Masasi: Watu 6 wafariki kwa kupigwa na radi kwenye sherehe ya kijana wao aliyemaliza kidato cha nne

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,076
49,785
Watu 6 wamefariki papohapo Kwa kupigwa na Radi huku wengine wakijeruhiwa walipokuwa kwenye sherehe ya kumpongeza Kijana wao kuhitimu form 4 huko Kijijini Maparagwe.

-

Watu sita wamefariki dunia na wengine watano kujeruhiwa wilayani Masasi, mkoani Mtwara baada ya kupigwa na radi wakati wakiwa kwenye sherehe ya kumpongeza kijana wao aliyehitimu kidato cha nne mwaka huu.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa ACP Nicodemus Katembo kwa Wahandishi wa Habari ameeleza kuw, tukio hilo limetokea jana Novemba 3, 2023 saa 12 jioni katika kijiji cha Maparagwe, kata ya Chikukwe wilayani Masasi.

Amewataja waliofariki kuwa ni Patrick Said Maurus (42), Fatuma Rashid (40), Rosina Wales (46), Regina Vicent (55), Zainabu Abdulrahman (62) na Zainabu Mussa (44).

Na kwa upande wa majeruhi amesema waliojeruhiwa ni Amina Abdulrahman (62), Haiman Fafhili (04), John Nguli (39), Luiz William (36), na Mzamiru Said (2).

Majeruhi hao wamelazwa katika hospitali ya Ndanda na wakiendelea kupata Matibabu.


Chanzo: Kusini Yetu online

My Take

Chukueni tahadhari, mvua huja na madhara ya vifo vya Radi na Mafuriko.

R.I.P wafiwa na tunawaombea majeruhi wapone haraka.
 
Huu mtindo wa kufanya sherehe za kuimaliza form 4 kumbe umeshika Kasi namna hii? Baada ya miaka kadhaa kutakuwa na sherehe za kumaliza chekechea
 
Ne
Huu mtindo wa kufanya sherehe za kuimaliza form 4 kumbe umeshika Kasi namna hii? Baada ya miaka kadhaa kutakuwa na sherehe za kumaliza chekechea
Nenda Mbinga Mkoani Ruvuma,hizo za kuhitimu chekekea zipo na zilianza miaka kadhaa.
Nadhani hizi sherehe uchwara zimetamalaki sana hasa maeneo ambayo miundombinu ya mawasiliano ni duni,jamii inaishi kwa kuoneshana,hakuna viwanja vingi vya kujidai,zingine ongezeni lkn vikundi vya akina mama ambo suala la kufiwa ndipo mwanachama huchangiwa ama hupewa kiasi kikubwa cha fedha kuliko matibabu ndio chanzo cha sherehe za kipuuzi km hizo.
 
Watu 6 wamefariki papohapo Kwa kupigwa na Radi huku wengine wakijeruhiwa walipokuwa kwenye sherehe ya kumpongeza Kijana wao kuhitimu form 4 huko Kijijini Maparagwe.

-
Watu sita wamefariki dunia na wengine watano kujeruhiwa wilayani Masasi, mkoani Mtwara baada ya kupigwa na radi wakati wakiwa kwenye sherehe ya kumpongeza kijana wao aliyehitimu kidato cha nne mwaka huu.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa ACP Nicodemus Katembo kwa Wahandishi wa Habari ameeleza kuw, tukio hilo limetokea jana Novemba 3, 2023 saa 12 jioni katika kijiji cha Maparagwe, kata ya Chikukwe wilayani Masasi.

Amewataja waliofariki kuwa ni Patrick Said Maurus (42), Fatuma Rashid (40), Rosina Wales (46), Regina Vicent (55), Zainabu Abdulrahman (62) na Zainabu Mussa (44).

Na kwa upande wa majeruhi amesema waliojeruhiwa ni Amina Abdulrahman (62), Haiman Fafhili (04), John Nguli (39), Luiz William (36), na Mzamiru Said (2).

Majeruhi hao wamelazwa katika hospitali ya Ndanda na wakiendelea kupata Matibabu.


Chanzo: Kusini Yetu online

My Take
Chukueni tahadhari,mvua huja na madhara ya vifo vya Radi na Mafuriko.

R.I.P wafiwa na tunawaombea majeruhi wapone haraka.
Radi ni mtihani sana
 
Back
Top Bottom