feyzal
JF-Expert Member
- Apr 20, 2016
- 8,552
- 17,248
CCM ni wale wale tena leo hii press binafsi sijaona alichoongea kinachoshtusha zaidi ya kung'ata ng'ata maneno na kuona aibu. Pole pole ni kansa usaliti unamtafuna siwezi kumuamini kama alivyo Zitto Zuberi Kabwe.Hajasema sheria za chama, kasema desturi za chama.
Yeye haamini katika sheria za chama ( KATIBA).
Ndo maana kasema kidesturi kuna watu hawaruhusiwagi na CCM kupanda kuwa Rais, yani Spika, PM, na VP.
Lakini katiba ya CCM inasema mwanachama yeyote anaweza kugombea chochote.
Sheria iliyoandikwa kwenye makaratasi kwa Mwafrika ni kitu kigeni, kigumi, kinamkera sana Mwafrika
Sheria ya kwanza Uingereza ilitungwa mwaka wa 1215. Tunahotaji miaka 800 ka.a wao ili tuelewe sheria ni nini.
Sawa kabisa, ni kweli kabisa haya yaliasisiwa na kina Magufuli.
Je hawa wa sasa, do they get a pass ( yani wanapeteshwa, wanasameheka) kwa saab eti hawakuyaanzisha?
Tena wanayaendeleza kwa moto mkali zaidi. Watu wananyopolewa vitandani mbele ya wake zao hapo hapo sebuleni wanapigwa rungu puuuuu, wanakuburuza nje, kwenye basi la abiroa mchana kweupe mjini sio shambani, watu wanaitwa polisi wafate mali zao, wanapotea jumla.
Hapo unasemaje mimi sijayaanzisha lakini unayaendeleza na moto ule ule au zaidi ???????