Kwa kupenda vitu vipya na maonyesho waswahili hatujambo....
Kwanini tusiboreshe kwanza huku
Ni lini Muhimbili itahamia Mlongazila?
Siku ukiugua utajua umuhimu wake
Kumekuwa na mafanikio makubwa katika utoaji wa huduma za afya Hospitali ya Taifa Muhimbili. Kwamba sasa, wagonjwa wenye matatizo ya moyo wataweza kufanyiwa uchunguzi na kuweza kuhudumiwa kwa kuzibua mishipa inayopeleka damu kwenye moyo kwa mfumo wa kisasa zaidi.
Kwamba wagonjwa wenye matatizo hayo ya moyo, wataweza sasa kuzibuliwa matundu hayo kwenye moyo bila kufanyiwa upasuaji kifuani. Hii, kwa hakika ni habari njema, tena yenye kustahili kupongezwa.
Kwa mujibu wa taarifa kuhusu mafanikio haya, ni kwamba kufungwa kwa mtambo maalumu Hospitali ya Taifa Muhimbili, "Cath Lab" ndiko kutafanikisha huduma hizo muhimu katika maisha ya binadamu.
Kwa ufafanuzi tu ni kwamba, Cath Lab ni mtambo maalumu unaotumika kufanya uchunguzi, kuzibua mishipa inayopeleka damu kwenye moyo na kuziba matundu ya moyo bila kufanya upasuaji.
Kwa kuzingatia ukubwa wa magonjwa ya moyo nchini na gharama ambayo serikali na hata watu au taasisi binafsi zimekuwa zikiingia kusafirisha wagonjwa wa moyo kwa ajili ya kuokoa maisha yao kwa tiba za aina hii nje ya nchi, hakika, kwa kiasi kikubwa hatua hii itasaidia kuipa sura mpya sekta ya afya hapa nchini.
Tunajivunia wataalamu wetu nchini ambao tayari wameutumia mtambo huu kwa ufanisi mkubwa, kupitia Kitengo cha Tiba ya Moyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, wakifanikiwa kufanya tiba ya moyo kwa kuziba matundu ya kwenye moyo bila kufanya upasuaji wa kifua.
Lakini si tu wataalamu wetu hapa nchini bali hata wenzao kutoka nje ya nchi ambao, kwa pamoja, wamefanikisha tiba hiyo, hao ni pamoja na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Prince Sultan Cardiac Centre ya Riyadh Saudi Arabia.
Tunaungana na Watanzania wengi katika kuamini kwamba hi ni hatua nyingine kubwa katika nyanja ya tiba na afya nchini baada ya kushuhudia ushirikiano wa aina hii na hospitali nyingine kadhaa za kimataifa kwa kutumia mifumo ya habari kama Video Conference ambayo huwawezesha madaktari kufanya upasuaji nchini kwa kushirikiana na madaktari bingwa wenzao walioko nje ya nchi.
Labda hadi magufuli aapishwe
Kuwa na mitambo ni jambo moja na kupata huduma ni jambo lingine
Binafsi ndugu yangu amelazwa pale wiki ya tatu sasa hajapata huduma simply salio hamna inatakiwa 2m Iliafanyiwe manuva apate matibabu.
Nimejaribu kukomaa lakini hizo danadana nimeona naweza kumpoteza ndugu yangu tuna tafuta salio.
Mkuu ni majanga, yahani taifa lenye
watu zaidi ya milioni 45 wanatumia ct-scan machines moja! huku mkiongeza idadi ya magari ya washa washa
Miaka yote hii ya uhuru, suala la kununua mashine ya moyo, CT-scan, MRI, haikustahili kuwa suala la kutangaziwa kitaifa.
Sasa hata kujenga flyover nchi nzima inatangaziwa na rais wa nchi na makamu wake wanaitwa kufungua daraja!
Hayo ni matunda ya walipa kodi.
Ushauri tu!Afya haina siasa!ni vizuri kufuatilia kwa makini elimu ya Afya ili kuepuka kupata magonjwa ambayo kimsingi yanaepukika!ulevi kupindukia,uvutaji wa sigara, madawa ya kulevya, utumiaji na unywaji wa vitu vikali kwa afya, matumizi ya kemikali, vipodozi na mazingira hatarishi!! Haya mambo ndo yanafanya watu kuteseka na magonjwa makubwa!Pia tatizo la watu kutokujenga utamaduni wa kufanya mazoezi mara kwa mara kunafanya taifa lisiwe na watu wenye afya bali uwepo wa wingi wa watu wenye afya mgogoro!
Huduma za afya ni ghari hakuna asiyejua hilo ndo maana kuna baadhi ya mambo yanafanywa kwa awamu na sasa yamefanyika na hali iko tofauti na mchangiaji alivyosema!nimesema Siasa hazina nafasi kwenye afya, maaana afya ni uhai!Kama mchangiaji huna jipya bora ukae kimya tu na kupita kimyakimya kwenye uzi huu!
Kumekuwa na mafanikio makubwa katika utoaji wa huduma za afya Hospitali ya Taifa Muhimbili. Kwamba sasa, wagonjwa wenye matatizo ya moyo wataweza kufanyiwa uchunguzi na kuweza kuhudumiwa kwa kuzibua mishipa inayopeleka damu kwenye moyo kwa mfumo wa kisasa zaidi.
Kwamba wagonjwa wenye matatizo hayo ya moyo, wataweza sasa kuzibuliwa matundu hayo kwenye moyo bila kufanyiwa upasuaji kifuani. Hii, kwa hakika ni habari njema, tena yenye kustahili kupongezwa.
Kwa mujibu wa taarifa kuhusu mafanikio haya, ni kwamba kufungwa kwa mtambo maalumu Hospitali ya Taifa Muhimbili, "Cath Lab" ndiko kutafanikisha huduma hizo muhimu katika maisha ya binadamu.
Kwa ufafanuzi tu ni kwamba, Cath Lab ni mtambo maalumu unaotumika kufanya uchunguzi, kuzibua mishipa inayopeleka damu kwenye moyo na kuziba matundu ya moyo bila kufanya upasuaji.
Kwa kuzingatia ukubwa wa magonjwa ya moyo nchini na gharama ambayo serikali na hata watu au taasisi binafsi zimekuwa zikiingia kusafirisha wagonjwa wa moyo kwa ajili ya kuokoa maisha yao kwa tiba za aina hii nje ya nchi, hakika, kwa kiasi kikubwa hatua hii itasaidia kuipa sura mpya sekta ya afya hapa nchini.
Tunajivunia wataalamu wetu nchini ambao tayari wameutumia mtambo huu kwa ufanisi mkubwa, kupitia Kitengo cha Tiba ya Moyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, wakifanikiwa kufanya tiba ya moyo kwa kuziba matundu ya kwenye moyo bila kufanya upasuaji wa kifua.
Lakini si tu wataalamu wetu hapa nchini bali hata wenzao kutoka nje ya nchi ambao, kwa pamoja, wamefanikisha tiba hiyo, hao ni pamoja na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Prince Sultan Cardiac Centre ya Riyadh Saudi Arabia.
Tunaungana na Watanzania wengi katika kuamini kwamba hi ni hatua nyingine kubwa katika nyanja ya tiba na afya nchini baada ya kushuhudia ushirikiano wa aina hii na hospitali nyingine kadhaa za kimataifa kwa kutumia mifumo ya habari kama Video Conference ambayo huwawezesha madaktari kufanya upasuaji nchini kwa kushirikiana na madaktari bingwa wenzao walioko nje ya nchi.