Muhongo anaivuruga TANESCO, Magufuli yuko wapi?

Muhongo anaivuruga TANESCO, Magufuli yuko wapi?

Usiwe unatazama mambo kwa roho ya kimasikini

Wafanyakazi wa Tanesco huo umeme ni jasho lao
ukifanya kazi Daily News gazeti hununui
ukifanya kazi tigo au voda airtime hununui
iko dunia nzima

hata wapiga debe tu daladala hawalipi nauli.....
tangaza maslai yako na tanesco mkuu, maana inaelekea kuna mrija wako umekatwa na profesa. Haaaaaaaaaaaaaaa.
 
Yapo Mengi tu....
anachofanya na vurugu......
Kama kuna management conflicts mbona ni vitu vya kawaida kwenye kazi au hamjawahi kuwa managers? Iteni vikao vya management na mumueleze matatizo yake yeye ni binadamu ataelewa na aterekebisha ikishindikana basi toeni ripoti kwa mwajiri wake kuliko kuleta majungu mtandaoni.
Analeta siasa tu kwenye mambo ya kitaalam....
halafu lawama iwashukie Menejimenti
 
Watu wachache watakuelewa
watu wanafikiri kutangaziwa bei imeshuka basi ndo mafanikio...
mtu hajawahi kuongoza hata nursery school leo ajifanye CEO...
unafikiri hata tukisema atakusikiliza?Magufuli alishampa kibuli siku hile ya uzinduzi wa Kinyerezi II!
 
Mkuu fuatilia tu media
hata Tanesco kupunguza bei ya kuunga umeme lilikuwa agizo lake
kwa masharti kuwa serikali itatoa ruzuku
ni kweli inatoa ruzuku but haitoshelezi
na ina maana kuwa Tanesco isijiendeshe kwa faida na isijitegemee
isshi kwa ruzuku......na mwisho ndo hayo kwenda kukopa na deni kuongezeka....

soma hata ile hotuba ya Zitto siku ile anafunga ishu ya Escrow
aliitaja deni la Tanesco before Muhongo lilikuwa bilioni 50
now zaidi ya bilioni 300....

Now ameteuliwa tena na Magufuli anakuja na maagizo tele ya dizaini hiyo
Haya matatizo ya Hiyo loss unayo ongelea sio kutokana na uamuzi wa Prof Mhongo , Bali ni kutokana na mikataba mibovu iliofungwa kwa Tanesco kabla Prof hajawa waziri , hivyo kusema ni due to his Presence au maamuzi yake. Ni uwongo , na kutumia Zitto Kama reference hakufanyi Hiyo statement kuwa kweli.
 
Unamtuhumu Muhongo,lakini unashindwa kuleta hizo tuhuma unadai watu wafuatilie media,sasa hii mada umeileta ya nini ?

TANESCO iko chini ya wizara ya Nishati na Muhongo ndio waziri wa Nishati anaingiliaje wakati ndio wizara yake ?

Umeona Prof. Magembe alichofanya TANAPA ?
Umeona Prof Mbarawa alichofanya TTCL,TRL,TCRA ?
Umeona Prof Ndalichako alihofanya NECTA,TCU ?

Kuna tofauti gani na anayofanya Muhongo,kama kuna issue nyingine ni bora uiseme kuliko kuleta tuhuma na unashindwa kuzielezea

Mkuu siamini kama huna elimu hata kidogo ya menejimenti
mameneja wa mikoa na wilaya waripoti kwa waziri we unaona ni sawa?
Waziri kutoa maagizo kwa njia ya simu ni sawa?

hivi labda nikuulize wewe ndo meneja wa wilaya au kanda wa Tanesco
ceo wako akupe maagizo ya nenda kushoto na waziri aje aseme nenda kulia
we unaonaje? ni sawa?

Mawaziri wengine hao wanatimua na kuweka watu wengine....hawafanyi daily tasks...kama Muhongo
Muhongo hajatimua mtu ni kuwapa maagizo yake tu daily
 
ruzuku haitoshi huku wafanyakazi wa tanesco wakipeana umeme unit 700 kwa mwezi kwa shilingi elfu 10 tu...

yaani ukiajiriwa tanesco ukitoa elfu 10 unapewa unit 700 za umeme... na hapo hapo shirika linategemea serikali iwape ruzuku... kiukweli watanzania hatuna.shukrani.... tanesco ni jipu kubwa sana na najua mhongo akisaidiana na mwenzake wa kanda ya ziwa jemedari mkuu lazima walitumbue tu... tuwape muda... tanesco haimalizi huu mwaka na management hii hii ya kaskazini iliyozea ujanja ujanja
umejiekeza vizuri sasa hiyo kaskazini inahusiana vipi ?
 
Hivi watu mnaowatetea hao tanesco kuna lipi la kujivunia tokea imekuwepo? Bora shirika life tu maana hakuna lolote la maana wanalojua. Kila siku kulalamika tu nazani ndo shirika la hovyo na wafanyakazi wa hovyo Tanzania. washenzi sana hao tanesco
 
Kama kuna management conflicts mbona ni vitu vya kawaida kwenye kazi au hamjawahi kuwa managers? Iteni vikao vya management na mumueleze matatizo yake yeye ni binadamu ataelewa na aterekebisha ikishindikana basi toeni ripoti kwa mwajiri wake kuliko kuleta majungu mtandaoni.

We umewahi fanya kazi na Muhongo?
lini alielezwa kitu akaelewa?

JF ni public forums.....hapa hata Waziri Ndalichako uwaziri wake ulianzia hapa kupigiwa debe
haya sio majungu .....mengi tuliyo yaongea kuhusu Muhongo huko nyuma yamewafikia mabosi wake na walimrekebisha
 
sio kweli kila mfanyakazi wa voda au tigo hanunui vocha.. wanaopewa vocha ni wachache sana ambao kazi zao zinahitaji airtime allowance. na hiyo ni kampuni zote hata tanesco nina imani wapo wanaopewa vocha na shirika... na hawapewi hizo vocha sababu wanafanya kazi voda.. bali wanapewa sababu zinatumika kutimiza majukum yao kazini..

je mfanyakazi wa tra anasamehewa kodi yoyote??

Usiwe unatazama mambo kwa roho ya kimasikini

Wafanyakazi wa Tanesco huo umeme ni jasho lao
ukifanya kazi Daily News gazeti hununui
ukifanya kazi tigo au voda airtime hununui
iko dunia nzima

hata wapiga debe tu daladala hawalipi nauli.....
 
Mkuu fuatilia tu media
hata Tanesco kupunguza bei ya kuunga umeme lilikuwa agizo lake
kwa masharti kuwa serikali itatoa ruzuku
ni kweli inatoa ruzuku but haitoshelezi
na ina maana kuwa Tanesco isijiendeshe kwa faida na isijitegemee
isshi kwa ruzuku......na mwisho ndo hayo kwenda kukopa na deni kuongezeka....

soma hata ile hotuba ya Zitto siku ile anafunga ishu ya Escrow
aliitaja deni la Tanesco before Muhongo lilikuwa bilioni 50
now zaidi ya bilioni 300....

Now ameteuliwa tena na Magufuli anakuja na maagizo tele ya dizaini hiyo
The Boss, I hope wewe ni mwajiliwa wa Tanesco. Au!... Kwa nafasi yake niliamini anafanya hayo yote baada ya mawasiliano ya ndani na menejiment. Kama sivyo kunaweza kuna tatizo lakini pia hali ya taaisi za serikali ilivyokuwa inaendeshwa inatia mashaka.

Bodi za wakurugenzi zilikuwa ni vikundi vya makubaliano ya mambo ya kipuuzi kabisa yenye maslahi kwao wana bodi. Hayo ni kote tangu NSSF, PPF, PSPF, TBS, TPDC, Universities, etc. etc. Kwa mwanasiasa ambaye ndo anayekuwa punching bag kuitetea Tanesco kule Bungeni, inakuwa aibu kubwa kuanza kusema hayo ni maamuzi ya menejimenti. Huyo CEO inafikia hatua huwezi kumuamini kumuachia aamue anachotaka.

Kwa hizo ruzuku pia namtetea kiasi. Yaonekana Tanesco wanataka kuendesah shirika bila investment. Kukiwa na ongezeko la mahitaji wao wanasukuma gharama kwa watumiaji badala ya wao kuweka mtaji na baadaye wapate faida. Watumiaji wanachangia REA wakati hiyo kwa Tanescvo ni investment na baadaye watakaopata faida siyo wachangiaji, ni Tanesco!

Tanesco itapata faida baada ya kuongeza idadi ya watumiaji umeme. Hao watumiaji umeme wataongezekaje kama unaweka gharama ambazo ni exorbitant! Mbona mbinu ni rahisi. Hata konda anakudai nauli baada ya kuwa umepanda na kuondoka kituoni.
 
Usiwe unatazama mambo kwa roho ya kimasikini

Wafanyakazi wa Tanesco huo umeme ni jasho lao
ukifanya kazi Daily News gazeti hununui
ukifanya kazi tigo au voda airtime hununui
iko dunia nzima

hata wapiga debe tu daladala hawalipi nauli.....
Kama ni hivyo mwalimu akifundisha sekondari mtoto wake asilipe ada ya Wizara? Ukiwa daktari au mfamasia madawa bure tuu! Hizo analyses ni ngumu kuzihalalisha.

Tatizo muliko kwenye mashirika yanayopokea pesa za wateja munadhani ndo munaendesha nchi. Kuna watu wako ktk kazi muhimu sana kuliko hizo lakini hawapokei pesa kwa huduma yao kwa mteja. Nimekwishatoa mfano wa zimamoto anavyojitoa mhanga, au nesi anavyokusafisha na kipindupindu yako. Angalia risk kwake halafu wewe utetee kupata umeme wa bure kama mfanyakazi wa Tanesco!
 
Kwani nani mwenye mwenye final say kati ya CEO na Waziri, mwachine Prof. afanye kazi zake kadri anavyo ona inafaa - nyie mna mamlaka gani ya kumkoromea Prof.Muhongo, mmezoe kufanya mpendavyo bila ya kuratibiwa na mtu yoyote, mnalifanya Shirika la umma kama la watu binafsi/ukoo - akija mtu mwenye strategy tofauti na yale mliozoea - mfano Prof.Muhongo basi mnajengea majungu, lawana na mambo ya kubuni tu.

Mtu aliye kwenda shule anaweza kuja hapa na kudai eti Prof.Muhongo anataka kubinafisiza kitengo cha uzalisha umeme - nani kawambieni kwamba shirika moja la umeme kujishughulisha masuala yote ya uzalishaji umeme,usafirishaji umeme na usambazi umeme ndiyo njia sahihi ya ku run Tanesco - upuuzi huo unafanywa hapa Tanzania tu, ndio maana Tanesco anagubikwa na matatizo lukuki kutokana na Shirika kuwa kubwa mno ukiongezea na urasimu na wizi.

Dk.Magufuli akishirikiana na Prof.Muhongo walivunje Shirika laTanesco na kulijenga upya liwe na kampuni tatu tanzu zinazo jitegemea namely: Power generation, Power transportation na Power distribution - Mataifa ya Ulaya na Marekani ndizo mbinu wanazo zitumia katika sekta ya umeme - sisi hapa tunakuja na majungu ya kumsema sema Prof. eti hafai!! Kisa? anataka kubinafisisha kitengo cha uzalishaji!

Mnajifanya mmesahau kauli ya Dk.Magufuli - alisema hatasikiliza majungu kuhusu Prof.Muhongo au mnafikiri alikuwa anatania - anatujua baadhi yetu tulivyo wanafiki na wazushi.
 
Wanaomsifia Muhongo sijui wana-share nini nao.Nilimdharau baada ya kuanza kutoa majibu ya hovyo kwa Mnyika mtu kama yeye Prof.
 
Tanesco ni kati ya mashirika yanayoendeshwa na wajinga sana kama siyo wapiga dili wakubwa sana wanaotufanya tusiendelee.

Kati ya watu wa kubadilishwa wote kama ingewezekana wafanya kazi wa Tanesco hasa wenye maamuzi katika shirika.

Madili makubwa yako huko.

Kama akina iptl.agreco na wengine bado wanalipwa na tanesco wakati hakuna mabadiliko ya upatikanaji umeme ni upumbavu kuwatetea menejiment iloshindwa kazi. Ikija mikataba feki na ya kinyonyaji ni wao nso wanaongoza..eti unaitetea management ya Tanesco?

Shirika limefungwa na minyororo mikubwa hata Rais hadiriki kugusa kwa maalahi ya nchi kisa watu wachache wametumia akili yao kuingia mikataba ya hovyo kuwanufaisha!!

Leo wanadiriki kuitangazia uma kwamba Tanzania matumizi kwa sasa ya umeme ni megawat 1030 wakijitapa wanazalisha umeme zaidi ya megawat 1400 huku kuna maeneo yana mgao mfano g/mboto siku tatu hawana umeme toka tarehe 3.rangi tatu leo asubuhi walikuwa na mgao.hayo ni baadhi ya sehemu ninayojua.

Na kuna maeneo mengi tu.

Wamekalia kupiga dili tu hakuna wanachokifanya kuinusuru nchi iwe na nishati ya kutosha ili nchi iweze kuendelea.

Nikiona mtu anatetea Tanesco namuona kama mhaini flani asiyewajali watanzania wenzake.

Nyie endeleeni ipo siku yenu..najua hamtafanya kazi Tanesco milele.

Mabadiliki yatakuja tu huko mbeleni hata kwa ulazima na hizi kero na hujuma za wazi kwenye maendeleo ya nchi yatakwisha
 
Mkuu siamini kama huna elimu hata kidogo ya menejimenti
mameneja wa mikoa na wilaya waripoti kwa waziri we unaona ni sawa?
Waziri kutoa maagizo kwa njia ya simu ni sawa?

hivi labda nikuulize wewe ndo meneja wa wilaya au kanda wa Tanesco
ceo wako akupe maagizo ya nenda kushoto na waziri aje aseme nenda kulia
we unaonaje? ni sawa?


Mawaziri wengine hao wanatimua na kuweka watu wengine....hawafanyi daily tasks...kama Muhongo
Muhongo hajatimua mtu ni kuwapa maagizo yake tu daily

Still unaendelea kumtuhumu mtu kwa assumption,hadhi ya JF ni kubwa scandal nyingi nchi hii zimeibuliwa hapa
  1. Labda uko Tanesco ,tuletee hayo maagizo ambayo Muhongo ametofautiana na CEO wa Tanesco ?
  2. Tuonyeshe hayo maagizo Muhongo alilyoyatoa Tanesco kwa njia ya simu ?
 
Back
Top Bottom