Nimekuelewa vizuri,na umenijibu vizuri na nimekufahamu kwa kisasi kuliko post yako ya kwanza ilivyokaa.Sasa kuhusu uhalali wa mafuta umesema siyo mada,niliheshimu hilo.
Lakini sijui kama umefika kwenye level ya ukimsikiliza mtumishi fulani kwa muda yanakuwepo mawasiliano na unashuhudiwa na Roho ya kuwa huyu anachofundisha ni kweli ingawa sikatai ya kwamba anaweza kukengeuka mbele ya safari.
Ukisikiliza video za walionusulika wanasema mambo yalikuwa safi ila walipoanza kukanyaga mfuta ndiyo shida ikatokea,nielewe nilipoandika Mungu muda mwingine huongea na wanadamu ila hushindwa kumwelewa.
Niliposema issue ya Mwamposa yule mtumishi wa Mwanza (Malisa) ameilinganisha na Ayubu pale hakutumia maandiko kwa usahihi kwa sababu Ayubu alipoteza watoto wake wa damu na mali zake hapo Kilimanjaro Mwamposa hajapoteza watoto wake wa damu au mali zeke kama ambavyo Ayubu alipoteza.Nilitaka upate picha ambavyo muda mwingine Neno la Mungu linatumiwa vibaya.Sikumanisha lile siyo jaribu kwake,na kama tunaliita jaribu kama ulivyosema ,je maandiko yanasemaje kuhusu majaribu kama ulivyoliita?Je Mungu humjaribu mtu au shetani?Au tamaa zake mwenyewe?
Kuna swali mitume na manabii wengi hawapendi kuulizwa?Swali hili ni muhimu kwa kila anayejiita mtumishi wa Mungu ajue majibu yake.
Mathayo 16:13-17
":13 Yesu alipofika pande za Kaisarea Filipi, aliwauliza wanafunzi wake, “Watu wanasema Mwana wa Mtu kuwa ni nani?” 14 Wakamjibu, “Wengine wanasema kuwa ni Yohane mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.” 15 Yesu akawauliza, “Na ninyi je, mwasema mimi ni nani?” 16 Simoni Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.” 17 Yesu akasema, “Heri wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana si binadamu aliyekufunulia ukweli huu, ila Baba yangu aliye mbinguni. "
Leo kwa mfano useme jina la mtumishi fulani wa Mungu,watu watakuambia huyo ni tapeli,huyo ni mwizi.
Je watanzania wanasema Mwamposa ni nani?Yesu tofauti na watumishi wa siku hizi alikuwa tayari kujua watu wanasema yeye ni nani,kama angekuwa Yesu ni tapeli tungeambiwa lakini walisema ni Eliya,wengine Yohana mbatizaji etc,baada ya kupata majibu ya watu wa nje,akawauliza wafuasi wake.Simoni Petro akapatia,ya kuwa Yesu ni Kristo.Heri wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana si binadamu aliyekufunulia ukweli huu, ila Baba yangu aliye mbinguni. ,sasa unasemaje wewe binafsi juu ya watumishi ambao watu wanasema ni matapeli,wapiga madili?Je tuyapuuze majibu ya hawa watu ikiwa Yesu mwenyewe alitaka kujua watu wanamsemaje sisi tunaojiita watumishi hili eneo hatutaki kusikia watu wanasemaje?Something is not right somewhere. Nakubaliana na uliyoandika ila nimalize kwa kuwaonywa wakristo hizi ni nyakati za hatari,kuwa makini na mahali unapoabudu,tumia muda wako kujifunza Neno la Mungu kwani ni taa na litakuponya.
Niliposema baba zao wa kiroho tunaweza kuwajua?Sikuwa na maana kama baba zao wako sahihi au hawako sahihi,lengo langu ni tujue chanzo cha imani hizo ,tujue lini mafuta yalianza,na nani alianza kuwapa watu mafuta.
Mimi sijafuatilia kujua Mwamposa historia yake ,lakini wengine kama Prophet Shillah atakuambia baba yake ni prophet Bushiri,sasa kama kuna mwingine baba yake ni TB Joshua watu wanaojua watujuze.Ukijua baba yake ni rahisi kujua mtoto alivyo amejifunza wapi.
Nakubaliana na wewe ya kwamba Roho mtakatifu ndiyo mwalimu sahihi,na ni kweli maandiko yanataka tuongozwe kwa Roho,lakini kabla huyo Roho hajakuongoza si kuna mtu alikufundisha Neno,si Kuna mtu alikuongoza sara ya Toba,si kuna mtu alikuchunga na kukulea katika mambo ya imani huyo ndiyo nilimanisha.Tukijua imani yake ilivyo tutajua kama ni sahihi au si sahihi kwa kutumia maandiko.
Taifa la Nigeria mambo ya dini yameleta shida sana,mpaka kuna kipindi watoto wadogo walikuwa wanatuhumiwa uchawi,kwa hiyo matangazo ya wanaojiita watumishi wa Mungu yakabadilika wanakuambia "tunanguvu za kuwashinda wachawi,njoo kwetu".
Hata kama lengo lako ni chanzo cha vifo lakini kumbuka ni nani anaweza kumfanya mtu afe kwa sababu yoyote ile.Na niliposema polisi tusiwalaumu,naomba unielewe na najua wewe unajua ya kwamba "mambo yote huanza katika ulimwengu wa Roho na baadaye kutokea katika ulimwengu wa mwili" kwa hiyo hata hivyo vifo vilianza katika ulimwengu wa Roho,polisi yeye mambo ya Rohoni hawezi kuyazuia ndiyo maana huwezi peleka polisi kezi ya kulogwa.Wewe unachofanya unaongea kama mtu unayeijua kweli na pengine unaweka kweli pembeni na kuongea katika utaratibu wa kawaida wa maisha.Ombi langu kwako unganisha knowledge yako kwenye spiritual issue na physical kisha toa maoni yako ili watu wapone.Hapa tunataka watu wapone,unajua kuna watu hata Mungu akiongea hawaelewi?Kuna Mchungaji alikutwa amelewa chakali video zikasambaa lakini bado wafuasi hawaelewi hata Mungu anapofunua yaliyo sirini.Kuna muda wa kuwaombea watu na kuna muda wa kuwaonya na kuwaambia yawapayo kutenda.
kanisa la Mungu limeingiliwa pale tunapoweza kusema hatutakiwi kukaa kimya,Kunaandiko agano la kale sikumbuki mstari lakini linaeleza kitu kama "je mambo haya yalikuwepo enzi za babu zenu?"Mambo ya mafuta ya upako je yalikuwepo miaka ya 80,90?Hapa watumishi hujitetea kwa kusema wamefunuliwa na Roho Mtakatifu na tena watakuletea na mistari kussuport,kuna mtu amesema sikumbuki kama ni wewe ya kwamba Yesu aliponya mtu kwa mate.Ni kweli lakini Yesu alikuwa na njia nyingi,na alipoondoka alituambia tuombe lolote kwa jina lake.Unataka watu wafunguliwe,omba kwa jina la Yesu,unataka mtu apone omba kwa Jina la Yesu,sasa siku hizi hizi technologia wanatudanganya wameombea mafuta kisha mafuta yatatuponya.Hapo watu wanaondolewa taratibu katika kumtegemea Mungu wanaenda kwenye vitu.Hii ni sawa na mkristo anayecheza kamali taratibu anaanza kutegemea nguvu ya buku badala ya Mungu.Sikatai ya kwamba kuna mafunuo lakini mafunuo ni kitu cha kutumiwa sehemu fulani kwa kadri ambavyo Roho wa Mungu ameona lakini haimanishi ni fundisho.Namanisha kama wewe Mungu ulipokuwa unamwombea mtu fulani,Mungu akakufunulia ombea maji kisha mpe anywe na yule mtu baada ya kunywa akapona.Hii haimanishi kila mgonjwa uombee maji umpe anye.Tunahitaji kuongozwa na Roho Mtakatifu.kama kuna mtu alifunuliwa mafuta basi haikutakiwa kuwa katikakila jambo.Yesu mwenyewe kuna wengine hata hakuwaombea,aliwaambia tu "imani yako imekuponya".Kwa hiyo njia za kupokea uponyaji au muujiza ni nyingi lakini njio yoyote ikitumika inatakiwa isiwe kinyume na neno la Mungu na kama njia hiyo inatoka kwa Mungu aliye wa kweli italeta amani kwa watumishi wengine ila kama haitoki kwa Mungu wa kweli friction itakuwepo.Na kwa nini wanaotuhumiwa hawaziachi hizo njia na kutumia jina la Yesu?Jina laYesu ili litende kazi kuna jinsi ambavyo anayelitumia anatakiwa kuwa si kila mtu,ndiyo maana wale watoto waliwaiga wanafunzi wa Yesu wakayaamulu mapepo yatoke,yakwaambia Yesu tunamju na Paulo tunamju,yakawapiga.Mungu anaweza kumtumia mtu yeyote ambaye atakuwa tayari kutii na kufuata maagizo ya Mungu.
Ni kweli doctrine zinaweza kutofautia lakini kuna yale mafundisho ya msingi,biblia ndiyo msingi wetu.Roho Mtakatifu ni mzuri hutufundisha.Yesu aliwaambia wanafunziwake watakuwa mashahidia kuanzia uyahudi,samaria mpaka mwisho wa nchi,injili ya mfuta ya upako,chumvi ya upako etc haikubaliki kwenye maeneo mengi ya dunia hii inaifanya isiye injili ya kweli kwani kuna maeneo haipokelewi siyo na wapagani,haipokelewi na watumishi wa Mungu,kwa sababu ina ukakasi ndani yake.Mwenye masikio na asikie.
Hawa jamaa ambao ni mbwa mwitu ndani ya ngozi ya kondoo wana network kubwa,na kwa sababu wanawatu wengi tunakoelekea na kwa kuwa ni unabii unatimia watawapata wengi yamkini hata wateule kama ambavyo maandiko yanasema.
Watumishi wa siku hizi wengi waovijana wanapenda publicity,wanapenda kutabiri hata kwenye mambo ambayo yanaonekana wazi.
Mo alivyopotea,kuna watumishi wanakuambia "mimi pekee ndiyo niltabiri kuwa atapatikana siku ya Ijumaa " wakati huo kuna wenzake naye anasema mimi pekee(hapa unajua hapo kuna shida,Roho hapingani).Sasa hapo hata kwa akili ya kibinadamu unaona kuna shida.
Tusome bibilia zetu,tumwombe Roho Mtakatifu atufundishe na tuache unafiki wa kuingia makanisani na wakati huo huo tunaiba,tunasema uongo,tuko fiesta na kwenye singeli hapo utakuwa unapoteza muda wako.Mungu wetu ni Mungu mwenye wivu atamhukumu kila mtu sawasawa na matendo yake.
Mnaojiita watumishi wa Mungu mnatakiwa mjue watu wanasema wewe ni nani na usipuuze majibu yao.Kama wakikuita wewe ni mwizi,tapeli etc basi angalia umekosa wapi,fanya toba na umwombe Mungu akusaidie,tukumbuke hao watu pia wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
Unahitaji kumpokea Yesu leo?Njoo inbox