Profesa Janabi ataka watu wembamba wasinyanyapaliwe

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,660
12,305
PROFESA Mohamed Janabi amesema mtu kuwa mwembamba haina maana kwamba ni mgonjwa, akionya unyanyapaa dhidi ya kundi hilo ambalo yeye ni sehemu yake.

Mkurugenzi Mtendaji huyo wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ametoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Afua ya Mfumo Jumuishi hospitalini huko.

Katika uzinduzi huo, Prof. Mohamed Janabi, amesema unyanyapaa upo hata miongoni mwa WAVIU, akieleza alivyoshuhudia hali hiyo wakati anatoa matibabu kwa kundi hilo.

Amesema kuwa alipokuwa anatoa matibabu kwao, wengi wao walimwona anafaa kuwatibu, wakiwakataa madaktari wengi kutokana na yeye (Janabi) kuwa mwembamba, hivyo kudhani naye huenda anaishi na VVU.

Credit - Nipashe
 
Back
Top Bottom