Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Watu watatu wakazi wa kijiji cha Mahurunga kilichopo wilayani Mtwara, Mkoani Mtwara wamefariki baada ya kushambuliwa na nyati wakiwa shambani
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani humo ACP Nicodemus Katembo ametoa taarifa hiyo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari ambapo ameeleza kuwa tukio hilo limetokea Machi 20 Saa 5 Asubuhi wakati watu hao wakiwa shambani
ACP Katembo amewataja watu hao kuwa ni Rashid Bakari (40) Mkazi wa Kijiji cha Kitunguli, Salum Yusuf (46) na Said Musa (45) Wakazi wa Kijiji cha Mahurunga
Taarifa hiyo ya Jeshi la Polisi imeendelea kufafanua kuwa baada ya watu hao kushambuliwa taarifa zilifika kwa Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wanaolinda mpaka ambao walifika haraka eneo la tukio na kumuua Nyati huyo ambapo baada ya uchunguzi wa kitaalamu miili ya marehemu hao ilichukuliwa na ndugu kwa ajili ya mazishi na kuwataka wananchi kutoa taarifa wanapoona wanyamapori katika makazi ya watu
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani humo ACP Nicodemus Katembo ametoa taarifa hiyo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari ambapo ameeleza kuwa tukio hilo limetokea Machi 20 Saa 5 Asubuhi wakati watu hao wakiwa shambani
ACP Katembo amewataja watu hao kuwa ni Rashid Bakari (40) Mkazi wa Kijiji cha Kitunguli, Salum Yusuf (46) na Said Musa (45) Wakazi wa Kijiji cha Mahurunga
Taarifa hiyo ya Jeshi la Polisi imeendelea kufafanua kuwa baada ya watu hao kushambuliwa taarifa zilifika kwa Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wanaolinda mpaka ambao walifika haraka eneo la tukio na kumuua Nyati huyo ambapo baada ya uchunguzi wa kitaalamu miili ya marehemu hao ilichukuliwa na ndugu kwa ajili ya mazishi na kuwataka wananchi kutoa taarifa wanapoona wanyamapori katika makazi ya watu