haya!

Utata:

1. Utaongezaje wigo wa ufaulu bila kushusha alama za ufaulu? Je, kushusha viwango vya ufaulu SI sawa na kupanua wigo wa ufaulu?

2. Je, Mulugo na wasanii wenzake wanaposema kwamba 'wamepanua wigo wa ufaulu' kwa sababu ya kuondoa 'murundikano' katika madaraja ana maana gani? Kwa jinsi nilivyomuelewa ni kwamba wanafunzi wengi walikuwa 'wanarundikana' (wanafeli) katika madaraja ya 3 na 4, hivyo Wizara 'imepanua' wigo wa ufaulu kwa kushusha alama za daraja la 3 hadi pointi 47! Mwanafunzi akipata pointi 47 anakuwa amepata daraja la 3 na anaenda sekondari. Haya ni maajabu ya Musa!

3. Pia Mulugo kadai kwamba ufaulu wa alama B umevunjwa mara mbili--B flat (B) na B plus (B+). Sababu aliyotoa ni kwamba lengo la kufanya hivyo ni kupunguza 'mrundikano' wa wanafunzi waliokuwa wanapata alama B. Kumbe wanafunzi wengi wakipata alam B ni tatizo? Ina maana kwamba wanafunzi wanaopata alama B wanasomea kwenye vyumba vya madarasa vilivyogawanywa sawa katika madaraja (A, B, C, na D) kwa maana kwamba wale wenye alama B walikuwa wengi hivyo wakawa wanarundikana mno kwenye madarasa yao? Kama sivyo, je kuna tija gani ya kitaaluma ya kugawanya alama hiyo kuwa B na B+ kama sio umburula tu?

Jamani, mimi sijamuelewa kabisa huyu TanZimbabwe. Kama kuna aliyemuelewa, atufafanulie tafadhali.
 
TOPIKI HII NAOMBA ISIUNGANISHWE NA NYINGINE MAANA INA MAAUDHUI TOFAUTI SANA NA ZILIZOJADILIWA.
UTEKELEZAJI WA MABADILIKO YA UPANGAJI WA MATOKEO YA SEKONDARI USITISHWE MARA MOJA.
Maamuzi ya kufanya mabadiliko katika alama za ufaulu na madaraja ni uamuzi uliokosa weledi na umakini.

Elimu yetu ina matatizo lukuki na inatakiwa kufanyiwa reform na si kudonoadoa tu tena pasipostahili.
1.mabadiliko yote yaliyofanywa hayatatui wala hata tatizo moja la kimfumo kwenye elimu yetu.
2.mabadiliko yaliyofanywa hayatasaidia kuondoa tatizo la wanafunzi kuanza kidato cha kwanza wakiwa hawajui kusoma na kuandika na wanaendelea mpaka kidato cha nne bado wakiwa hawajui kusoma na kuandika. Huu ni mfumo wa ajabu kabisa mana walimu wa sekondari nao wameshindwa kumwelekeza huyo asiyejua kusoma na kuandika na mbaya zaidi mfumo unamruhusu ama haumubaiani mpaka anafika kidato cha nne.haya ndio mambo ya kushughulikia.
3. mabadiliko haya hayajibu wala kuondoa tatizo la wanafunzi kwa sasa kushindwa kuielewa lugha ya kufundishia(kiingeleza) tofauti na zamani ambapo hata wale wazee waliokomea la nane walikimudu sawa sawa kiingeleza na hakukuwa na malalamiko kuwa lugha ni tatizo.
4.mabadiliko haya hayajibu wala kutatua tatizo la utungwaji na uidhinishaji wa vitabu vibovu na vya hovyo kutumika mashuleni tena vikiwemo na vya serikali mf kitabu cha hisabati kidato cha pili toleo jipya ni kitabu cha hovyo kabisa.
5.mabadiliko haya hayajibu wala kuondoa tatizo la wanafunzi kukosa uwezo wa kujieleza na kufanya kazi.
6.mabadiliko haya hayajibu wala kutatua tatizo la elimu yetu kushindwa kulisaidia taifa kupiga hatua kwenye sayansi na hatimaye mapinduzi ya viwanda.
7.mabadiliko haya hayajibu wa kutatua tatizo la mitihani kutungwa nje ya mihutasari(sylubus).
8.mabadiliko hayo hayajibu wala kuondoa tatizo la mitihani inayojibika kwa muda mrefu kuliko muda unaopangwa mf mtihani wa masaa matatu unahitaji masaa sita kuujibu.
8. mabadiliko haya hayajibu wala kuondoa tatizo la wanafunzi kukaa bila kusoma na wala kufundishwa tokea kidato cha cha kwanza hadi kidato cha nne bila kusoma hata topiki moja katika somo husika na wanapaswa kujibu mtihani sawa na aliyesoma na kufundishwa topiki zote.
9.mabadiliko haya hayatatui wala kuondoa tatizo la kukosekana kwa utunzi wa vitabu hapa nchini kwa ngazi ya kidato cha tano na sita katika masomo ya sayansi.

Kitu kibaya zaidi katika maamuzi haya ya alama na madalaja.
1. Mabadiliko haya hayajahusisha wadau wa elimu huku katibu mkuu akiamua kudanganya wazi wazi kuwa wadau walihusishwa,wakati waziri mkuu anaunda tume ilitegemewa kuwa tume ya waziri mkuu ingeweka wazi chanzo cha ubovu wa matokeo na ndipo serikali wangetutaka kufanya ama kutoa maoni ya kufanya EDUCATION GENERAL REFORM na mwisho hoja zingejadilika juu ya mapendekezo mengi na mwisho maamuzi yangeafikiwa.badala yake majibu ya panda wamekaa nayo na wakajipa maamuzi ya kuleta mabadiliko ya ajabu kabisa.
2. Hakuna chuo chochote mpaka sasa kinachojua ni alama zipi kati ya hizi mpya zinafaa kudahili mwanafunzi katika kozi ipi,ngazi ipi,ni kwa matokeo yapi mwanafunzi aka-resit kupata sifa ya kusoma kitu Fulani,mathalani inajulikana D tatu(D D D ) hazitoshi kumfanya mtahiniwa apate sifa ya kwenda kidato cha tano lakini wanajua anaweza kusoma certificate Fulani,sasa mfano atakaepata E tatu(E E E) hakuna chuo kilichojiandaa wala kujua ana qualify kusoma nini?pia kama daraja la nne la pointi 26,28,29 nk halikumfanya mwanafunzi kwenda advance lakini sasa daraja kwa pointi hizi si la nne tena bali daraja la tatu.
3. Mabadiliko haya hayajafanyiwa majaribio maana wamekurupuka sana na kuyafanya kuwa maamuzi ya dharura,utaendaje kutumia mfumo mpya katika mtihani wa mwisho kidato cha nne kwa wanafunzi ambao kwa miaka yao yote minne shuleni waliandaliwa kwa mfumo wa zamani.
Hapa tunajaribu makali ya panga kwenye shingo za watu, tutegemee wengi kuathirika,wenye matokeo watayasheherekea lakini hawa wataalamu wa baadae watakaotolewa katika mfumo huu ndio watakaoleta balaa katika kazi zao na athali zitakuwa za jamii yote,ikumbukwe maamuzi ya crash program(walimu wa bodaboda waliohitimu ualimu ndani ya miezi miwili),maamuzi ya mungai kuondoa masomo ya bishara na kilimo,maamuzi ya kuondoa mchujo kidato cha pili.
Haya ni baadhi ya maamuzi machache yaliyogharimu elimu na taifa.

HOJA ZILIZOTUMIKA NI KUFANYA MABADILIKO NI HOJA NYEPESI KWELI.
1. Utofauti wa miundo katika mitihani kati ule muundo wa Baraza la mitihani la taifa unajulikana kama FLEXIBLE GRADE RANGES yaani pamoja nakusema kuwa A inaanzia 81 baraza wanaweza kubadilisha kutokana na matokeo na kuamua ama A ianzi 70 ama 85 ama 90, na ule muundo wa unatumika katika mashule unaojulikana kama FIXED GRADE RANGES yaani mashuleni A inabakia kuwa 81 mpaka 100 bila kuajali matokeo yapoje.je hili nalo limewahi kuwa tatizo?limewahi kujadiliwa?
2. Utofauti wa alama za ufaulu zinazotumika kati ya kidato cha nne na kidato cha sita wakati elimu ni ileile ya sekondari.
Yaani Olevel kuna A,B,C,D na F wakati Alevel kuna A,B,C,D,E,S na F pia hata marks zinatofautia mfano kwa O level 81 mpaka 100 ni A wakati Alevel 75 mpaka 100 ni A.sasa hizi hoja tujiulize ni lini zimewahi kuonekana ni tatizo?ni lini zimewahi kujadiliwa?je ni tatizo kweli?
 
Mfumo mpya wa ufaulu: ni upi una manufaa kwa kongeza tija katika elimu: DIV V ya Prof Mchome au DIV ZERO ya Le Prof Mulugo (Tanzania ni muungano wa Tanganyika na visiwa vya Zimbabwe- mwanamotapa)?

Cha msingi wanafunzi wanatakiwa wapate elimu bora sasa hiyo div 0 ibadilishwe iitwe v haibadilishi maana; kufeli ni kufeli tu!
 
Back
Top Bottom