'MTIHANI MKUBWA' anasimulia mwanasiasa Julias Mtatiro

Sexer

JF-Expert Member
Oct 22, 2014
8,216
7,908
MTIHANI MKUBWA....

Bibi yetu mpenzi (pichani katikati), amezaliwa kabla ya vita ya kwanza ya Dunia. Jana Alhamisi saa 10 jioni
alimzika kijana wake muhimu hapa Kiabakari-Musoma, huyu ni Mzee Silyvester Korogo (Born on 1932 akiwa mtoto wa nne wa bibi). Wakati picha hii inapigwa jana nilikuwa nazungumza na bibi na swali kubwa aliloniuliza ni...

BIBI; "Kisika...(jina alilonipa utotoni)...namuulizia mwanangu Malima, anaendeleaje?" (Yani, bibi anamuulizia kijana wake mwingine wa kipekee na peke yake aliye hai baada ya kifo cha Mzee Korogo. Ananiuliz kwa sababu iliamriwa asijulishwe kuwa vijana wake wote wamefariki kwa mpigo).

MIMI; "...kama ulivyojulishwa, Uncle Malima alienda Musoma Mjini na amelazwa akitibiwa KISUKARI ambacho hapa Kiabakari hakitibiwi kwani hakuna daktari".

BIBI; "...sasa anaendeleaje huko hospitali?",

MIMI; "...tukitoka kumzika Mzee Korogo mimi na wenzangu tutakwenda Musoma Mjini kumjulia hali".

BIBI; "...ukitoka Musoma uje unieleze hali yake",

MIMI; "...ntafanya hivyo bibi"

BIBI; "....na umwambie aje kunisalimia haraka"

MIMI; "...kwaheri bibi"..

Baada ya Mazungumzo yetu, Padre Wojciech Adam Kościelniak aliongoza ibada fupi nyumbani kwa marehemu kisha tukaelekea kwenye makaburi ya Kanisa Katoliki na kumzika mjomba wetu mpendwa.

Usiku wa kuamkia leo, watoto wa pekee wa bibi waliobakia (MAMA LUCY na MAMA JANE) wakaniita na kunikumbusha mazungumzo yangu na bibi, wakanambia sasa kukikucha kesho (yaani leo Ijumaa), mpelekee bibi yako mrejesho wa hali ya mgonjwa mliyeahidiana, mjulishe amefariki asubuhi. Huu ni MTIHANI MKUBWA kabisa kukabidhiwa na watu wazima and I am speechless! Hii kazi ntaifanyaje?

Kijana wa bibi aliyekuwa amebaki badala ya Mzee Korogo ni huyo Uncle MALIMA tu (aliyestaafu Jeshi mwaka Juzi), Malima amefariki ghafla siku moja baada ya kifo cha kaka yake. Bibi amesafiri na kufika msibani bila kujulishwa kuna msiba juu ya msiba.

Niwaelezeapo jambo hili bibi anajua ana kijana mmoja hai na kuwa amemzika mmoja jana. Kumbe ukweli ni kinyume kabisa, bibi amepoteza vijana wote ndani ya siku mbili na leo lazima aambiwe ukweli mchungu. Hii kazi niliyopewa sijaipenda kabisa!

Mtatiro J,
Kiabakari, Musoma.
0ea9693d03b7a01a40d5bbc2c66b2f00.jpg
 
Pole sana, ni mtihani mkubwa lakini huna budi kuukabili, maisha haya tunapitia mitihani mingi sana
 
Jamani bibi, Mungu amtie nguvu na kumpa faraja, inahuzunisha sana.
 
Mtatiro ni aina ya watu sijua dhaifu au jasiri ...kwa kifupi ni mtu anayejitahidi kuishi kwa uhalisia katika maisha yake ya kila siku na ukifuatilia simulizi zake zote hutoka moyoni kwa uhalisia.
Ni simulizi fupi sana lakini inayobeba maana kubwa sana hasa kwa maisha ya Mwafrika halisi! Poleni sana.
 
Kosa kubwa ulilifanya mwanzo, kusema uongo hasa husiokuwa na faida. Ulipaswa kumueleza pale pale kila kitu alipokuuliza.
Kauli aliyokuambia kwamba "mwambie akiapata nafuu aje haraka kunisalimia" imebeba mengi sana katika kifua cha bibi na inaonekana hakuwa tayari hata kukuambia wewe au mtu yeyote zaidi ya Uncle Malima (RIP). Hili litazidi kumsumbua na kuwaza sana. Na pengine akachukia kama akigundua alidanganywa.
Tuhepuke Uongo.
Mwisho nikupe pole sana kwa misiba mizito ya pamoja kuondokewa na watu muhimu katika Familia yenu.
Pumziko la milele awapee eeh Bwana, na mwanga wa milele awaangazie marehem wapumzike kwa Amani....!
 
Inna Lillah wa Inna Illah Rajiun M/Mungu akupeni nguvu kwenye kipindi hichi kigumu
 
MTIHANI MKUBWA....

Bibi yetu mpenzi (pichani katikati), amezaliwa kabla ya vita ya kwanza ya Dunia. Jana Alhamisi saa 10 jioni
alimzika kijana wake muhimu hapa Kiabakari-Musoma, huyu ni Mzee Silyvester Korogo (Born on 1932 akiwa mtoto wa nne wa bibi). Wakati picha hii inapigwa jana nilikuwa nazungumza na bibi na swali kubwa aliloniuliza ni...

BIBI; "Kisika...(jina alilonipa utotoni)...namuulizia mwanangu Malima, anaendeleaje?" (Yani, bibi anamuulizia kijana wake mwingine wa kipekee na peke yake aliye hai baada ya kifo cha Mzee Korogo. Ananiuliz kwa sababu iliamriwa asijulishwe kuwa vijana wake wote wamefariki kwa mpigo).

MIMI; "...kama ulivyojulishwa, Uncle Malima alienda Musoma Mjini na amelazwa akitibiwa KISUKARI ambacho hapa Kiabakari hakitibiwi kwani hakuna daktari".

BIBI; "...sasa anaendeleaje huko hospitali?",

MIMI; "...tukitoka kumzika Mzee Korogo mimi na wenzangu tutakwenda Musoma Mjini kumjulia hali".

BIBI; "...ukitoka Musoma uje unieleze hali yake",

MIMI; "...ntafanya hivyo bibi"

BIBI; "....na umwambie aje kunisalimia haraka"

MIMI; "...kwaheri bibi"..

Baada ya Mazungumzo yetu, Padre Wojciech Adam Kościelniak aliongoza ibada fupi nyumbani kwa marehemu kisha tukaelekea kwenye makaburi ya Kanisa Katoliki na kumzika mjomba wetu mpendwa.

Usiku wa kuamkia leo, watoto wa pekee wa bibi waliobakia (MAMA LUCY na MAMA JANE) wakaniita na kunikumbusha mazungumzo yangu na bibi, wakanambia sasa kukikucha kesho (yaani leo Ijumaa), mpelekee bibi yako mrejesho wa hali ya mgonjwa mliyeahidiana, mjulishe amefariki asubuhi. Huu ni MTIHANI MKUBWA kabisa kukabidhiwa na watu wazima and I am speechless! Hii kazi ntaifanyaje?

Kijana wa bibi aliyekuwa amebaki badala ya Mzee Korogo ni huyo Uncle MALIMA tu (aliyestaafu Jeshi mwaka Juzi), Malima amefariki ghafla siku moja baada ya kifo cha kaka yake. Bibi amesafiri na kufika msibani bila kujulishwa kuna msiba juu ya msiba.

Niwaelezeapo jambo hili bibi anajua ana kijana mmoja hai na kuwa amemzika mmoja jana. Kumbe ukweli ni kinyume kabisa, bibi amepoteza vijana wote ndani ya siku mbili na leo lazima aambiwe ukweli mchungu. Hii kazi niliyopewa sijaipenda kabisa!

Mtatiro J,
Kiabakari, Musoma.
0ea9693d03b7a01a40d5bbc2c66b2f00.jpg
Pole sana kamanda Julius, nadhani mjiandae kwa msiba wa 3 kwa sababu ninahisi Bibi hawezi kuhimili mshituko huo, ataaga pia! Mungu awape nguvu kamanda.
 
MTIHANI MKUBWA....

Bibi yetu mpenzi (pichani katikati), amezaliwa kabla ya vita ya kwanza ya Dunia. Jana Alhamisi saa 10 jioni
alimzika kijana wake muhimu hapa Kiabakari-Musoma, huyu ni Mzee Silyvester Korogo (Born on 1932 akiwa mtoto wa nne wa bibi). Wakati picha hii inapigwa jana nilikuwa nazungumza na bibi na swali kubwa aliloniuliza ni...

BIBI; "Kisika...(jina alilonipa utotoni)...namuulizia mwanangu Malima, anaendeleaje?" (Yani, bibi anamuulizia kijana wake mwingine wa kipekee na peke yake aliye hai baada ya kifo cha Mzee Korogo. Ananiuliz kwa sababu iliamriwa asijulishwe kuwa vijana wake wote wamefariki kwa mpigo).

MIMI; "...kama ulivyojulishwa, Uncle Malima alienda Musoma Mjini na amelazwa akitibiwa KISUKARI ambacho hapa Kiabakari hakitibiwi kwani hakuna daktari".

BIBI; "...sasa anaendeleaje huko hospitali?",

MIMI; "...tukitoka kumzika Mzee Korogo mimi na wenzangu tutakwenda Musoma Mjini kumjulia hali".

BIBI; "...ukitoka Musoma uje unieleze hali yake",

MIMI; "...ntafanya hivyo bibi"

BIBI; "....na umwambie aje kunisalimia haraka"

MIMI; "...kwaheri bibi"..

Baada ya Mazungumzo yetu, Padre Wojciech Adam Kościelniak aliongoza ibada fupi nyumbani kwa marehemu kisha tukaelekea kwenye makaburi ya Kanisa Katoliki na kumzika mjomba wetu mpendwa.

Usiku wa kuamkia leo, watoto wa pekee wa bibi waliobakia (MAMA LUCY na MAMA JANE) wakaniita na kunikumbusha mazungumzo yangu na bibi, wakanambia sasa kukikucha kesho (yaani leo Ijumaa), mpelekee bibi yako mrejesho wa hali ya mgonjwa mliyeahidiana, mjulishe amefariki asubuhi. Huu ni MTIHANI MKUBWA kabisa kukabidhiwa na watu wazima and I am speechless! Hii kazi ntaifanyaje?

Kijana wa bibi aliyekuwa amebaki badala ya Mzee Korogo ni huyo Uncle MALIMA tu (aliyestaafu Jeshi mwaka Juzi), Malima amefariki ghafla siku moja baada ya kifo cha kaka yake. Bibi amesafiri na kufika msibani bila kujulishwa kuna msiba juu ya msiba.

Niwaelezeapo jambo hili bibi anajua ana kijana mmoja hai na kuwa amemzika mmoja jana. Kumbe ukweli ni kinyume kabisa, bibi amepoteza vijana wote ndani ya siku mbili na leo lazima aambiwe ukweli mchungu. Hii kazi niliyopewa sijaipenda kabisa!

Mtatiro J,
Kiabakari, Musoma.
0ea9693d03b7a01a40d5bbc2c66b2f00.jpg
Poleni kwa misiba...hakuna namna mkuu,andaa mazingira ili bibi ajue ukweli.
Watu wa zamani, wana machale kwa hiyo muda si mrefu atagundua tu.
Aambiwe kabla hajagundua yeye mwenyewe.
 
Hii si stori tu kwamba stori yakusemwa ,nyuma ya pazia lipo kuu,lilobeba hiyo stori ,
Pamoja na ukongwe wa bibi huenda ikawa ngumu sana kuukabir ukwel juu yalotokea hasa ukizingatia ukongwe wake na dhat kwa wanaye walosalia
 
Back
Top Bottom