Mtoto wa Diamond na kitu cheusi mkononi..

Mtoto wa Diamond na kitu cheusi mkononi..

Watu wakigoma wanaimani hizo sana nliwahi safiri kwa gari hadi kigoma watoto wote kwenye hilo gari walikuwa wamefungwa kiuzi cheusi mkononi na kiunoni hadi leo sikuwahi kujua ina maana gani

Sio kigoma tu niutamaduni karibia mikoa mingi tu watoto hufungwa hivyo viuzi mkononi na kiunoni
 
vitu vya asili. ni mchanganyiko wa kinyesi cha TEMBO na mbegu za BANGI! Na kipande cha nguo nyeusi A.K.A Kaniki"
 
Basi walokole kazi mnayo huyo mtoto wameshawekeza mizimu na majini ndani yake.
 
Fanya uwe na mtoto utajua watu wengine bana kwa hiyo muafrica amekuwa mzungu hata ww ulivalishwa mpaka ya kiunoni
 
Eti hakuna asiye zindikwa duniani hivi wewe kwa akili yako unafikiri watu wote wanaamini ktk mambo kama hayo mf.mimi nina watoto wangu hakuna aliye wahi kwenda hata kwa mganga wa kienyeji na sitegemei kwenye familia yangu kamanitafika kwa mganga wa kienyeji

Zamu yako ikifika ndipo utajua watu huwa wanakwenda kwa mganga kwa hiyari au lazima kama hayajakupata usiombe yakakupata hakuna mtu hata mmoja duniani anayependa pesa zake zitoke hata kidogo mshukuru Mungu kwa ulivozaliwa.
 
Kuna tatizo gani? Kwani ni lazima itikadi zifanane? Mwacheni buana hakuna cha ajabu hapo. Kama unaamini hayo mambo unaweza ukamvalisha mwanao, na kama Huna iman na hayo mambo achana nayo hautaulizwa. Lakini yakiwafika ndio mtajua.
 
Nimewahi kuona watoto wengi wakiwa wamevalishwa hivyo vitu sidhani kama waliowavalisha ni wajinga au waliwavalisha kwa bahati mbaya kila kitu kina maana yake
 
Hizi ni mila tu watoto wengi wa kiafrika halisi tunapitia ila nyiye mnaokwenda kuogelea baharini na baba na mama zenu na vichupi mtashangaa
 
Wanaharakati wa HAKI ZA MTOTO mukuje huku kunawapasa. Jiulize, Je mtoto huyu mzuri namna hii angeulizwa kama anataka kuvikwa hilo litambaa bovu la kaniki angekubali?
Wateteeni wasio na wa kuwasemea
 
Ni imani za kishirikina tu hakuna namna nyingine yakueleza....
 
Watu wana imani za ajabu ajabu sana. Kwa hiyo kinachomlinda huyo mtoto ni hicho kihirizi au hicho ndio mungu?

Imani zingine aisee ni za kijinga.
 
Hiyo ni dawa ili asishtuke shtuke au kulia lia.
Niliambiwa inawekwa bangi,kitunguu swaumu na mavi ya tembo na mvuje (siujui)

Kinachofanya asishtuke ni mchanganyiko wa vilivyoweka akilala mkono unakua karibu na pua anakua anavuta harufu inamlewesha analala vizuri sana.
Huwa na nguvu zaidi siku za mwanzo baadae dawa inaisha nguvu kinabadilishwa.

Sina ushahidi ni simulizi tu niliipata vijijini huko Muheza.
 
Back
Top Bottom