Mtu mweusi: Kiumbe mwenye historia tata

Mtu mweusi: Kiumbe mwenye historia tata

History ya mtu mweusi ipo sema tu kuna baadhi ya watu wameficha, waliwezaje kugundua kuwa wayahudi WA mwanzo walikuwa weusi. Documents zikivumbuliwa kituo cha Kwa Vatican zikienda Vatican hazirudi hakuna cha mrejesho. Kuna documents nyingi za kale zimegundulika zimefungiwa huko Vatican. Kwa mazingira haya uwezi kupata ukweli wowote ule.
Huko Vatican zinapelekwa kwa sababu gani?
 
Mimi ni kurya kutoka Rorya, je naweza kuwa mchagga kwa kujua kuzungumza kichagga!? Naomba ufafanuzi hapo mamaangu!! Unaposema uarabu ni lugha sielewi!;

Hapana, huwezi kuwa Mchagga kwa kuzungumza Kichagga.

Uarabu ni lugha na Waarabu lugha mama kwao ni Kiarabu.

Neno Arabia linatokana na lina asili ya neno Arabbiya au caravan, msafara.

Watu hubabaika kwa kusikia nchi inaitwa Saudi Arabia, kumbuka tu kuwa jina Saudi Arabia lilianzishwa juzi juzi tu, mwaka 1932. Saud ni jina la ukoo wa Ibn Saud.
 
Yote yatafahamika baada ya vita ya tatu ya dunia baina ya wazungu na waislamu, mengi yatafichuka
 
NADHARIA YA KWANZA
:-MTU MWEUSI NDIYE MJENZI MKUBWA WA USTAARABU HAPA DUNIANI

A: ASILI YA MAJINA YA JAMII ZA WATU NDANI YA NADHARIA.

Kuna maneno ambayo yatatumika hivyo ili kuweka mambo sawa na kutowachanganya wasomaji ngoja nielezee chimbuko lake katika historia. Jambo muhimu kabisa kukumbuka ni kwamba majina mengi ya sehemu, taifa au jamii ya watu fulani mara nyingi hutokana na asili ya eneo lile (kama tabia ya nchi), jina la baba wa jamii ile au mtu aliyekaa katika lile eneo husika. Mfano, taifa la Israeli limetokana na Yakobo ( 2006-1859 K.K) ambaye anaaminika kuwa ndiye Baba wa jamii ya Waebrania: au neno Ethiopia, wanahistoria kama Herodotus wa Ugiriki(484-425 K.K) na Flavius Josephus wa Rumi ( 37-100 B.K) walilitumia kutoka kwenye lugha ya kigiriki "Ethiopos" ambalo linamaanisha mtu ambaye ngozi yake imeungua na jua. Hivyo Basi nchi ya Ethiopia ambayo zamani iliitwa Abyssinia imelichukua neno ambalo linaelezea sifa ya watu wanaokaa nchi hiyo: Au Bara la Ulaya ambalo ni Europe limetokana na jina ambalo linaelezea sifa ya eneo ambalo linahusishwa na mwanamke Europa ambaye kwa lugha ya Kigiriki jina lake lina neno "Eurus" na "ops/op-lopt". Ambapo "Eurus" linamaanisha Pana na "ops/op-lopt" linamaanisha sura au uso. Hivyo Ulaya maana yake uso mpana kwasababu Wagiriki pamoja na watu wa zamani waliamini ni eneo kubwa sana.

Neno Afrika limegubikwa na utata mwingi kama ambavyo historia ya watu wake ilivyogubikwa na utata. Mpaka sasa watu tofauti wamejaribu kuelezea chanzo cheke kila mtu akivutia kwake. Baadhi ya wasomi wameelezea neno Afrika lilitokea baada ya Jemedari wa jeshi la Rumi aitwae Scipio Africanus ambaye alishinda vita dhidi ya Ufalme wa Karthago (Carthage) mnamo mwaka 146 K.K. Ambapo dola la Karthago lilikuwepo sehemu ambapo ipo Tunisia leo, hivyo basi Afrika likapewa jina hilo la huyo jemedari. Wengine wakasema neno la Afrika asili yake ni Kigiriki ambapo neno "Aphrike" linalomaanisha Baridi ndiyo asili yake. Wengine wakasema neno la kilatini "Aprica" linalomaanisha hali ya jua kali ndiyo asili yake. Mwanahistoria wa Kigiriki Leo Africanus alisema Afrika asili yake ni neno "Aphrike" linalomaanisha sehemu yenge baridi kali na ya kutisha. Lakini wasomi wengi wanadai kwamba neno Afrika asili yake ni lugha mbili za Kifonike (Phoenecian) na kilatini. Katika lugha ya Kifonike ambayo ilikuwa ni ya watu walioijenga Karthago neno "Afri" kwao ilikuwa ni Vumbi na neno "Ica" limetoholewa kwenye lugha ya Kilatini kumaanisha Ardhi,nchi. Hivyo basi neno Afrika linamaanisha "Nchi/Ardhi yenye vumbi.

Neno Uarabuni nalo lina asili pana katika muktadha wake. Kwanza kabisa wanahistoria manguli wanalihusisha na maneno ya majigambo ya dola la Kiashuru (Assyria) yaliyoandikwa mwaka 853 K.K. Hili lilitokana na kitendo cha mfalme Shalmanasi kumpiga kivita moja ya machifu wake walioasi. Jina la huyo chifu ni Gindibu Mwarabi. Wanahistoria wengi walitumia kuwaelezea watu wa Shamu ambao walikaa katika ghuba ya Uarabu. Lakini wanahistoria kwa upande mwingine wanahusisha neno "Arabu" na lugha za watu wa mashariki ya kati hasahasa Waebrania. Ambapo ziliezea sifa za neno na watu wenyewe. Neno la Kihebrania "Arav" linamaanisha jangwa, ambapo zaidi zaidi kuna lugha zinawealezea zaidi kama watu wanaohamahama au wafanyabiashara. Ukisoma kwenye Biblia kitabu cha pili cha Mambo ya Nyakati 17: 11 kwenye lugha ya Kihebrania utaona kwa mara ya kwanza linatumika kuwaelezea Waarabu kama jamii ya wafugaji. Lakini kwasababu sehemu kubwa ya Elimu ya dunia ya leo imepata ushawishi kutoka kwa nchi za Kigiriki basi Wanafalsafa na Wanahistoria wa Kigiriki walitumia neno Uarabuni kuelezea sehemu yote ya Rasi ya Uarabuni pamoja na nchi kama Misri.

Neno Ethiopia Wagiriki wamelitoa kwenye neno lao "Ethiopos" ambalo "Aitho" linamaanisha naungua na neno "ops" linaamnisha Uso. Hivyo Ethiopia ni mtu aliyeungua uso kwa maana nyingine ni mtu mweusi, na katika historia ya kale watu walioandika sana kama Herodotus, Appolodorus, Marcellinus na Josephus wanasema kuwa watu weusi walikaa mashariki ya kati, Misri, Sudan, Ethiopia, Visiwa vya bahari ya meditteranea na Afrika Kaskazini. Haya yote yalizungumzwa na wanahistoria katika kikao cha UNESCO ambapo tamati haikufikiwa. Japo kwenye Biblia kitabu cha Yeremia 13:23 Mungu aliuliza kwamba Je, Mkushi/Ethiopia anaweza kubadili rangi yake ya mwili? Hili linathibitisha kwamba katika historia kulikuwa na watu weusi na walikuwa wana mchango mkubwa sana kwenye dunia. Herodotus katika maandishi yake aliwaelezea wanaume weusi "Ethiopians" kama watu warefu, wazuri wa sura na wenye nywele ngumu. Lakini leo kuna nchi ya Ethiopia ambayo watu wake wamijiita hivyo kutokana na mandhari ya kihistoria.

Neno Misri katika historia linaonyesha kutumika kimakosa. Kwanza Katika dunia ya kale Wamisri waliita nchi yao "Kemet" ambalo lilimaanisha ardhi nyeusi ya mto naili na pia eneo la watu weusi. Mwanahistoria Flavius Josephus ndiye aliyeelezea Historia ya Malkia wa Sheba ambaye alienda kumtembelea mfalme Suleimani. Huyu malkia wengi wanamuita Mekeda lakini pia katika lugha ya Amhara kuna kumbukumbu inayotoa jina lake jingine kama Birkis. Daktari wa Historia Windsor Rudolf anasema wafalme wengi japo siyo wote walikuwa na majina zaidi ya moja. Mfano Suleimani alipewa jina Yededia alipozaliwa lakini alipokuwa mkubwa aliapishwa kama Suleimani, au Mtoto wa mfalme Suleimani Menelik wa Kwanza alivyoenda kuapishwa Yerusalem alipewa jina Daudi kama babu yake. Hivyo isichanganye mtu kama Josephus alitumia Mekeda na Wengine wakamuita Birkis.

Tukirudi kwenye neno Misri, Wagiriki walilichanganya na jina la mji mkuu wa Kibiashara Misri kipindi hicho ulioitwa "Thebes" ambapo jina lake la pili uliitwa "Aigyptos" hivyo wafanyabiashara wengi waliuita Aigyptos na hivyo jina likakaa hadi kuitwa Egypt. Mfano wa haya mambo hata leo hii upo, katika historia ya Tanganyika hatujawahi kuwa na kabila la Wahehe lakini kutokana na Wajerumani kukosea kabila la Wahehe likazaliwa mpaka leo hii lipo. Au Sehemu kama Tosa-Maganga mkoani Iringi kumtokana na makosa ya wageni kuandika kile walichokisikia wenyeji wakisema. Hivyo Dola la Kale la Misri liliitwa KEMET (Nchi ya Nile Nyeusi au nchi ya watu weusi)

MUHIMU: Tujifunza kitu muhimu, kwamba katika historia siyo kila mtu ambaye alikuwa ni Mwarabu alikuwa ni mwarabu mweupe wa leo hii, na pia siyo kila Mwafrika alikaa hapa Afrika, tukifika huko mbele tutona jinsi ambavyo kulikuwa na muingiliano mkubwa katika hivi vizazi. Mfano mzuri ni kwamba Misri ya leo hii siyo Misri ya zamani kwasababu imetawaliwa na watu wengi tofauti kwa vizazi vingi. Daktari Ivan Van Sertima anasema kwamba kama ilivyo leo Marekani ambayo ilikuwa nchi ya Wahindi wekundu ndivyo ilivyo leo Misri. Kwamba Wenyeji ambao ni Wahind wekundu ni wachache kuliko wahamiaji kutoka barani Ulaya. Hivyo naomba tuvumiliane maana mwishowe nitaweka kila kitabu nilichokisoma na kukifanyia kazi ili wale wanaopenda kusoma wapitie wenyewe na wachambue kipi ni kweli na kipi siyo ukweli.

TUTAENDELEA HIVI PUNDE.................................................

B: MWANZAO WA VIZAZI VYA BINADAMU KUTOKA KWA NUHU.

CC: KENZY , Hoshea , R Mbuna , binjo , Luggy
 
Bado unarudia "mweusi", nimesema; Uarabu si rangi ya mtu, uarabu ni lugha.

Sasa sijuwi ni nani alikujaza ujinga kuhusu Waarabu kuwa si weusi pia.
Mkuu inawezekanaje mtu mzima na msomi kama wewe unajazwa ujinga namna hii na unashindwa kujitambua.
Yaani unaamini hata Wewe ni mwarabu?
Hivi kuzungumza lugha flani una kuwa kabila hilo?
 
Mkuu vipi kuhusu hawa Moors ambao walitoka North Africa na kuvamia ulaya Spain,Portigal etc na kutawala huko muda mrefu. Hebu weka hizi taarifa sawa kidogo. Wazungu wasije wakawa wanatupiga fix maana inaonekana Mtu mweusi zamani alikkuwa kichwa sana
 
Mkuu vipi kuhusu hawa Moors ambao walitoka North Africa na kuvamia ulaya Spain,Portigal etc na kutawala huko muda mrefu. Hebu weka hizi taarifa sawa kidogo. Wazungu wasije wakawa wanatupiga fix maana inaonekana Mtu mweusi zamani alikkuwa kichwa sana

Kufuatana na maandiko ya Walter Rodney , wale waliovamia maeneo ya spain na portugal ni waarabu ambao kwa sasa ndio wapo maeneo ya Tunisia, Morocco na Algeria.
I stand to be corrected.
 
Kufuatana na maandiko ya Walter Rodney , wale waliovamia maeneo ya spain na portugal ni waarabu ambao kwa sasa ndio wapo maeneo ya Tunisia, Morocco na Algeria.
I stand to be corrected.
Wenda ukawa sahihi kwa asilimia kadhaa.
1: Hawa jamaa walitokea Africa kaskazini na kaskazini-Magharibi
2Pili hawa jamaa walikuwa ni waislamu maana ilikuwa ni kipindi cha Islamic calphate (Nadhani chini ya Caliph Umar)
3:Hwa jamaa walikuwa mchanganyiko wa Waarabu, Watu weusi wa kutoka kaskazini magharibi mwa afrika, ma machotara wa kiarabu na watu weusi. Na kabila la berbers ambao hawa jamaa wanasemekana pia wanauhusiano na watu weusi.
4:Wenda wazungu wanaficha ili isionekane wameshawahi kutawaliwa na Waafrika kwa muda mrefu kuliko wao kututawala sisi.

Labda kuna watu wanamaarifa zaidi wataweka sawa hizi records.
Asante mkuu
 
Wenda ukawa sahihi kwa asilimia kadhaa.
1: Hawa jamaa walitokea Africa kaskazini na kaskazini-Magharibi
2Pili hawa jamaa walikuwa ni waislamu maana ilikuwa ni kipindi cha Islamic calphate (Nadhani chini ya Caliph Umar)
3:Hwa jamaa walikuwa mchanganyiko wa Waarabu, Watu weusi wa kutoka kaskazini magharibi mwa afrika, ma machotara wa kiarabu na watu weusi. Na kabila la berbers ambao hawa jamaa wanasemekana pia wanauhusiano na watu weusi.
4:Wenda wazungu wanaficha ili isionekane wameshawahi kutawaliwa na Waafrika kwa muda mrefu kuliko wao kututawala sisi.

Labda kuna watu wanamaarifa zaidi wataweka sawa hizi records.
Asante mkuu

Katika kitabu cha How Europe underdeveloped Africa, hayo matukio yanaelezwa kwamba yalitokea kipindi ambacho African level of development was almost the same with that of Europe.
 
Katika kitabu cha How Europe underdeveloped Africa, hayo matukio yanaelezwa kwamba yalitokea kipindi ambacho African level of development was almost the same with that of Europe.
kweli mkuu naamini kuna kipindi tuliwazidi kabisa.
Shida yetu ni upendo kipindi ambacho tunawazidi ujanja tungwahujumu kama wao walivyotuhujumu tungekuwa mbali.
ila haya mambo ya historia ya Mtu mweusi wameyasabotage sana
 
Mkuu inawezekanaje mtu mzima na msomi kama wewe unajazwa ujinga namna hii na unashindwa kujitambua.
Yaani unaamini hata Wewe ni mwarabu?
Hivi kuzungumza lugha flani una kuwa kabila hilo?
Huyo kachanganya mambo ya dini na waarabu ndio walivyowaambia kuwa ukiongea tu then wewe Ni mwarabu
 
Huyo kachanganya mambo ya dini na waarabu ndio walivyowaambia kuwa ukiongea tu then wewe Ni mwarabu
hahahahaa maadam bhana..., huwa anarahisisha mambo sana. Kiila kitu lazima kilazimishwe kuhusishwa na Islam.
 
Mkuu vipi kuhusu hawa Moors ambao walitoka North Africa na kuvamia ulaya Spain,Portigal etc na kutawala huko muda mrefu. Hebu weka hizi taarifa sawa kidogo. Wazungu wasije wakawa wanatupiga fix maana inaonekana Mtu mweusi zamani alikkuwa kichwa sana

Mkuu naomba nisiwe msemaji sana katika hili, lakini naomba twende kwa vithibiti kutoka vyanzo mbali mbali ambavyo wasomi wakubwa wa historia ya mtu mweusi wameandika:

HAPA NI BAADA YA KUZALIWA KRISTO NA KUANGUKA KWA DOLA YA RUMI:

"The reins of their (Moors) horses were as fire, their faces black as pitch, their eyes shone like burning candles, their horses were swift as leopards and the riders fiercer than a wolf in a sheepfold at night . . . The noble Goths [the German rulers of Spain to whom Roderick belonged] were broken in an hour, quicker than tongue can tell. Oh luckless Spain" - Dr Ivan Van Sertima, in The Golden Age of the Moors.

HAPA NI KABLA YA KUZALIWA KRISTO, VITA KUBWA KATI YA WEUSI NA DOLA YA RUMI:

"When this was done in an ancient-history classroom at the University of Pennsylvania, Prof. William C. McDermott responded: "Yes, Hannibal was as black as King David." - The New York Times published in 1991.

Links:
1. Hannibal of Carthage Was No More Black Than King David
 
Mkuu inawezekanaje mtu mzima na msomi kama wewe unajazwa ujinga namna hii na unashindwa kujitambua.
Yaani unaamini hata Wewe ni mwarabu?
Hivi kuzungumza lugha flani una kuwa kabila hilo?
Duuuh hata mimi nina ukakasi hapo...yaani hata mimi nikifahamu kiarabu naweza kuwa Muarabu duuuh.... FaizaFoxy ikoje hapo kaka..??
 
Back
Top Bottom