Katika maisha haya kuelekea mafanikio kila mmoja anapambana kwa namna anavyojua yeye katika lengo la kufika kule anakoona kuna mfaa......
Katika mapambano hayo kila mmoja anatumia silaha yake ambayo anaamiini itamletea ushindi ....
Njia uliyoitumia wewe kupata mafanikio maishani mwako haimaanishi kuwa inaweza kumfanya mwingine awe kama wewe.......
Tumetofautiana katika kuyapima mafanikio kama tulivyotofautiana katika kuyatafuta mafanikio....sisi walalahoi mafanikio yetu makubwa ni kuweza kumudu kupata milo mitatu kwa siku moja na kuweza kumudu gharama za kulipia pango lako......inawezekana wewe mafanikio ni kujenga nyingine bora zaidi ya ile ya mwanzo hiyo inategemea na jinsi gani ulivyofanikiwa mipango yako......wakati mwingine utofauti wa hali ya maisha kwenye jamii zetu ndio unaoleta usawa kwa namna moja au nyingine........
Maisha ni mchakato na mafanikio ni matokeo ya mchakato huo ulioambatana na mipango mizuri ya kufika huko......ukiona maisha yako yamejaa mataabiko na mahangaiko basi jua wazi kuwa kuna sehemu kwenye mchakato huo ulijikwaa......kuna wengine walijikwaa kwenye kukosa elimu na hatimaye wakairudia elimu na baadae kuyapata matunda yake ambayo wao wanayaita mafanikio.....kuna wengine walijikwaa kwenye ujasiliamali na wakajaribu njia zingine wakajikuta wamefika kule walipotaka wafike.....
Katika ulimwengu huu wa nyama na ngozi hakuna asiyependa upepo wa raha ,burudani na starehe zipulize upande wake.....tumetofautiana tu namna tunavyoyaendea hayo mafanikio.....na ndio maana wapo watu wanapambana na maisha mpaka leo hii kuelekea uzeeni na baadhi wamefanikiwa na wengine bado wanachakarika lakini lengo na dhamira ni kufika huko huko kunakoonekana kuna mafanikio....
Katika harakati hizi za kupambana na maisha aliyefeli ni yule aliyefariki na kuzikwa kaburini....lakini ilihali mtu bado ana uhai wake na bado anapambana haijalishi ana umri gani huwezi kumhukumu kuwa ameshafeli.......kwani hakuna ajuaye kesho.......
Watu wa imani tuna amini kuwa RIDHKI anatoa muumba kwa waja na humpa yule amtakaye.....kuchelewa kwako kupata mafanikio kunaweza kukawa na njia moja wapo ya kukuepusha majanga na kupata kwako kukawa ni kukuleta karibu na majanga.......
NB; UNAWEZA UKAWA UMEPATA KUMBE NDIO UMEKOSA...NA UNAWEZA UKAWA UMEKOSA KUMBE NDIO UMEPATA.......
Maisha hayana mjuzi....,
Samahan hebu nieleweshe hapo namna gan kuish kwnye kuish uhalisia wa maisha ya sasa.Tatizo kubwa linalosumbua vijana ni kujisahau na kuwa kwenye comfort zote. Hatuishi kwenye uhalisia wa maisha ya sasa. Hatuna utaratibu wa kujiwekea malengo yanayotekelezeka.
LIFE BEGINS AT THE AGE OF 40YRZ UWE TAYARI UNA KILA KITU NYUMBA,USAFIRI,BIASHARA NA FAMILIA,UKIFIKA UMRI HUO HAUNA KITU BASI UMEFAIL MAISHA MOJA KWA MOJA
Unakuta mtu anaishi maisha fake badala ya kuangalia uhalisia wa maisha.Samahan hebu nieleweshe hapo namna gan kuish kwnye kuish uhalisia wa maisha ya sasa.
kwa Hiyo wanaume tu ndo wanahangaika kutafuta Mali. wanawake ni kuwaza ndoa na watoto tu?:
1. Kwa wanaume: Muda wako unakimbia lakini hujaoa, huna hela isipokuwa tu ya kula tena ya kuungaunga, huna shamba, huna kiwanja, huna nyumba, huna mchumba, huna mke wala huna mtoto, ukijicheki hivi hujui unakoelekea.
2. Kwa wanawake: hela huna, labda vimizinga vya hapa na pale ambavyo havikufikishi popote, huna mchumba, hujaolewa, au una mchumba sugu, umeolewa ukaachika (Mungu aepushe mbali), single mother, ]