Kwa jinsi walivyo kuja naona ni msamehe tu. Hakuna binadamu aliyekamilika.
Labda lakini mimi niko karibu kupata jiko. Sijui yeye vp? Nauaga aga ukapera nibaki njia kuu.
sioni dalili ya wewe kupata jiko wala sufuria make tangu umeanza story ungeshakuwa na mke labda na mtoto kaanza kutambaa lakini wapi!!!!
Haya ni maamuzi ya mwisho. Nimejistukia maana hata mambo hayasongi. Nitakuarika kwenye sherehe ya kufunga pingu za maisha.
Sio stori ni hali halisi dada. Mimi kaka yako nataka nikuletee wifi yako.
bora tangawizi, hii imewekwa pilipili manga
Tushajua umeombwa msamaha na umefatw kwenu na.baba mkwe cc Mafikizolo
Nilokuwa nimesafiri kwenda kijijini kwetu. Mtandao ulikuwa haupatikani. Leo nimeingia kwenye jiji la mihangaiko.
Nadhani mtakumbuka mashariti ya wazazi wa mtoto wa kitusi yalivyo nishinda na kuamua kumwaga manyanga.
Wiki iliyopita alikuja nyumbani kwetu kijijini akiwa na baba yake. Aisee mtoto kapungua kabisa.
Aliponiona alimwaga machozi na kunikimbilia.
Kwaufupi wameomba msamaha na kusema hayo yote waliyoyasema hayatakaa yatokee.
Sikuwajibu chochote na tunategemea mwezi ujao tukakutane kwenye kikao na wazazi wangu.
Wana JF nifanye nini sasa hapa?
Mzee wa ki-tutsi akuombe msamaha wewe? You can't be serious.
kwani vipi mkuu? watutsi hawaombagi msamaha? au hawaombagi msamaha kwa non-tutsis?