Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 8,848
- 15,253
Ni Binti wa umri wa miaka 11 ambae yupo darasa la tano.
Binti huyu pamoja na umri wake mdogo lakini ameeathirika sana kisaikolojia kutokana na kutumika kingono kutoka kwa vijana wenye umri mkubwa.
Binti huyu mamake aliachana na Baba yake na kwenda kuolewa sehemu nyingine na kumuacha binti akiwa na Baba yake, kutokana na tabia ya baba yake ya ulevi na kutojitambua na kushindwa kumlinda mtoto wake huyo vijana walevi wa mtaani wakaanza kutumia mtoto huyo kingono tangu akiwa na umri wa miaka 9.
Mama mmoja jirani ambae pia ni mjane aliamua kumchukua mtoto huyo na kuishi nae japo kwa tabu kutokana na kwamba huyo mama ni mlevi na hana kipato maalumu zaidi ya vibarua vya hapa na pale.
Kilichonisikitisha ni baada ya kumuona binti huyo mdogo na pia mwenye umbo dogo kabisa ambae vijana wanamrubuni kwa kumpa kiasi cha shilingi 100, na sh 200 baada ya tendo.
Ilibidi niulizie kwanini mtoto huyo mdogo afanyiwe vitendo hivyo kila wakati tena kwa kujirudia? Ndipo nikaelezwa kuwa mtoto huyo hayupo sawa sawa kichwani.
Kuhusiana na swala la polisi kesi zilishapelekwa huko na inajulikana
Mwisho wa huyu mtoto utakuwaje?
Nimeshindwa kuweka picha ya mtoto ili kulinda maadili. Na utu wa mtoto
Binti huyu pamoja na umri wake mdogo lakini ameeathirika sana kisaikolojia kutokana na kutumika kingono kutoka kwa vijana wenye umri mkubwa.
Binti huyu mamake aliachana na Baba yake na kwenda kuolewa sehemu nyingine na kumuacha binti akiwa na Baba yake, kutokana na tabia ya baba yake ya ulevi na kutojitambua na kushindwa kumlinda mtoto wake huyo vijana walevi wa mtaani wakaanza kutumia mtoto huyo kingono tangu akiwa na umri wa miaka 9.
Mama mmoja jirani ambae pia ni mjane aliamua kumchukua mtoto huyo na kuishi nae japo kwa tabu kutokana na kwamba huyo mama ni mlevi na hana kipato maalumu zaidi ya vibarua vya hapa na pale.
Kilichonisikitisha ni baada ya kumuona binti huyo mdogo na pia mwenye umbo dogo kabisa ambae vijana wanamrubuni kwa kumpa kiasi cha shilingi 100, na sh 200 baada ya tendo.
Ilibidi niulizie kwanini mtoto huyo mdogo afanyiwe vitendo hivyo kila wakati tena kwa kujirudia? Ndipo nikaelezwa kuwa mtoto huyo hayupo sawa sawa kichwani.
Kuhusiana na swala la polisi kesi zilishapelekwa huko na inajulikana
Mwisho wa huyu mtoto utakuwaje?
Nimeshindwa kuweka picha ya mtoto ili kulinda maadili. Na utu wa mtoto