Mtu mzima asiyekunywa pombe anaonekanaje? Kuna tatizo gani?

Magnificient

JF-Expert Member
Aug 8, 2013
1,162
701
Huwa napata changamoto nikijichanganya na marafiki zangu kupata vinywaji pamoja.
Mimi ni mtu mzima, ila sinywi pombe wala kutumia kilevi chochote. Wananishangaa sana na kujiuliza kwa nini situmii pombe na wananiona kama mtu wa ajabu sana. Tatizo liko wapi kama mtu mzima hanywi pombe?

Kinywaji changu kikubwa ni mchanganyiko wa Grand Malt na Coca-Cola na huwa nakifurahia na kunywa sana. Tusiokunywa pombe tunaonekanaje? Kuna ajabu gani kwa mtu mzima kutokunywa pombe? Anakosa nini? Kuna tatizo gani kwa mtu mzima kutokunywa pombe?
 
uko sawa tu,pombe haina dereva.ila wengi wao wanadhani ukiwa mnywaji ndo u-bab kubwa.pombe c kila k2.na hakuna athari.
 
Ata mimi sinywi pombe ata hiyo grandmalta sinywi watu wananishangaa nawezaje hii hali.
 
Wakat wengine wanasali kila cku tuacheje ww unajiuliza, pombe haina ishu mkuu,kwa vile unakuta ushazoea na company pia,kwanza pombe inapunguza thinking capacity, na kama uwezo wako wa kufikir ukipungua sana kutoka itakuwa ngumu sana hasa hiki kipindi cha mh. Magu ambacho ni no easy money!
 
Mimi siwaoni vibaya......japo siwaelewi.......lakini wanaokunywa grand malta na Coke......naona kama wanakunywa molases sijui kwa nini........na molases Yaeda tunaundia piwa.......
 
Mkuu wanaobeza wengi wanatamani wawe kama wewe kuacha kunywa hawawezi
 
Mimi siwaoni vibaya......japo siwaelewi.......lakini wanaokunywa grand malta na Coke......naona kama wanakunywa molases sijui kwa nini........na molases Yaeda tunaundia piwa.......

Wasiokunywa pombe wengi wao ni watu wajungu....na huwa ndoa zao zina migogoro sana.
........ni watu complicator sana sababu ya misongo ya mawazo ya kila mara.
 
Watu wasio kunywa pombe ni wambeya sana.

Yeah...ni wa ajabu sana...hata wengi wanaoleta hapa jamvin kuwa wanasumbuliwa na wake zao hawanywi pombe....
Drink responsibly....
 
Huwa napata changamoto nikijichanganya na marafiki zangu kupata vinywaji pamoja.
Mimi ni mtu mzima, ila sinywi pombe wala kutumia kilevi chochote. Wananishangaa sana na kujiuliza kwa nini situmii pombe, na wananiona kama mtu wa ajabu sana. Tatizo liko wapi kama mtu mzima hanywi pombe?
Kinywaji changu kikubwa ni mchanganyiko wa Grand Malt na Coca-Cola na huwa nakifurahia na kunywa sana. Tusiokunywa pombe tunaonekanaje? Kuna ajabu gani kwa mtu mzima kutokunywa pombe? Anakosa nini? Kuna tatizo gani kwa mtu mzima kutokunywa pombe?
Pombe ni kama hivi
 

Attachments

  • IMG-20151227-WA0005.jpg
    IMG-20151227-WA0005.jpg
    144.6 KB · Views: 844
Mimi siwaoni vibaya......japo siwaelewi.......lakini wanaokunywa grand malta na Coke......naona kama wanakunywa molases sijui kwa nini........na molases Yaeda tunaundia piwa.......

Hahaaa piwa=gongo????
 
Sasa na wewe utuuzima wote huo kwanini hunywi pombe. Kunywa pombe bana, hata kwenye mambo yetu yale unakuwa uko fiti kweli. Duniani kote watu wenye akili lazima wapige monde. Hata kwa wale wanaoamini Ukatoliki Papa wao anagonga monde na wao wala hawakatazwi.
 
Huwa napata changamoto nikijichanganya na marafiki zangu kupata vinywaji pamoja.
Mimi ni mtu mzima, ila sinywi pombe wala kutumia kilevi chochote. Wananishangaa sana na kujiuliza kwa nini situmii pombe, na wananiona kama mtu wa ajabu sana. Tatizo liko wapi kama mtu mzima hanywi pombe?
Kinywaji changu kikubwa ni mchanganyiko wa Grand Malt na Coca-Cola na huwa nakifurahia na kunywa sana. Tusiokunywa pombe tunaonekanaje? Kuna ajabu gani kwa mtu mzima kutokunywa pombe? Anakosa nini? Kuna tatizo gani kwa mtu mzima kutokunywa pombe?

Wewe mlevi kabisa.... Ni mlevi wa Grandmalt na Coca. Nakusihi uache kbs maana ni hatar kwa afya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom