Muafaka CCM, CHADEMA waiva

Muafaka CCM, CHADEMA waiva

Yes I agree, wa kwanza ni Dr, Dr, Dr, JK, Dr, Mary Mwanjelwa, Dr Rwakatare, Dr Augustino Mrema n.k aaaaah nilitaka kusahau Dr Didas Masaburi, Dr Masumbuko Lamwai, Dr Mihanjo, Dr Mwakyembe, Dr Daud Balali, Dr, Benson Bana, Dr e.t.c. Tumethubutu, tumeweza, tunasonga mbele. Sikuwahi kufikiri kuwa kumbe majibu ni rahisi kiasi hiki. Umesahau Ma Prof nao wako wengi kama Prof Mukandala, Benno Ndulu, Kikula, Mlacha, n.k
Hongereni sana Mkuu
Thanx....we have the government too!!......mkitaka kuingia kitaa it's all good,tutachapana vilevile.
 
Ndipo fikra zako zilipoishia?? wakati mwingine kukaa kimya ni busara zaidi...

Naongea na aliye kuajiri wewe kaa pembeni, kuna wakati na maneno ya kuongea na Mbwa au Mwenye mbwa naomba ujue hilo, mwache mwenye mbwa ajibu wewe kaa pembe kwanza muda wako haupo mbele yangu, umeshawai kuona nimekuuliza au nimechangia hoja yako yoyote?, sijawai na sitakuja kuwai maana wewe si wa stahili yangu.
 
Nape Mi sina heshima yeyote na wala siitaji heshima aina hiyo unaidhani na kufikiri nina heshima kubwa mbele za Mungu wangu na sehemu ambazo watu wanatumia ubongo zaidi kuliko mdomo! kama nilivyokwisha kusema ndivyo unavyothibitisha hapa labda ujiulize mwenyewe wajumbe waliokuwa wanachaguliwa na M/Mkuu kuingia NEC walikuwa wanamwakilisha nani katika vikao vya NEC? au kwa lugha rahisi wanamwongoza nani? katika shughuli zao za kila siku? Ulikuwa Kiongozi wa NEC! au Kiongozi wa M/Mkuu!?

Wewe hujawai kuwa kiongozi mahala popote Nape, huo ndio ukweli labda kama wewe dhana yao ya neno uongozi inakinzana na maana halisi ya uongozi, maana hata Qadhaffi alikuwa anasema yeye ni kiongozi wa Libya ingawa walibya walikuwa hawajampigia kura hata siku moja.
Nape haoni tofauti ya kiongozi na mtawala, kwanza ukatibu uenezi wake si wa kitaifa.
 
Nape unapaswa kumwomba radhi KIKWETE ambaye ni m/kiti wa chama chako kwa kusema kuwa ana majungu kwani nimeiona barua ya msajili rais alipewa nakala na PINDA NA AKARIDHIA LEO UNAPOSEMA NI MAJUNGU NI KUWA WAZIRI MKUU NAYE NI MAJUNGU KWANI NDIO ALIMWANDIKIA MSAJILI. :

Kwa taarifa yako MKAMA kashamjibu msajili utaficha wapi sura yako?

Kuhusu Arusha ni kuwa kwa mujibu wa sheria na kanuni hapakuwa na uchaguzi wa meya kwani taratibu ni kuwa lazima 2 ya 3 ya wajumbe wawepo ukumbini na wasaini mahudhurio ila kwa arusha hakuna kitu kama hicho .

Pili, madiwani waliomchagua meya hawakuitwa kwenye kikao na ndio maana wa CDM hawakuwepo kwani taratibu ni kuwa barua zinapaswa kwenda ndani ya siku 7, halikufanyika.

Mengine kesho, ila NNAPE KIRI UMEKURUPUKA KUJIBU GAZETI NA UMEWADHALILISHA VIONGOZI WAKO AKIWEMO M.KITI WAKO JK.KWA KUWAITA WAZUSHI .
 
Yes I agree, wa kwanza ni Dr, Dr, Dr, JK, Dr, Mary Mwanjelwa, Dr Rwakatare, Dr Augustino Mrema n.k aaaaah nilitaka kusahau Dr Didas Masaburi, Dr Masumbuko Lamwai, Dr Mihanjo, Dr Mwakyembe, Dr Daud Balali, Dr, Benson Bana, Dr e.t.c. Tumethubutu, tumeweza, tunasonga mbele. Sikuwahi kufikiri kuwa kumbe majibu ni rahisi kiasi hiki. Umesahau Ma Prof nao wako wengi kama Prof Mukandala, Benno Ndulu, Kikula, Mlacha, n.k
Hongereni sana Mkuu
Umemsahau Prof. Maji marefu.
 
Mbona huu ni upupu. Kesi kukaliwa vibaya ndio kitu gani? kwenye mdahalo umezungumza hilo hilo hata wakifungwa wao sio wa kwanza. Ila tambua yana mwisho haya. Sioni haja ya muafaka kati ya magamba na cdm muda ushapita. Hoja Uliyojenga hapo kawaambie chekechea sio watu walioenda shule.
 
Thanx....we have the government too!!......mkitaka kuingia kitaa it's all good,tutachapana vilevile.
Ngoja kwanza babu yenu aliyekuwa anawapa kichwa Afrika achapwe nasikia ameomba yaishe wanamme wamekataa.
 
lazima 2 ya 3 ya wajumbe wawepo ukumbini na wasaini mahudhurio ila kwa arusha hakuna kitu kama hicho ..

Mimi huwa najiuliza kama huko CDM kuna watu wanaojua taratibu kama wewe, inakuwaje wanaowaongoza ni wapuuzi? Maana hapo nilipo Bold kama wewe ungekuwa ni Lema aliyewatoa madiwani nje baada ya kusaini haya yote yasingetokea. Gombeeni nafasi za uongozi katika CDM muondoe upuuzi wa akina Lema maana una cost maisha na muda wa CDM.
 
Mpuuzi nini wewe, kama unamuuliza mwenye stahili yako kwanini usimfuate huko Lumumba? Kwanini uulize hapa kwenye jukwaa la jumuia, halafu stahili gani uliyonayo wewe, akili zako tu kutokana na unayoandika zinaonesha hazikutoshi. Kama unataka kuongea na Nape peke yakee tafuteni faragha yenu muongee huko uone kama kuna mtu atakuingilieni lakini ukija hapa unaongea na public. Wewe ni mpuuzi limbukeni na mshamba sana.
Arafat kakuambia sibiri kwanza aongee na mwenye mbwa kinachokufanya ubweke ni nini..
 
Umemsahau Prof. Maji marefu.

Hawajui tofauti ya vyeti na elimu ndio maana mtu anaweza kusema kuwa anaowasomi wengi wasio na tija ambao hawana uwezo wowote katika kusukuma durudumu la maendeleo.

Hii sababu ya kutokujuwa tofauti ya elimu na vyeti ndio inawasukuma kutafuta vyeti hata kwa fedha huku kichwani hakuna kitu. Ni ngumu sana ukiwa nchni kama USA au UK kujuwa kuwa mtu ni Prof au Dr hasa mkiwa Club, kwenye train au basi na hata ndani ya vyuo vikuu vyote vikubwa hata vile vya top ten. Lakini papers zao ndio dira za nchni zao na vyama vyao.

Soma coalition agreement ya Conservative Party na Liberal Democrats alafu soma tena ya CCM na CUF ujajuwa tofauti ya hawa watu wenye vyeti mia ubongo wa darasa la saba walivyo na matatizo na wanavyoburuza kipumbavu na upupu wao.

Utasikia Bungeni Mh Dr Eng ABCD..., mara Mh Dr xyz...., hata ma-nurse wanajiita ma-Dr.
 
Mpuuzi nini wewe, kama unamuuliza mwenye stahili yako kwanini usimfuate huko Lumumba? Kwanini uulize hapa kwenye jukwaa la jumuia, halafu stahili gani uliyonayo wewe, akili zako tu kutokana na unayoandika zinaonesha hazikutoshi. Kama unataka kuongea na Nape peke yakee tafuteni faragha yenu muongee huko uone kama kuna mtu atakuingilieni lakini ukija hapa unaongea na public. Wewe ni mpuuzi limbukeni na mshamba sana.

Ahaa Pole sana, imekuuma lakini ndio ukweli kama mwenye mbwa kaja kuna haja gani ya kuendelea kuongea na Mbwa wakati mwenyewe yupo?

Mi siku zote huwa sizozani na kelele za mbwa hata siku moja.

 
Ahaa Pole sana, imekuuma lakini ndio ukweli kama mwenye mbwa kaja kuna haja gani ya kuendelea kuongea na Mbwa wakati mwenyewe yupo?

Mi siku zote huwa sizozani na kelele za mbwa hata siku moja.



Low self esteem, ninao uwezo wa kupeleka haya mazungumzo huko unapopataka, tena nina nyenzo zoote ikiwemo ID zaidi ya 15 za kuja kutukana hapa, lakini kwa kuwa naheshimu haya yanayojadiliwa hapa nakuomba tena kwa unyenyekevu acha kutupeleka huko, nadhani kuna sehemu katika moyo wako mkunjufu wa kitanzania itakuwa imenisikia ahsante.
 
Low self esteem, ninao uwezo wa kupeleka haya mazungumzo huko unapopataka, tena nina nyenzo zoote ikiwemo ID zaidi ya 15 za kuja kutukana hapa, lakini kwa kuwa naheshimu haya yanayojadiliwa hapa nakuomba tena kwa unyenyekevu acha kutupeleka huko, nadhani kuna sehemu katika moyo wako mkunjufu wa kitanzania itakuwa imenisikia ahsante.

ECOLI Kumbe unaweza kuwa Mstaarabu! Hapo umeongea lakini ulivyoanza wewe ulidhani nitakaa kimia! Mi sina haja ya kuwa na ID zaidi ya moja.

Haya lete hoja sasa kwanini hamtaki mazungumzo? au mpaka mgogoro wa ndani uishe? Maana kweli kukaa na CDM kujadili mgogoro wa AR wakati nyie wenyewe mme elemewa na migogoro kila kukicha yataka moyo, hasa Septemba hii ambayo hamtavuka salama.
 
Haya lete hoja sasa kwanini hamtaki mazungumzo.

Yaani hapo ndipo hata Dr Slaa anashindwa kujustify, kwa nini mfanye mazungumzo na CCM? CCM si mahakama wala halmashauri, kama mna haja na mazungumzo au kama Mkuchika kakosea kwa nini ninyi msiongee na bosi wa Mkuchika ambaye tayari mnaendelea naye katika mazungumzo? Labda ingekuwa huyo mkurugenzi kaamua uchaguzi ufanyike na CCM wakakimbia hapo mngeweza kuihusisha lakini as it is now endeleeni na mahakama, mkurugenzi aliyepindisha uchaguzi kwa madai yenu, na madiwani wenu, acheni CCM ifanye shughuli zake kwa kuwa CCM si chama cha kushughulika na mgogoro wa halmashauri moja mwaka mzima wakati kinaongoza halmashauri karibu nchi nzima.
 
..., kwa nini mfanye mazungumzo na CCM? CCM si mahakama wala halmashauri, [...] kama Mkuchika kakosea kwa nini ninyi msiongee na bosi wa Mkuchika [ ... ]endeleeni na [...] mkurugenzi aliyepindisha uchaguzi [ ... ] acheni CCM ifanye shughuli zake kwa kuwa CCM si chama cha kushughulika na mgogoro wa halmashauri moja mwaka mzima wakati kinaongoza halmashauri karibu nchi nzima.

Kuna wakati kujadiliana nanyi inahitaji moyo sana. Maana nyie ni zaidi ya kinyonga.

Hayo maneno yako yanakinzana yenyewe mpaka napata mpaka hata siamini kama yanatoka kwa mtu mmoj au watu tofauti kila mmoja kaweka beti zake! maana inaonekana hapo hata Mkuchika si CCM tena ili mradi umejenga hoja yako. Na CCM si chama kilichoshikilia Dola hapa ili maradi kama unaweza kujenga hoja ili kuepusha CCM na lawama za watendaji wa Serikali?!

Sawa, Sasa huyo Bosi wa Mkuchika unayemsema ni yupi na yupo chama gani! Maana kama W/Mkuu ni CCM na ndiye aliyetowa maagizo kwa Tedwa juu ya kukalisha CCM na CDM kutatuwa hujuma za KiQadhaffi zilizofanywa AR.
 
Yaani hapo ndipo hata Dr Slaa anashindwa kujustify, kwa nini mfanye mazungumzo na CCM? CCM si mahakama wala halmashauri, kama mna haja na mazungumzo au kama Mkuchika kakosea kwa nini ninyi msiongee na bosi wa Mkuchika ambaye tayari mnaendelea naye katika mazungumzo? Labda ingekuwa huyo mkurugenzi kaamua uchaguzi ufanyike na CCM wakakimbia hapo mngeweza kuihusisha lakini as it is now endeleeni na mahakama, mkurugenzi aliyepindisha uchaguzi kwa madai yenu, na madiwani wenu, acheni CCM ifanye shughuli zake kwa kuwa CCM si chama cha kushughulika na mgogoro wa halmashauri moja mwaka mzima wakati kinaongoza halmashauri karibu nchi nzima.
Jaribu kuongoa kwa mantiki wakati CCM wanaongea na Kafu kule zanzibar Kafu ilikuwa mahakama.
 

Kuna wakati kujadiliana nanyi inahitaji moyo sana. Maana nyie ni zaidi ya kinyonga.

Hayo maneno yako yanakinzana yenyewe mpaka napata mpaka hata siamini kama yanatoka kwa mtu mmoj au watu tofauti kila mmoja kaweka beti zake! maana inaonekana hapo hata Mkuchika si CCM tena ili mradi umejenga hoja yako. Na CCM si chama kilichoshikilia Dola hapa ili maradi kama unaweza kujenga hoja ili kuepusha CCM na lawama za watendaji wa Serikali?!

Sawa, Sasa huyo Bosi wa Mkuchika unayemsema ni yupi na yupo chama gani! Maana kama W/Mkuu ni CCM na ndiye aliyetowa maagizo kwa Tedwa juu ya kukalisha CCM na CDM kutatuwa hujuma za KiQadhaffi zilizofanywa AR.

Sasa hapa naona kazi inakuwa ngumu, maana nilikuwa sijui hata uelewa wa masuala ya msingi kama, serikali na chama upo wapi. Sina maneno rahisi ya kulieleza hili zaidi ya haya, Kikwete tunapomuita Rais inamaana ni kiongozi wa serikali na tunapomuita mwenyekiti wa CCM ni kiongozi wa chama.

Hii ni dhana rahisi sana, mtu mmoja anaweza kuwa na role zaidi ya moja, mfano Mengi ni mwenyekiti wa makampuni ya IPP lakini pia ni baba. Mwanawe Regina ni mfanyakazi wa IPP, inategemea na mazingira lakini Mengi anaongea na Regina wakati tofauti tofati kama baba na mazingira ya kazi anaongea na mwanawe kama bosi wake. Ndivyo ilivyo kwa serikali na chama, chukulia Mkuchika ni mtoto wa CCM na CCM ni baba kwa Mkuchika.

Lakini pia CCM ana duka linaitwa serikali, sasa Mkuchika akitumwa kuuza duka baba yake kama muajiliwa tayari anakuwa na mahusiano ya aina mbili na CCM (yaani baba na bosi reje mfano wa regina na Mengi). Sasa ukigombana na Mkuchika labda kakuchulia mpira mliokuwa mnachezea, unapokwenda kushitaki kwa CCM hapa unakuwa unatumia ile mamlaka ya uzazi yaani baba. Lakini kama wateja wakikuta duka halijafunguliwa hawaendi kumuambia CCM kama baba bali bosi.

Nilitumia mfano huu kwa wanafunzi wa mwaka wa pili chuo kikuu wakanielewa naa assume na wewe unaweza kuelewa. Ushauri wangu kabla hata hujaenda huko kwenye masuala ya chaguzi anza kwanza kujifunza hizi dhana, maana ni lazima uweze kuzitofautisha la sivyo hutaelewa kwa nini Pinda ni muhisika mkuu kwenye chaguzi za halmashauri na Mukama.
 
Jaribu kuongoa kwa mantiki wakati CCM wanaongea na Kafu kule zanzibar Kafu ilikuwa mahakama.

CCM na CUF waliona kuna mgogoro unaohitaji kusuluhishwa wakati huo, hapa pande zinazovutana hazi husishi CCM(labda serikali yake) kwa hiyo hakuna haja yao wao kwenda kusuluhishwa, in short CCM haina matatizo na CDM huko Arusha kwa hiyo hata wakienda mezani wao wataweka nini mezani. Maana ili kusuluhishwa na lazima kila upande uwe na madai sasa napata shida kuyaona madai au tuhuma za CCM. Kwa kuwa hata kama walishiriki uchaguzi basi wakuulizwa ni yule aliyewaita. Sioni sababu gani CCM inahusika.
 
Back
Top Bottom