Mtwara kumekucha; Maandano ya kupinga kusafirisha gesi yaja

Status
Not open for further replies.
swali zuri sana,tunataka zile ahadi walizotuambia kua baada ya kugundua gesi,kuwa viwanda vingi vitajengwa,gesi itabaki,na viwanda vya kutengeneza gesi ya matumizi ya majumbani vitajengwa huku,na viwanda mbalimbali,mfano leo kusini ndio umeme haukatiki mikoa mingine ina tatizo la umeme tokea ishu ya Richmond,na mpaka leo umeme dar,arusha aujatulia,kwanini viwanda aviletwi kusini

Jamani watu wa kusini acheni ubinafsi. Kumbukeni kuwa viwanda vyewenye ni vya kutegemea wawekezaji kwahiyo mtakuwa hamwuatendei haki waTZ wenzenu mkigomea gesi isiende DAR. DAR ndo kuna viwanda vingi na pia itatumika kuzalisha umeme wa gridi ya taifa ili kuondoa tatizo la umeme nchi nzima. Nyie sasa hivi mnajinoma na umeme wa Artumas tena kwa bei chee na umeme wenu kama mko Ulaya vile maana haukatiki. Wahurumieni waTZ wenzenu nao wapate nishati ya uhakika. Pia kuna ndugu zenu wengi tu waonaofanyakazi kwenye viwanda huko DAR. Viwanda vitakuja pole pole kwa kadri wawekezaji watakapoona fursa ya kuwekeza huko kwa maana hata mkiikatalia hiyo gesi si kwamba ndo wawekezaji watakuja kesho na kuanza kujenge viwanda kama mnavyodai.
 
Kwanza, nawaombeni watu wa kusini kuwa kesho muwe makini sana na vitu vyenye ncha kali na pili, nafikiri huu ni upepo na utapita tu!
 
kama wananchi hiyo gesi wanaitaka kwa ajili ya matumizi gani hasa.

Wananchi lazima iwakomboe kwa ajili ya kupikia. Ila si wananchi Wa kusini tu, watanzania wote lazima wawezeshwe kupikia gesi.

Nachowashauri watu wa kusini waombe mgao wao kama watu Wa kusini.
 
Watu wa kusini nendeni shule nyie. Acheni ubinafsi na uchoyo usio wa maana. Hivi kila mtu akisema ang'ang'anie kilicho chake, tutafika kweli?
 
Swali la kitoto kweli ilo....I notice smthing on you.

I guess Akili yake ni ndogo ya majibu mepesi kwenye masuala magumu kama haya, Kama Kaka Yake Mkuu wa Nchi hii I mean JK, tumefika hapa tulipo kwa ajili ya udhaifu wa Rais Kikwete na watendaji wake sasa ni zamu yetu wananchi kusimama na kusema kuwa tumevumilia vya kutosha, mmetunyanyasa vya kutosha hatuko tarari kuendelea kuvumilia ujinga wenu tena. Wasambaa wanasema kama mbwahi mbwahi tu.
 
Wananchi lazima iwakomboe kwa ajili ya kupikia. Ila si wananchi Wa kusini tu, watanzania wote lazima wawezeshwe kupikia gesi.

Nachowashauri watu wa kusini waombe mgao wao kama watu Wa kusini.

Nadhani we are so clear hatuna wakugawana nae we need our own resource itukomboe mali na raslimali za kaskazini zimetumika huko na sasa hii kwa nini ichukuliwe kama keki ya taifa?? Kusini kwanza Tanzania baadae, tumechoka na mambo ya Kuendelea kukandamizwa hata hapa tunapoona fursa ya kukwamuka napo bado wakandamizi wanataka kuendelea kutukandaza, enough is enough.
 
Hivi kabla ya gesi Mtwala walijua mahitaji yao yanatoka mikoa ippi!?
Bado kidogo dsm watazuia mapato yao,mza dhahabu na samaki zao,kirimanjaro na mrima wao,mara na arusha na mbuga zao nk je tutafika!!!?
 
40% of GDP ni kutoka dar,sasa bomba likipelekwa kuna shida gani?ila kuibana serikali ihamasishe uwekezaji huko pia ni sawa sawa
 
Ujumbe umefika lakini niwaombe muache bomba liendelee ili faida itakayopatikana iwarudie. kwa bahati Dar inawakilisha watanzania wengi na vingi vitu huletwa hapa kutoka mikoani; bidhaa nyingi hutengenezwa hapa Dar na huenda kila mahali pamoja na Mtwara. gesi itaawanufaisha pia watu wa Mtwara. Kwa kweli ujumbe wenu unaeleweka gesi ije lakini simamieni suala lenu la msngi.
 
Jamani watu wa kusini acheni ubinafsi. Kumbukeni kuwa viwanda vyewenye ni vya kutegemea wawekezaji kwahiyo mtakuwa hamwuatendei haki waTZ wenzenu mkigomea gesi isiende DAR. DAR ndo kuna viwanda vingi na pia itatumika kuzalisha umeme wa gridi ya taifa ili kuondoa tatizo la umeme nchi nzima. Nyie sasa hivi mnajinoma na umeme wa Artumas tena kwa bei chee na umeme wenu kama mko Ulaya vile maana haukatiki. Wahurumieni waTZ wenzenu nao wapate nishati ya uhakika. Pia kuna ndugu zenu wengi tu waonaofanyakazi kwenye viwanda huko DAR. Viwanda vitakuja pole pole kwa kadri wawekezaji watakapoona fursa ya kuwekeza huko kwa maana hata mkiikatalia hiyo gesi si kwamba ndo wawekezaji watakuja kesho na kuanza kujenge viwanda kama mnavyodai.

Almas, Tanzanite, Dhahabu, na Madini mengine hebu tuambie toka kwenye haya madini sisi wa KUSINI tumepata nininhasa?? Tumechoka na Kauli za kinafki za kusema tuache ubinafsi, Miaka 50 ya uhuru Mtwara bado mvua ikinyesha haifikiki bado mnasema ubinafsi? Acheni umangi meza na kuona wapi pana ukweli na wapi watu wanakandamizwa!!! Hatu taki kufika mahala mtulazimishe kufanya ambayo hatuyawazi kwa sasa ila if u push us we will do that for sure.
 
40% of GDP ni kutoka dar,sasa bomba likipelekwa kuna shida gani?ila kuibana serikali ihamasishe uwekezaji huko pia ni sawa sawa

real I hate to see some cant see tumekandamizwa toka uhuru na sasa tunapata fursa bado kuna wapuuzi wanata kuendelea kuuona ukandamizaji wa mikoa ya kusini unaendelea. we will fight for our rights till the last blood drop we shade.
 
Almas, Tanzanite, Dhahabu, na Madini mengine hebu tuambie toka kwenye haya madini sisi wa KUSINI tumepata nininhasa?? Tumechoka na Kauli za kinafki za kusema tuache ubinafsi, Miaka 50 ya uhuru Mtwara bado mvua ikinyesha haifikiki bado mnasema ubinafsi? Acheni umangi meza na kuona wapi pana ukweli na wapi watu wanakandamizwa!!! Hatu taki kufika mahala mtulazimishe kufanya ambayo hatuyawazi kwa sasa ila if u push us we will do that for sure.

Hata unachoongea hukielewi wewe. Hebu nenda huko kwa wasukuma wenzangu kawaulize wananufaikaje na hizo almasi na dhahabu kama si kufukuzwa kwenye ardhi zao na wengine kufukiwa wakiwa hai kwenye mashimo kisa wamegoma kuwapisha wawekezaji. Zaidi ya hayo wananyweshwa maji yaliyochanganyikana na kemikali za sumu toka migodoni na kuna watu wengi tu hii leo ni wagonjwa kwa kunywa sumu hizo. Angalia migogoro ilivyo huko Mara karibu na migodi ya dhahabu, sasa sijuwi unaongea nini wewe. Zaidi sana wanapata mgao kidogo kwa mwaka kwa ajili ya maendeleo ya eneo husika na migao hiyo jamaa walikuwa hawatoi mpaka Muhongo amekuja kuwakurupusha. Kama ni ajira huenda hata ndugu zenu wengi tu toka huko kusini wameajiriwa kwenye haya makampuni ya madini. Tena kaka yenu Mkapa ndo kanufaika zaidi na haya madini maana ndo aliyesaini mikataba ya kinyonyaji ili yeye awekewe pesa huko Uswisi. Ukisema mvua ikinyesha Mtwara haifikiki sijuwi wewe umefika Mtwara mara ya mwisho lini, kwa maana kama bado basi ni kipande kidogo sana Mtwara iunganike na DAR kwa lami. Mkuu acheni gesi iende DAR inufaishe taifa zima.
 
Wananchi wanaona,wamejifunza Watawala bado wamelala.
Kanda ya ziwa wawekezaji wameingi kuchimba dhahabu,mikataba mibovu tena inasainiwa Dar Es Salaam,na wadau hawakushirikishwa,hawajalindwa na mikataba hii ya uwekezaji.

Ukiona,na kutathimini utakuta CCM kanda ya ziwa inapingwa na wananchi,na CDM meendelea kuwa mshindani mkubwa.kwasababu ya makosa yaliyofanyika katika uwekezaji sekta ya madini,huku wananchi wakiona wanaporwa haki na maliasili yao(madini).

Mtwara na Mikoa ya Kusini,itakuja kuwa maeno magumu kwa Watawala siku za usoni,kwani Serikali imeshindwa kuweka vipaumbele vya kunyanyua hali za maisha ya wananchi wa kawaida.

Bado,wananchi wanashangaa kauli za Serikali zenye kubadilika;mfano ilisemekana umeme ungezalishwa na ARTUMAS kwai cha MW 300,kiwanda cha simenti ,mbolea vingejengwa Mtwara.Lakini sasa imekuwa kimya badala yake Gesi inasafirishwa kwenda DAR kwa watumiaji wakubwa,sawa lakini kwa nini mpango wa uzalishaji umeme kwa gesi usiwepo ili kusaidia Mikoa ya Kusini hadi Ruvuma na hatimaye GRID ya Taifa?!

Kibaya zaidi matokea ya upatikanaji wa mafuta hayapo wazi,Kenya na Uganda wameweka wazi matokeo ya upatikanaji wa mafuta,sisi tuna tatizo gani?
 
maandamano yasio na tija wala faida.
Mnalia umeme kila siku mnategemea mtambo
aliofungua jk pale kinyerezi utatumia maji kuzalisha umeme?
Gesi tayari inatumika mtwara mna mtambo wa kuzalisha
umeme mbona nyumba zenu za nyasi na makuti hamjaweza kutumia umeme?
Tukiwawekea processing industry mtwara nmategemea kupata ajira wakati hamtaki kusoma?
Si ndio nyie mko dar mnajiita wamachinga? Mbona mmekimbia kwenu?
Kuna mama ntilie wa kigeni kwenye zile blocks za kuchimba gesi ndio wanagawa vyakula kule
mlishaomba hizo tenda mkanyimwa??

Mnajidanganya tu madini,gesi na mafuta ni kwa manufaa ya watanzania wote, rudini darasani
mkasome mjue namna ya kutumia rasilimali na kuepusha mikoa yenu na umaskini
mna ardhi yenye rutuba, mna korosho hata kuzipalilia hamwezi

mikoa yenu wangepewa wasukuma,wanyakyusa na wachaga ingekuwa mikoa tajiri.
Kila siku mnavaa nguo za kijani mnaimba chama chajenga nchi mnalalamika nini
maji mmeyavulia nguo ingieni muoge bakini na umaskini wenu
hata mkipigwa mabomu mmeyataka wenyewe

atakaetukana na atukane ukipigwa bun shauri yako mmezidi uvivu afu mnataka bwerere
kaeni vijiweni endeleeni kunywa gahawan gesi lazima ije dar penda msipende



mbona unakimbilia kujidefend kwa kuwaasa watu wasikutukane kwa kuhofia ban??

Si kwa sababu unajua ulichokiandika ni upuuzi na wenda wazimu??

Nani amtukane mwendawazim?kumtukana mwendawazim ni kujitia wendawazim tuh
kaokote makopo,wenyewe tunajua tunachokipigania
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom