Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,742
Mwasisi wa Chadema,Edwin Mtei amesema kuna baadhi ya watu nchini wanakesha usiku na mchana kuhakikisha wanafanya njama za kukidhoofisha na hata kukipoteza kabisa chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Mtei,alitoa kauli hiyo wakati chama hicho kikiwa katika wakati mgumu baada ya baadhi ya viongozi wake kushambuliana kupitia mitandao ya kijamii, huku aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Arusha,Samson Mwigamba akisimamishwa kwa madai ya kukiuka kanuni za chama hicho.
Akihojiwa na gazeti hili, Mtei alisema kuna baadhi ya watu kutoka Chama Tawala cha CCM wanahakikisha wanatengeneza mifarakano kila kukicha ili kukivuruga Chadema.
Alisema mara baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa kauli kuwa huenda CCM ikang"oka mwaka 2015, baadhi ya makada na viongozi wameanza kukesha wakifanya mbinu ya kukivuruga ili Chadema kisishike dola.
"Kuna watu wa CCM wanakesha usiku na mchana kuhakikisha wanatuvuruga, ili tusishike dola mimi nasema hawatuwezi" alisema Mtei
Hatahivyo, alisema kitendo cha kusimamishwa na hata kufukuzwa baadhi ya makada wa Chadema kimetokana na usaliti ndani ya chama hicho huku wengine wakikubali kutumiwa na CCM.
Chanzo: Mwasisi awashukia
Mtei,alitoa kauli hiyo wakati chama hicho kikiwa katika wakati mgumu baada ya baadhi ya viongozi wake kushambuliana kupitia mitandao ya kijamii, huku aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Arusha,Samson Mwigamba akisimamishwa kwa madai ya kukiuka kanuni za chama hicho.
Akihojiwa na gazeti hili, Mtei alisema kuna baadhi ya watu kutoka Chama Tawala cha CCM wanahakikisha wanatengeneza mifarakano kila kukicha ili kukivuruga Chadema.
Alisema mara baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa kauli kuwa huenda CCM ikang"oka mwaka 2015, baadhi ya makada na viongozi wameanza kukesha wakifanya mbinu ya kukivuruga ili Chadema kisishike dola.
"Kuna watu wa CCM wanakesha usiku na mchana kuhakikisha wanatuvuruga, ili tusishike dola mimi nasema hawatuwezi" alisema Mtei
Hatahivyo, alisema kitendo cha kusimamishwa na hata kufukuzwa baadhi ya makada wa Chadema kimetokana na usaliti ndani ya chama hicho huku wengine wakikubali kutumiwa na CCM.
Chanzo: Mwasisi awashukia
Moja kati ya madai aliyoyatoa mheshimiwa aliyekuwa makamu wa mwenyekiti ni kwamba mzee mtei anawachagulia viongozi hili ni suala serious kuzungumzwa na kiongozi mkubwa kama huyu kama lingezungumzwa mitaani ingekuwa hakuna haja ya kujibu lakini majibu yako yanaitajika katika hili.
kuhusiana na sababu zingine alizozitoa kuhusiana na kuhujumu wagombea na watu kushindwa kurudisha kadi ni suala la kiutendaji zaidi kuliko hujuma kwani alilalamikiwa na viongozi wenzake huko Rukwa na siyo makao makuu kwahiyo kuja kuwalalamikia wenzake makao makuu naona kama ilikuwa ni excuse zaidi ya kutaka anayoyataka mwenyewe labda kwa kutumiwa au sababu binafsi.
binafsi naamini aliyekuwa makamu wa mwenyekiti alikuwa na matatizo ya utendaji kwani sijawahi kusikia akiongea bungeni wala kusikia kaitisha mkutano wa chama mahala popote kujaribu kujenga chama kwahiyo ushauri wangu kwa chadema muwe makini katika uteuzi wenu mjitahidi kutumia record ya mtu ktk kukitumikia chama na siyo majina yao mtu kama alikuwa dormant wakati akiwa ni mwananchama wa kawaida msitegemee akichaguliwa ndio ataanza kuifanya kazi huko ni kujidanganya au mtafanya makosa kama haya ya arfi.
MANENO YA MTEI Kuhusu Arfi kujiuzulu
Akizungumzia akiwa nyumban kwake tengeru kuhusu hatua ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema (Bara), Saidi Arfi kujiuzulu,
Mtei alisema kuwa inafaa kiongozi huyo ajitazame upya na kujisahihisha badala ya kuwa mlalamikaji kila siku.
"Aache kulalamika kwa sababu, wakati alipochaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti mimi nilisimamia uchaguzi. Kama alikuwa na ndoto kwamba siku moja atakuwa mwenyekiti wa Chadema taifa alipaswa kujichunguza kwanza," alisema.
"Naunga mkono uamuzi wote wa Kamati Kuu, kuwasimamisha na kuwavua uongozi Naibu Katibu Mkuu wetu Zitto Kabwe na Dk Kitila Mkumbo."
Source: Mwananchi