Nina jamaa zangu wawili ambao wako kwenye ndoa, mmoja ni zaidi ya miaka tisa,lakini hawajafanikiwa kupata mtoto.Japo hawasemi lakini kwa kuwatazama na jinsi watu wanavyonong'ona penbeni inaonyesha kabisa hawako happy kwenye ndoa zao.Je ni kweli kwamba mkipata mtoto huifanya ndoa yenu iwe imara zaidi?Mi binafsi nachukulia kama mipango ya Mungu tu, labda watafanikiwa mbele ya safari.