Eng, nakupongeza kwa kumkumbusha huyu jaama. Yupo Mwandishi anajiita Mwalimu Mkuu wa Watu, yeye ansema kina Sitta na mitume wake na vita hewa ya ufisadi waliiisimamisha nchi kwa miaka mitatu na sasa wanataka kuisimamisha kwa wimbo wa CDM. Namshangaa na yeye anaingia kwenye lama dhidi ya maandamano ya Chadema wakati kilichofanya wao wasitishe kuandamana ni umati kidogo wa watu waliojitokeza Mbeya ukilinganisha na ule wa CDM. Fanyeni kazi ya kujenga nchi mwaka 2015 haupo mbaliJirani taratibu basi, na ujibu mada kama kiongozi si kishabiki utakuwa huna tofauti na wengineo...btw CDM inawakimbiza kwelikweli, mkilala mkiamka Magwanda, mkinywa chai , mkifuturu Shibuda, mkikesha mkisali Arusha...
Je CCM imeshika hatamu ili kujibishana na chama chenye theluthi tu ya wabunge wote ? Je mmepewa hii dhamana ili mkosoe tu chama cha upinzani ? Nadhani mmepoteza mwelekeo..huu ni wakati wa kufanya mambo mliyoyatolea ahadi au kama msemavyo 'ilani ya uchaguzi' mpaka tufike 2015 mtakuwa mnalalama na CDM mpaka hakuna cha maana tutakachokiona kwenu
Consider yourselves warned!