G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 12,418
- 39,523
Vigogo watano wa Chama Cha Mapinduzi wanatarajiwa kutoa msimamo wao juu ya ni nini watakifanya juu ya chama chao mwishoni mwa wiki ijayo.
Miongoni mwa vigogo hao yupo kigogo mmoja ambaye ataisambaratisha kabisa jumuiya moja maarufu ndani ya chama hicho.
Wadokezi wangu wameninyetisha kuwa kwa sasa ndani ya CCM kuna mpasuko mkubwa ambao haujawahi kukikumba chama hicho tangu kuanzishwa kwake ingawa mambo bado hayajaonekana hadharani.
Baadhi ya vigogo wanatarajiwa kutoa misimamo yao, wapo ambao wamekuwa ni watu wa karibu kabisa kwenye kampeni za mgombea urais wa Chama hicho John Magufuli katika siku za awali ingawa kwa sasa wamejiweka pembeni.
Wiki hiyo kutashuhudiwa kigogo mmoja wa kamati ya maadili ya chama hicho akitoka hadharani na kueleza waziwazi msimamo wake juu ya yaliyotokea ndani ya CCM na mwenendo wake kwa ujumla.
Habari nzito zinasema kuwa mgombea mwenza wa chama hicho bi Samia Suluhu amelalamikia kutengwa kabisa na wanawake wenzake huku wakibaki wawili ambao ni Angela Kairuki na Ummi Mwalimu wakijikongoja pamoja na wasanii mbalimbali.
Aidha hakuna kampeni za baadhi ya makundi kumsaidia mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho zaidi ya Abdulrahaman Kinana pekee huku vigogo wengine wengi wakijichimbia mafichoni jambo lililotafsiriwa kama hujuma dhidi ya mgombea huyo.
Miongoni mwa vigogo hao yupo kigogo mmoja ambaye ataisambaratisha kabisa jumuiya moja maarufu ndani ya chama hicho.
Wadokezi wangu wameninyetisha kuwa kwa sasa ndani ya CCM kuna mpasuko mkubwa ambao haujawahi kukikumba chama hicho tangu kuanzishwa kwake ingawa mambo bado hayajaonekana hadharani.
Baadhi ya vigogo wanatarajiwa kutoa misimamo yao, wapo ambao wamekuwa ni watu wa karibu kabisa kwenye kampeni za mgombea urais wa Chama hicho John Magufuli katika siku za awali ingawa kwa sasa wamejiweka pembeni.
Wiki hiyo kutashuhudiwa kigogo mmoja wa kamati ya maadili ya chama hicho akitoka hadharani na kueleza waziwazi msimamo wake juu ya yaliyotokea ndani ya CCM na mwenendo wake kwa ujumla.
Habari nzito zinasema kuwa mgombea mwenza wa chama hicho bi Samia Suluhu amelalamikia kutengwa kabisa na wanawake wenzake huku wakibaki wawili ambao ni Angela Kairuki na Ummi Mwalimu wakijikongoja pamoja na wasanii mbalimbali.
Aidha hakuna kampeni za baadhi ya makundi kumsaidia mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho zaidi ya Abdulrahaman Kinana pekee huku vigogo wengine wengi wakijichimbia mafichoni jambo lililotafsiriwa kama hujuma dhidi ya mgombea huyo.