Muhimbili Yabadilika, wauguzi wanakimbizana kutoa huduma kwa wagonjwa

Kingsmann

JF-Expert Member
Oct 4, 2018
4,448
16,312
"MADAKTARI, wauguzi wanakimbizana kutoa huduma kwa wagonjwa, kama wakati wa Rais John Magufuli.” Ni kauli ya mmoja wa wagonjwa waliozungumza na Raia Mwema jana, kuhusu mabadiliko ya utendaji wa hospitali hiyo, tangu ilipopata Mkurugenzi Mpya, Profesa Mohamed Janabi.

Mgonjwa huyo ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe, alisema kuna mabadiliko makubwa ya kiutendaji hospitalini hapo, kwani Profesa Janabi amekuwa akiingia kazini mapema kuliko madaktari wake, na kuzunguka kila sehemu na kila idara kuona wanavyohudumia wagonjwa. “Siku za nyuma wagonjwa tulikuwa tunawahi kufika, lakini huduma zinaanza saa tatu au saa nne. Sasa hivi madaktari wengi saa moja wako kazini, ikifika saa mbili kazi zinaanza yaani ni mshangao wa hali ya juu,” alisema mgonjwa huyo.

Mmoja wa wauguzi wa hospitali hiyo, alisema kuna mchakamchaka tangu Profesa Janabi aingie. "Mkurugenzi anafika, saa moja yuko kazini, wewe mwenzangu na mimi unaingiaje saa mbili? Akifika anazunguka kote, anajua nani wanapaswa kuwapo, akiona mgonjwa anazungumza naye, shida yake, kwa nini yuko hapa, amesikilizwa, yaani anafuatilia kila kitu," alisema Muuguzi huyo.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili hospitalini hapo, umebaini kuwapo mabadiliko hayo. Eneo ambalo madaktari wakilitumia kusimama na kupoteza muda, sasa hivi hakuna anayesimama nje, usafi unafanyika kwa kiwango cha hali ya juu.. Lakini pia madaktari na wauguzi wamekuwa na kuhudumia wakipokea wagonjwa vizuri tofauti na awali.

Wakati wa Rais Magufuli, huduma kwenye hopitali Hiyo ziliboreka huku kiwango cha rushwa kikielezwa kupungua. Madaktari na wauguzi waliwajibika ipasavyo, wakihofia kutumbuliwa kutokana na ziara za ghafla alizofanya hospitalini hapo.

Hivi karibuni, Rais Samia Suluhu Hassan alimteua Profesa Janabi aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, akichukua nafasi ya Profesa Lawrence Maseru aliyestaafu. Alimteua Dk Peter Kisenge kuziba nafasi ya Profesa Janabi. Kabla Dk Kisenge alikuwa Mkurugenzi wa Utafiti na Mafunzo JKCI.​


Raia Mwema.
 
IMG-20221011-WA0006.jpg
 
Hii siyo taarifa nzuri hata kidogo. Uadilifu na kujituma hakutakiwi kulazimishwa. Watu wanapofanya kazi kisa kuna mtu anawafuatilia ni ishara ya uovu wa kiwango cha juu sana.

Tunahitaji watumishi wanaoelewa majukumu yao na umuhimu wao katika kulijenga taifa bila shuruti. Tunahitaji nidhamu na uweledi miongoni mwa watumishi wetu ijengwe kwenye taasisi na siyo mtu mmoja.

Kumtegemea mtu mmoja ndo kunaturudisha nyuma toka enzi za Nyerere maana siyo wote watajitolea au kuwa na uchungu na nchi yao kila siku ila tukijenga taasisi zinazokuza uweledi, uadilifu na kujituma kazini tutafikia malengo mapema sana.
 
Hii hospitali ni kweli inahitaji mtu mkakamavu,walikuwa wanajifanyia kazi kwa mazoea sana.Sisahau nilikuwa na mgonjwa wangu miaka kadhaa imepita pale Muhumbili,wakati naondoka jioni nikaambiwa wanamuwekea drip,tukatolewa nje kuwa muda umeisha wa kuona wagonjwa,kesho yake nafika pale mida ya jioni drip iko pale imesogea kidogo tu,na imechomoka pale mkononi sijui ilichomoka saa ngapi,maana aliekwenda kuomuona asubuhi aliamini kuwa inaendelea kuingia,hali ya mgonjwa ilikuwa mbaya zaidi kwani alikuwa maechoka sana,nilipowaambia ndio wakaichomeka ikaanza kuingia tena,kwahiyo ina maana muda wote ule hakuna kilichoingia,na bahati mbaya kesho yake mgonjwa wangu alifariki dunia...
 
Hii hospitali ni kweli inahitaji mtu mkakamavu,walikuwa wanajifanyia kazi kwa mazoea sana.Sisahau nilikuwa na mgonjwa wangu miaka kadhaa imepita pale Muhumbili,wakati naondoka jioni nikaambiwa wanamuwekea drip,tukatolewa nje kuwa muda umeisha wa kuona wagonjwa,kesho yake nafika pale mida ya jioni drip iko pale imesogea kidogo tu,na imechomoka pale mkononi sijui ilichomoka saa ngapi,maana aliekwenda kuomuona asubuhi aliamini kuwa inaendelea kuingia,hali ya mgonjwa ilikuwa mbaya zaidi kwani alikuwa maechoka sana,nilipowaambia ndio wakaichomeka ikaanza kuingia tena,kwahiyo ina maana muda wote ule hakuna kilichoingia,na bahati mbaya kesho yake mgonjwa wangu alifariki dunia...
Daaaahhhh pole sana mkuu.
Matukio kama haya hua yanaumiza sana moyo, pamoja ya kua kila mtu lazima afe ila asilimia kubwa ya wagonjwa wetu hua wanapoteza maisha kutokana na uzembe wa makusudi wa madaktari wetu.
 
wani Profesa Janabi amekuwa akiingia kazini mapema kuliko madaktari wake, na kuzunguka kila sehemu na kila idara kuona wanavyohudumia wagonjwa.
nguvu ya soda, atachoka leo au kesho. Ni kuweka systems za kumwajibisha anayechelewa, sytem endelevu, short of that atachoka tu! Nilkuwa nchi fulani ulaya nafanya kibarua. Kumbe supervisor ana monito kila mtu. At the end of the month anapiga hesabu dakika/saa ambazo hukuwa kazini...anadeduct kwenye salary kuwa hizo saa hukuwa unafanya kazi, ulikuwa pasipo kazi. Adabu ilikuja siku iliyofuata.....huezi kuchelewa tena
 
nguvu ya soda, atachoka leo au kesho. Ni kuweka systems za kumwajibisha anayechelewa, sytem endelevu, short of that atachoka tu! Nilkuwa nchi fulani ulaya nafanya kibarua. Kumbe supervisor ana monito kila mtu. At the end of the month anapiga hesabu dakika/saa ambazo hukuwa kazini...anadeduct kwenye salary kuwa hizo saa hukuwa unafanya kazi, ulikuwa pasiko pazi. Adabu ilikuaja siku iliyofuata.....huezi kuchelewa tena
Huo ndo mfumo unaotakiwa...hakuna kitu kinauma kama kukatwa mshahara...huwez rudia uzembe.
Kampuni za wachina wana huo utaratibu, hawaangaiki na mtu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huo ndo mfumo unaotakiwa...hakuna kitu kinauma kama kukatwa mshahara...huwez rudia uzembe.
Kampuni za wachina wana huo utaratibu, hawaangaiki na mtu.

Sent using Jamii Forums mobile app
exactly, mzungu akikuona unasoma gazeti ana note time.. then at the end of the month anakwambia siku fulani muda huu mpaka huu ulikuwa unasoma gazeti! unanywea kesho adabu tele. unazima hata simu.....
 
Tatizo hatutengenezi mfumo, tunamtegemea mtu mmoja ndie alete uchapakazi kwenye taasisi kubwa milele .. ikitokea janabi akifa ama akistaafu je? Akaja bosi mvivu
 
Hii siyo taarifa nzuri hata kidogo. Uadilifu na kujituma hakutakiwi kulazimishwa. Watu wanapofanya kazi kisa kuna mtu anawafuatilia ni ishara ya uovu wa kiwango cha juu sana.

Tunahitaji watumishi wanaoelewa majukumu yao na umuhimu wao katika kulijenga taifa bila shuruti. Tunahitaji nidhamu na uweledi miongoni mwa watumishi wetu ijengwe kwenye taasisi na siyo mtu mmoja.

Kumtegemea mtu mmoja ndo kunaturudisha nyuma toka enzi za Nyerere maana siyo wote watajitolea au kuwa na uchungu na nchi yao kila siku ila tukijenga taasisi zinazokuza uweledi, uadilifu na kujituma kazini tutafikia malengo mapema sana.
Mawazo mfu ya nchi ya kufikirika...huo uwajibikaji wa kujituma mwenyewe utawashukia watendaji kwa uwezo wa Roho Mtakatifu? Lazima wapigwe jaramba kijeshi
 
kwahiyo mnataka kusema yule pulofeseli msitahafu alikua hajui alitendalo ama? huyu pulofeseli anayekula kiazi na maji siku nzima anajikuta anajua sana
 
Back
Top Bottom