Mufti Abubakari Zuberi ahimiza uharaka kesi ya mashehe wa Uamsho

Ileje

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,797
12,239
Dalili hizi zimeanza kuonekana baada ya Shehe Mkuu wa BAKWATA Mufti Zuberi kuzitaka mamlaka kuharakishwa kusikilizwa kwa shauri lao. Ni dhahiri shahiri serikali haiwezi kupuuza ombi lake na hivyo DPP ama atashauriwa kulifuta shauri hilo au ataanzisha mchakato wa kusikilizwa shauri hilo haraka.

========

MUFTI.jpg

Alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa mkutano wa viongozi wa dini waliokutana kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali yanayoendelea nchini.

Alisema ni miaka mingi sasa tangu kesi hiyo ianze kusikiliwa na kuomba wenye mamlaka ya kusimamia kesi kufanya haraka kusikiliza ili ifikie muafaka.

“Hatuwezi kuingilia mambo ya kisheria, lakini ninachoweza kuomba ni uharakishwaji wa kusikiliza kesi yao, kesi hii imekaa miaka mingi, suala hili niombe mamlaka husika ziharakishe kuisikiliza kwa sababu imekaa miaka mingi,” alisema Mufti na kuongeza:
“Usikilizwaji wa kesi kwa haraka na hukumu ikatolewa itajulikana nani ana hatia gani na achukuliwe hatua gani na nani hana, kuliko kukaa ndani muda mrefu bila kufahamu hatma yao.”

Miongoni mwa mambo mengine ambayo viongozi hao wa dini walizungumzia ni kuhusu vitendo vya ukatili vinavyoendelea kwa watoto na kuwataka wazazi kuwajibika katika malezi ya watoto wao.

“Hawa watoto ndiyo viongozi wa nchi tunaowategemea kesho, kwa hiyo tusipowajibika katika kuwatunza na kuwalinda tunakuwa tunaharibu taifa letu, ni vema kila mzazi, mlezi na jamii yote iwajibike katika kumlinda mtoto,”alisema Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)Jimbo la Mashariki na Pwani, Dk. Alex Malasusa.

Alisema: “Asilimia kubwa ya watoto huharibika tabia kutokana na kukosa uangalizi wa wazazi ambao wanabanwa na shughuli za kila siku, hivyo wanapaswa watenge muda wa malezi. Tuombe kwamba kila unapobarikiwa kupata mtoto, uwajibike pia na katika kumlea na kumlinda.”

Machi 28, mwaka huu Rais Samia Suluhu Hassan wakati akipokea taarifa ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ya mwaka 2019/2020, aliiagiza kuharakishwa kwa kesi, kuziondoa zisizo na msingi ili kuondokana na idadi kubwa ya kesi ambazo serikali imekuwa ikishindwa.

Vilevile, Juni 13, mwaka huu, viongozi wa dini Zanzibar, walimwomba Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Mwinyi, kuangalia suala la viongozi hao wa uamsho ambao wako mahabusu kwa muda mrefu.

Miongoni mwa mambo waliyomwomba ni kuangalia kama wana hatia au la, badala ya kuendelea kusota rumande bila kujua hatima yao.

Chanzo: Nipashe
 
Ila Tanzania hatuna Viongozi wa dini! Yaani dini na madhehebu yote Tanzania kwa 75% ni watafuta fursa tu! Nadhani sometimes Mwenyezi Mungu huwa anacheka tu! Anamuangalia Malasusa anacheeeka kisha anamgeukia Abubakary anaangua kicheko tena.

Anaachana nao anafungua files nyingine
 
Ila Tanzania hatuna Viongozi wa dini! Yaani dini na madhehebu yote Tanzania kwa 75% ni watafuta fursa tu! Nadhani sometimes Mwenyezi Mungu huwa anacheka tu! Anamuangalia Malasusa anacheeeka kisha anamgeukia Abubakary anaangua kicheko tena...
Ni jambo la kushangaza kwa sababu kwa takribani miaka 8 Mashehe wa Uamusho wamekuwa wakisota mahabusu bila kusikia kauli yo yote kutoka kwa viongozi wa BAKWATA. Aidha viongozi wa dini za kikristo nao wamekuwa kimya kama vile hawafamu cho chote kuhusu viongozi wenzao wa kiislamu.

Hongera kwake Shehe Ponda ambaye mara kadhaa amekuwa akiwasemea viongozi hao.

Viongozi wa dini zote watambue kuwa hawako salama sana katika nchi hii ambayo utawala wake hutegemea nani ni kiongozi na siyo Chama ngani kinaongoza serikali.
 
Huyu alikuwa wapi miaka yote minane? Alikuwa Saudia au Makkah? Alivyokuwa anashirikiana na DCI Mganga aliyetumbuliwa kwenda magerezani kufanya prebargain na wale wanaodaiwa kutakatisha pesa hakuwaona hao masheikh ili amshauri rafiki yake Mganga na mwendazake juu ya masheikh hao ili waharakishiwe kusikiliza? Aache unaa! Alishindwa kumtumia Mganga na meko kwani walikuwa mabest Sasa anahorojeka tu kutafuta popularity!
 
Dalili hizi zimeanza kuonekana baada ya Shehe Mkuu wa BAKWATA Mufti Zuberi kuzitaka mamlaka kuharakishwa kusikilizwa kwa shauri lao. Ni dhahiri shahiri serikali haiwezi kupuuza ombi lake na hivyo DPP ama atashauriwa kulifuta shauri hilo au ataanzisha mchakato wa kusikilizwa shauri hilo haraka.

========

Alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa mkutano wa viongozi wa dini waliokutana kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali yanayoendelea nchini.

Alisema ni miaka mingi sasa tangu kesi hiyo ianze kusikiliwa na kuomba wenye mamlaka ya kusimamia kesi kufanya haraka kusikiliza ili ifikie muafaka.

“Hatuwezi kuingilia mambo ya kisheria, lakini ninachoweza kuomba ni uharakishwaji wa kusikiliza kesi yao, kesi hii imekaa miaka mingi, suala hili niombe mamlaka husika ziharakishe kuisikiliza kwa sababu imekaa miaka mingi,” alisema Mufti na kuongeza:
“Usikilizwaji wa kesi kwa haraka na hukumu ikatolewa itajulikana nani ana hatia gani na achukuliwe hatua gani na nani hana, kuliko kukaa ndani muda mrefu bila kufahamu hatma yao.”

Miongoni mwa mambo mengine ambayo viongozi hao wa dini walizungumzia ni kuhusu vitendo vya ukatili vinavyoendelea kwa watoto na kuwataka wazazi kuwajibika katika malezi ya watoto wao.

“Hawa watoto ndiyo viongozi wa nchi tunaowategemea kesho, kwa hiyo tusipowajibika katika kuwatunza na kuwalinda tunakuwa tunaharibu taifa letu, ni vema kila mzazi, mlezi na jamii yote iwajibike katika kumlinda mtoto,”alisema Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)Jimbo la Mashariki na Pwani, Dk. Alex Malasusa.

Alisema: “Asilimia kubwa ya watoto huharibika tabia kutokana na kukosa uangalizi wa wazazi ambao wanabanwa na shughuli za kila siku, hivyo wanapaswa watenge muda wa malezi. Tuombe kwamba kila unapobarikiwa kupata mtoto, uwajibike pia na katika kumlea na kumlinda.”

Machi 28, mwaka huu Rais Samia Suluhu Hassan wakati akipokea taarifa ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ya mwaka 2019/2020, aliiagiza kuharakishwa kwa kesi, kuziondoa zisizo na msingi ili kuondokana na idadi kubwa ya kesi ambazo serikali imekuwa ikishindwa.

Vilevile, Juni 13, mwaka huu, viongozi wa dini Zanzibar, walimwomba Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Mwinyi, kuangalia suala la viongozi hao wa uamsho ambao wako mahabusu kwa muda mrefu.

Miongoni mwa mambo waliyomwomba ni kuangalia kama wana hatia au la, badala ya kuendelea kusota rumande bila kujua hatima yao.

Chanzo: Nipashe
Zee linafiki ili, mbona wakati wa magufuli hawakuongea ayo?
 
Kama ukisoma katikati ya mstari, utaelewa kuwa sheikh ni ice breaker au whistle blower tu, ili aonekane kuwa Kuna haja ya suala la masheikh kupatiwa ufumbuzi. Kimsingi masheikh wapo katika hatua za mwisho kuachiwa.
 
Mnafiki mkubwa huyu
Ulitaka aingie kwenye mzozo na serikali halafu mwisho wake utakuaje? huko jela kuna zaidi ya masheikh 170 ukiacha hao uamsho na kesi ni hizo hizo tu za ajabu ajabu wanapewa.
 
Back
Top Bottom