Mwana Mtoka Pabaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2012
- 15,117
- 16,500
Najiuliza maswali makuu mawili na sipati JIBU
1. kwanini serikali ina arakisha huumradi kabla yakutatua matatizo yaliyopo ?
2. kwanini huu mtambo wa umeme usijengwe mtwara umeme ukasafirishwa kuja Dar? mbona uliweza kutoka kidatu ukaja dar hapo mtwara tumeshidnwa nini ?
Pinda aliposema mpigwe, hakuwa amekosea kwa 100%, akili km zako hazina tiba zaidi ya kichapo kikali. Haya maswali ni ya kipuuuzi kweli kweli. Sidhani kama maswali haya hayajawahi kujibiwa ni vile tu ili uelewe ni lazima udhamirie kuelewa.
GESI SIO UMEME PEKE YAKE. Utakuwa ni ujinga usio na kipimo kuzalisha umeme Mtwara halafu uusafirishe hadi Dar baadaye wewe huyo huyo usafirishe gesi nyingine kwa ajili ya matumizi yaliyobaki. Wengi wenu mnaofikiri kwa kutumia viungo vya kukalia mnadhani kuna tija Power Plant kwenye mji wako.
Umeme unaozalishwa Kidatu unazalishwa kwa maji na hatuna mahitaji ya maji toka Kidatu na ukumbuke maji yanazalisha umeme kwenye maporomoko kwa hiyo huwezi kuyasafirisha na kuuzalishia umeme sehemu nyingine ambapo hakuna maporomoko.
Labda nikuulize swali wewe na wengine wenye akili kama zako: Kwa mitambo ile ya umeme kuwepo pale Kidatu, ni nini wananchi wa Kidatu wanafaidika?
Tutumie akili zaidi ya ushabiki na upuuzi.