Mtoto alipoharibu

Mtoto alipoharibu

Ukifuatilia vizuri huu uzi, utawajua wachepukaji dhahiri kabisaa kutokana na majibu yao..
 
mtoto hapo anashida kwa kweli.. wanaume wachepukaji tumieni kinga mnatesa watoto
dhaaa!! It's true kinga n muhimu sana ukiwa na,nyumba ndogo wanaume tujiongeze lacvyo watt wetu watateseka sana kukosa malez ya baba na ndo tunaowaona huko barabaran wakizagaa wengi kila kukicha

Ee mungu nisaidie watt wang wote wawe wa ndan ya ndoa waje wapate malez yote baba na mama
 
dhaaa!! It's true kinga n muhimu sana ukiwa na,nyumba ndogo wanaume tujiongeze lacvyo watt wetu watateseka sana kukosa malez ya baba na ndo tunaowaona huko barabaran wakizagaa wengi kila kukicha

Ee mungu nisaidie watt wang wote wawe wa ndan ya ndoa waje wapate malez yote baba na mama
ni jambo jema .. bora wawe mitaani hatuna mkataba na Mungu utaishi miaka mingapi.? mchepuko na wewe unajipanua unatiiwa mimba upo kwenye nyumba ya kupanga ama kweli akili za kushikwa ni shida.. mi no kwa kweli acha nionekane anaendekeza pesa aisee
 
Ukizinduka tu unamkuta dogo ndio anakuamsha 'dady amka'

Issue ni kuwa iweje uzimie baada ya kukutana na mtoto ambaye amekukimbilia na kukuita dad wakati watoto wengine mmepishana nao hawajafanya hivyo.
 
Issue ni kuwa iweje uzimie baada ya kukutana na mtoto ambaye amekukimbilia na kukuita dad wakati watoto wengine mmepishana nao hawajafanya hivyo.
Yaani akizinduka atazimia tena.
 
".....We normally meet our destiny on the way we chose to avoid it...."
 
Habari za leo wapendwa,

Jamani leo shost mwingine amepata majanga, huyu niliwahi kufanya nae kazi sehemu flani lakini bado tunamawasiliano.

Kisa chenyewe ni kuwa, shost alipokuwa 30+ aligundulika na fibroids, kwakuwa hakuwa na mume wala mtoto, alikuwa desperate kupata angalau mtoto akihofia baada ya matatibabu anaweza akose kabisa.

Sijui makubaliano yalivyokuwa lakini alikutana na kijana Peter ambae ni engineer, Peter ana mke na mabinti wawili. Shost amebahatika kupata mtoto wa kiume, Peter amechanganyikiwa kwa furaha. Peter aliahidi kumtunza mama na mtoto, aliwapangishia nyumba nzima lakini mbali kabisa na nyumbani kwake, mfano iwe Gongo la Mboto na Mbweni.

Peter alihakikisha mara mbili kwa wiki alikuwa kwa shost akimuogesha mtoto, kumsomea bedtime stories mpaka mtoto akilala ndiyo anaondoka kwenda kwake. Mtoto alimfahamu baba yake na mara nyingi aliuliza kwanini baba hakai na sisi, si fahamu ni jibu gani wazazi walimpatia.

Mke wa Peter hakuwa na fahamu yeyote kwa haya yote yanayotekea. Kasheshe imekuja kipindi hiki cha sikukuu, shost alikwenda kumnunulia mtoto mahitaji ya sikukuu Mlimani City na kugongana uso kwa uso na Peter akiwa na mkewe na watoto wao.

Katoto ka shost masikini kamemkimbilia Peter daddy, jamani Peter aliishiwa nguvu, mke amekuja juu, inakuwaje mtoto apite watu wote aje akuite wewe daddy?
hapo kwa kweli kuna shida kidogo, ndoa za wake wengi mbona zinaruhusiwa Tz, angefuata nyayo za mz Mengi, anabeba jiko mbili mchezo unaishia hapo. hakuna mtu angekwazika.
Ila kwa mazingira hayo inabidi bw. Peter afunguke, aeleze ukweli ulivyo asubiri msamaha kama utapatikana.
 
Kwa kweli hata cjui huyo mume atamuangaliaje mkewe, jaman wanaume achen michepuko mnazidisha watoto wa mitaan
 
Ilishawahi kunitokeai mimi hiyo . Nlilipanda basi ha humo ndani kulikuwa na katoto kamoja kimepakatwa na mama yake... katoto kaliponiona tu kakaninyooshea mikono na kuniita... DADDY!!!

Sijawahi kumuona huyo mama watoto wala mwanae maishani mwangu. Abiria wote walitumbua macho wakawa wanasubiri vioja vianze... lakini yule mama mtoto alimkana mwanae. Rabda nilifanana tu na baba yake!
 
Ilishawahi kunitokeai mimi hiyo . Nlilipanda basi ha humo ndani kulikuwa na katoto kamoja kimepakatwa na mama yake... katoto kaliponiona tu kakaninyooshea mikono na kuniita... DADDY!!!

Sijawahi kumuona huyo mama watoto wala mwanae maishani mwangu. Abiria wote walitumbua macho wakawa wanasubiri vioja vianze... lakini yule mama mtoto alimkana mwanae. Rabda nilifanana tu na baba yake!
Laiti ungepatikana pale Mlimani City wakati ule, umweleweshe mke wa Peter kwa maneno haya, engineer angekulamba miguu.
 
Laiti ungepatikana pale Mlimani City wakati ule, umweleweshe mke wa Peter kwa maneno haya, engineer angekulamba miguu.

Huruma kwa katoto .... Engineer kachemsha. He made his bed, now he must lie in it! Akimkana hapo mbele ya wife to save his skin, atamwelezaje tena akimtembelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom