Jogi na wenzako,
KWANZA NI VIZURI SANA KULIJUA TATIZO LA ARUSHA BILA USHABIKI WA KISIASA. HIVI NINI SABABU YA CCM NA CHADEMA KUKAA MEZANI HASA KWA VIONGOZI WA KITAIFA.. UGOMVI ULIOPO NI KATI YA CHADEMA NA MADIWANI WAKE WA ARUSHA....CCM INAINGIAJE HAPA?
Nape,
Mimi ni kijana mwenzako.
Kuwepo kwa wingi wa wapenzi wa CHADEMA au CCM hakutuzuii watu kama mimi tusiotaka kabisa kuwa na Chama tuhoji maswali ambayo mnaweza kudhani tunaegemea wapinzani wenu.
Kumbuka wengine tuna asili ya kudadisi kila kitu hadi kupata ukweli yaani kila kitu kwangu ni research. Nilimsikiliza kwa makini Prime Minister akijibu lile swali bungeni na yule dada (nimemsahau) aliyeuliza akaongeza kuwa "
kwa kuwa CHADEMA ni waongo kuhusu Arusha, wewe kama Waziri Mkuu una ushauri gani kwa madiwani waliofukuzwa".
Hebu ona hapa. Huyu dada na sehemu ya kubwa ya bunge ni kama walituambia kuwa kinachotoka kwenye mdomo wa Pinda ndiyo
definitive truth. Kuna tofauti gani na kusema "
Zidumu fikra sahihi za Waziri Mkuu" . Sasa fikra hizohizo zimewatokea puani hata wiki mbili hazijapita. Leo
truth holder yuleyule Pinda anasema angechukua uamuzi kuhusu Jairo, wiki mbili baadaye eti tunakuja juu kadhalilishwa. Binafsi nimefurahi yaliyotoke bungeni ili iwe fundisho kwa kauli rahisirahisi zinazohitaji tafakari kubwa.
Kinachozungumzwa kwenye thread hii ni kwamba barua imetoka kwa Tendwa inaenda CCM na CHADEMA. Wote wewe na CCM wenzako pamoja CHADEMA ni reciepient wa hiyo barua. Walichofanya wenzako CHADEMA ni
ku-publicize content za barua ambapo na sisi walau tunajua kuwa chini ya Tendwa mtakutana timu za CCM na CHADEMA. Tulikuwa hatujui sasa tumejua kilichomo.
CHama Chako kiliwahi kuficha ukweli kwamba sera ya bunge bado ni serikali mbili. Pius Msekwa akatoboa mbele ya waandishi kuwa "
sasa serikali tatu ni sera kamili ya bunge". NIlikuwa mdogo hiyo 1994 ikitokea hii a G55 lakini ninacho kitabu cha Nyerere kiitwacho "Uongozi wetu na Hatima Ya Tanzania", namini unacho na kifungue ukurasa wa 19 uone.
Tulidhani kijana mwenzetu utaondokana na hii fichaficha ambayo mwishowe ni kuumbuka tu. TUliamini hivyo ulivyoanza kwa speed na viwango kana kwamba unaondokana na fichaficha uliposimamia maamuzi ya NEC yako kuhusu magamba. Leo unarudi kulekule kwa kitu kidogo sana kwa barua ya Tendwa ambayo imesambazwa kwa wadaua wengi. Je, ingekuwa imesambazwa kwako tu ingekuwaje?
Kinachojadiliwa humu ni content za barua ile. Nimesema sina haja ya kupendwa na CCM au CHADEMA. Ukinithibitishia kuwa CHADEMA wanaongopa kwamba content za barua si kama wanavyoeleza basi mimi binafsi nitaanziasha thread nyingine ikisema
NAPE AIUMBUA CHADEMA KUHUSU BARUA YA TENDWA.
Na kama kweli hamuhusiki huko Arusha, hiyo barua inawataka nyinyi na CHADEMA mjadili nini. Kama unaamini kuwa mgogoro ni masuala ya ndani a CHADEMA na kwamba CCM mnaweza kualikwa basi ninakumbuka mwaka jana CCM mlialikwa kwa masuala ya ndani ya CHADEMA ambapo wewe ulkwenda na ukapokewa kwa furaha na vijana wa CHADEMA wakisema "njoo moja kwa moja" na wewe ukiwajibu "NImetumwa kumwakilisha Makamba". Hukukataa. Ulishiriki shughuli yao na sisi wafuatiliajia wa magazeti tukaona picha yako katikati ya wana-CHADEMA wakikushangilia.
Barua hiyo ya Tendwa siyo confidential. Wewe ni mwana JF nakupongeza kwa hilo. Hivyo kama CHADEMA ni waongo basi scan hiyo barua tutumie humu na kama nilivyosema nitakuwa wa kwanza kumlipua Slaa na wenzake.
Na kama hamhusiki kabisa, basi tutangazie wazi kuwa hakuna duniani mwene mamlaka ya kuwakutanisha nyie na CHADEMA hapa duniani kwa sababu mko kwenye mstari wa haki. Ukitutangazi hivyo nitakuwa wa kwanza kuwashambulia humu wanaokushambulia.
Jogi na wenzako,
TUNAJUA MEYA KACHAGULIWA KIHALALI NA MANISPAA INAENDELEA KUJENGWA, IKIZINGATIWA KUWA ILANI INAYOTEKELEZWA NI YETU , HATUNA MUDA WA KUJADILI WALA KULUMBANA KWA MIGOGORO ISIYOTUHUSU...TUNASUBIRI HIZO SIKU 30 ZA WATANI ZANGU...
TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE.
Tuletee kopi ya kanuni zote kuhusu uchaguzi wa meya Arusha. Hata kama ziko kanuni 200 wewe fanya jambo moja dogo sana. Tia tick kwenye kila moja kuonyesha kwamba CCM iliikamilisha kanuni ile bila utata. Mimi sina uvivu wa kusoma. Nimesema fanya hivyo hata kama ziko 200, lakini hata zikiwa 500 na nikaona tick yako imepita kwenye zote hizo bila hata moja kuvunjwa, basi nitakuwa wa kwanza kuwashambulia CHADEMA kuwa wamesababisha vurugu bure huko Arusha kiasi cha kufanya AICC ipoteze umaarufu kwa ukumbi wa Mlimani City wa pale Dar.
Ni hayo machache na ambayo ninaamini kwa uwezo wako kama kijana mwenzangu kwa nafasi yako nawe utayaona ni marahisi na utanitimizia.
Karibu na kidumu
Chama Cha Mapinduzi.