Muhongo agombaniwa kudhaminiwa

Muhongo agombaniwa kudhaminiwa

Udalali wake kwenye gesi ni upi we kilaza??? Hayo makampuni yalikuwepo kabla yake mbona hamkuwaita watangulizi wake madalali??? Tatizo mmenyimwa ulaji wa shortcut pale nishati basi kujifurahisha mmeona mumtungie majina ya waliowatuma mxyuuuu!!!

Kusema ukweli namuonea huruma sana the fixer wa issue ya kumuondoa Muhongo NISHATI NA MADINI.

Kuna kamsemo kanasemwaga humu kuwa DHAMBI HII ITAKUTAFUNA, ni ukweli usio shaka dhambi hii ya kumfitini Muhongo itamtafuna. Najua ana nguvu ya pesa, na ana nguvu ya media ila huwezi kupingana na mapenzi ya MUNGU.

Kibaya zaidi anajifanya kumsupport EL wakati anasahau mwaka 2008 alikuwa kinara wa kumchafua lowassa na mastermind wa kumuweka lowassa magogoni LA. Hajui hata hawa watu anaowassuport watamfanya nini wakiingia madarakani.

Alikosea sana alivyotumia ushawishi wake wa vyombo vya habari kumchafua mtu ambaye hana kosa Muhongo, bora hawa kina EL wanajulikana rangi zao halisi.

Sasa ile KARMA anayoisemaga jamaa mmoja PASCO ndo inaenda kujidhihirisha. Sijui mwisho wake utakuwaje.
 
huyu prof. atakuwepo ktk ile orodha ya stanbk ambayo orodha haikutoka...

ukichuja ktk mafisadi, utapata fisadi mkuu!!

Weka list na kiasi hapa, mwanaume mzima unaleta utabiri hapa huoni aibu
 
  • Thanks
Reactions: aye
huyu prof. atakuwepo ktk ile orodha ya stanbk ambayo orodha haikutoka...

ukichuja ktk mafisadi, utapata fisadi mkuu!!
With all confidence eti unasema atakuwepo. Seriously??????
Yani tuamini maneno yako kuwa atakuwepo kwa kitu unachoisia na hata huna ushahidi nacho.
Alafu kwa hizo hisia zako unamuhukumu mtu???? Sidhani hata kama unastahili kuingia mbinguni kwa mujibu wa imani za kiislamu na kikristo.
 
Wanakwepa Kodi? Kivipi, nyie msitufanye mbulula. Salsa mbona fedha ya Escrow ilitoka bila kulipiwa kodi? Acheni utoto wenu humu jf. Hafai Kabisa hana sifa ya kuchaguliwa labda ateuliwe kuwa Raid wa hicho kijiji chenu.
 
Kwa Lowasa(Mwakyembe katuonea),kwa Muhongo (Zitto katuonea), Hakuna mtia nia mwenye doa CCM,hata Chenge akitangaza nia sitashangaa wapambe wake waikisema mzalendo anakuja kutukomboa. This is CCM bana!.
 
Dalali naye anahangaika bure ubunge wenyewe amepewa uraisi naye anafikiria ni kupewa anajidanganya sana.
 
Acha undorobo wewe kama kauli yake ni ya uongo, si muende mkakope kwenye hayo mabenki na muwekeze ili kumprove wrong. Muhongo alifafanua hiyo kauli kuwa biashara ya gesi ni ya kubahatisha ndio maana anashauri watu wawekeze kwingine anawaonea huruma msifilisike, angalia uwezo wa makampuni yanayofanya utafiti nchini halafu ndo upige kelele.

Hayo mabenki yanakopesha kama yakiona una uweZo wa kurudisha salio hata kama ukikosa unachobahatisha. Hakuna benki inayokopesha kiholela, hao unaowatetea waambie wakakope kama watapata hiyo mikopo, sio unabwabwaja tu.

muhongo fisadi pia linajiamini,majizi ya ccm kama mashetani hayaogopi juzi tu leo anataka ikuru
 
nchi inaitaji watafiti,
nchi inaitaji wanasayansi,
nchi inahitaji mtu anaejua tulipotoka tulipo na tunapokwenda.. si mwingine ni profesa s.muhongo ntampigia kampeni huyu jamaa japo sijawai kuwaza kitu kama hicho kabla.. na ntamuombea pia MUNGU amnyooshee.
 
Tatizo lake moja tu, dharau na kujifanya anajua. Prof Lipumba ni mchumi wa dunia hadi world economic crisis inamjua lakin hatujasikia hata siku moja kujisifu sifu, yeye mpasua miamba kuutwa kujisifu tu, hapa hana nafasi
 
muhongo fisadi pia linajiamini,majizi ya ccm kama mashetani hayaogopi juzi tu leo anataka ikuru
kati ya wagombea wote, muhongo ni mzuri kuliko hata wagombea wote wa UKAWA.

aliituliza sana tanesco baada ya ngereja kutoimudu, ana akili na ndiye rais pekee ambaye kama tungempata angetusaidia sana. kwa bahati mbaya sana, lowasa ndiye anayependwa na watu na ndiye anayevaa mikoba mwaka huu.

natamani lowasa akiwa rais amchukue huyu jamaa awe waziri mkuu au amrudishe kwenye nishati na madini. ana uwezo mkubwa sana sana. namshauri amuunge mkono lowasa wakishaanza zile mbio ili wawe timu moja. nilisikitika sana wakati anajiuzuru hakutakiwa kutoka kabisa ile sector.
 
Kwa Lowasa(Mwakyembe katuonea),kwa Muhongo (Zitto katuonea), Hakuna mtia nia mwenye doa CCM,hata Chenge akitangaza nia sitashangaa wapambe wake waikisema mzalendo anakuja kutukomboa. This is CCM bana!.

Nikusaidie kitu ndugu yangu. Kwenye suala la RICHMOND ni ngumu sana kumsafisha lowassa kwa sbabu tu ushahidi wa barua upo kuwa alikuwa akiingilia taratibu kwa kuulizia mchakato unaendaje na hata kusema ile kampuni ipewe tender. kama unakataa kuna wanayo ile ripoti ya mwakyembe humu wakuwekee ujionee.Kwa suala la chenge ukweli uko wazi na hata uthibitisho wa miamala iliyofanyika kumuwekea hela kwenye account zake sasa hapo tumemaliza.

Twende kwa muhongo kuna uthibitisho gani wa uhusika wake kwenye escrow, kwa mawasiliano ya barua yalikuwa kati ya KATIBU MKUU NISHATI NA MADINI KAMA MTENDAJI MKUU WA WIZARA, MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI KAMA MSHAURI MKUU WA SERIKALI KWENYE MAMBO YA SHERIA NA BOT KAMA MUHIFADHI PESA. NI WAPI UMEONA KUNA BARUA MUHONGO ALIANDIKA?

AU UNAYO RIPOTI YAKO YA CAG NA PCCB AU TUME YA MAADILI TUWEKEE HUMU.NI WAPI KWENYE MIAMALA ILIYOFANYIKA ULIONA JINA LA MUHONGO KUWEKEWA FEDHA? TUWEKEE BASI HUMU.
 
Dalali naye anahangaika bure ubunge wenyewe amepewa uraisi naye anafikiria ni kupewa anajidanganya sana.

Mnazidi tu kujileta watoa tuhuma ila mkiambiwa ushahidi mnakimbia. Haya na wewe tuletee ushahidi wako wa uhusika wa Muhongo kwenye udalali na ufisadi wa escrow. Ukishindwa usiku mwema.
 
Wanakwepa Kodi? Kivipi, nyie msitufanye mbulula. Salsa mbona fedha ya Escrow ilitoka bila kulipiwa kodi? Acheni utoto wenu humu jf. Hafai Kabisa hana sifa ya kuchaguliwa labda ateuliwe kuwa Raid wa hicho kijiji chenu.
Huwajui wakwepa kodi kina nani???? Hujawai kusikia kuna kampuni fulani watu wanafanya kazi bila kupewa mikataba???
Hujui njia ya ukwepaji kodi kwa kutompa mfanyakazi mkataba??? Au fanya utafiti kama wafanyakazi wanaofanya kazi bila mikataba wanalipwaje mishahara yao??? na kama kuna kodi inakatwa???
 
muhongo fisadi pia linajiamini,majizi ya ccm kama mashetani hayaogopi juzi tu leo anataka ikuru
Duuh, wewe mwingine umejileta. Haya tupe ushahidi basi wa uliyoyasema. ila usikimbie kama wenzako walioulizwa ushahidi alafu wametokomea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom