Mkuu, huyo daktari kwa nini alitegemea kipimo cha damu tu? Ubaya wa kipimo cha damu ni kwamba huwezi kutofautisha kama una infection sasa hivi. Kitu wanachofanya kwenye kipimo cha damu ni ku-test antibodies za H-Pylori (kinga ya kupigana na hawa bacteria) kama unayo mwilini. Sasa kuwa na hizo antibodies ina maana either unao, au ulishaugua zamani na kupona na zimebakia tu antibodies. Kipimo wanachosema ni cha uhakika ni kile wanakupa chemical fulani unakunywa halafu unapewa mfuko wa nailoni unapumulia ndani wanaona kama hewa yako ina carbon dioxide, basi wanajua una hao bakteria. Au unapima choo. By the way Bongo nyoso. N hospital nyingi sana wanabambikia watu kuwa wana hawa bacteria bila kuwa nao. Ukweli ni kwamba wengi hawajui kupima sawasawa.
Kuhusu muda wa kupima tena ni wiki nne na kuendelea na ukipima damu inaweza kuonyesha unao wakati huna.