apolycaripto
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 644
- 225
Nimesoma kwa makini maoni ya Mwanakijiji pamoja na maoni ya Slaa,Zitto,Lwetama n.k.Nilichokibaini cha msingi hapa ni kuwa Mwanakijiji ameanza kupata wasiwasi na mbinu inayotumiwa na CDM katika harakati za kushika dola.Kwa Mwanakijiji anaona kivuli cha CCM kinaanza kuongezeka hasa baada ya mkakati wa kujivua gamba ambao kimsingi unanafasi yake kubwa katika mabadiliko ya Chama.Hapa Mwanakijiji anaona CCM katika uvuaji gamba haikomei kwenye mabadiliko ya CC na Sekretarieti yake,bado inamikakati makini ya kimafia yenye kuhakikisha CDM inapotea katika masikio ya Wananchi.
Upande wa pili,Mwanakijiji anaitizama CDM kama chanzo cha kuipa nguvu CCM badala ya kuidhoofisha.Mwanakijiji anaitizama CDM mbali na kupuuza mabadiliko ndani ya CCM bali pia imekuwa msaada mkubwa kwa mabadiliko hayo.CDM hapa inashindwa kutambua ni wapi CCM inapaswa kutokomezwa?na ni silaa gani ya kuitokomeza CCM?.
Maoni ya DR. Xavier Lwetama ambayo yameonekana wazi kupinga maono ya Mwanakijiji inadhihirisha uvivu wa kufikiri alionao.Lwetama mbali na kuwa na focus ya kutamani CCM ife ata Leo lakini inaonyesha njia ya CCM kufa haioni zaidi ya kutanguliza chuki binafsi na wala si " strategy".Dr. Lwetama akiwa anajinadi kama Mwanachama mfu wa CCM ,hii pia inaongeza changamoto ya kutokukubalika kwa hoja yake kwani ni dhahiri anaonyesha ushabiki wake kisiasa ni katika mlengo wa "opportunistic".Maoni yake ya kudai ushindani wa kimaadili (kutokutumia mbinu ya kudhoofishana) ila CCM ife hapa ndio njia na mbinu ya Lwetama inaposhindwa.CCM haiwezi kufa bila kudhoofika,ajali kwa binadamu ni sawa lakini si mfano wa CCM kufa kama ajali ya basi.
CDM imeonyesha ku-survive kwa makosa ya CCM,hii inamaana CCM ikijirekebisha kutokana na makosa yake CDM haipo.Mwanakijiji anapata wasiwasi kwani mwazoni CDM ilikuwa inampa nguvu na kuona kifo cha CCM kinakaribia sasa wasiwasi unatanda baada ya kuona CDM imempa kikombe CCM (adui) sasa karudi kazini na dhana za kummaliza mtoa kikombe.
Mwanakijiji hajakosea kwani anajua CCM si chama cha kawaida kama CDM inavyodhani.Anatambua na kusifu katika mada yake kuwa hawa ni watu wa siasa za Kisayansi na mbinu za kimafia kwa maana ya ubingwa wa kuuwa vyama pinzani.Ni kweli CCM inauwezo huo na kama CDM haitofikiri njia mbadala za kujiimalisha (kuachana na nyimbo za list of shame,remix etc.) ambazo CCM imeisha zirekodi kwa jina lake itakufa kabla ya 2015.
CCM haitanii na ndio kwanza safari imeanza na wanakwambia si nguvu ya soda.Kumbuka uzoefu wa CDM kisiasa ni mdogo kulinganisha na CCM hivyo na adui CCM ameishatambua silaa ilizonazo CDM sasa kilichobaki ni mchakato wa kukimaliza kisayansi.
Changamoto anayotoa Mwanakijiji kwa CDM ni kubwa kutokana na maswali haya.
Je!CDM watauweza mziki wa CCM?Je! CDM wanauwezo wa kucheza bila kusikiliza mziki wa CCM?.Ikumbukwe kuwa Watanzania watampigia kura Yule mwenye uwezo wa kumiliki Jukwaa.
Upande wa pili,Mwanakijiji anaitizama CDM kama chanzo cha kuipa nguvu CCM badala ya kuidhoofisha.Mwanakijiji anaitizama CDM mbali na kupuuza mabadiliko ndani ya CCM bali pia imekuwa msaada mkubwa kwa mabadiliko hayo.CDM hapa inashindwa kutambua ni wapi CCM inapaswa kutokomezwa?na ni silaa gani ya kuitokomeza CCM?.
Maoni ya DR. Xavier Lwetama ambayo yameonekana wazi kupinga maono ya Mwanakijiji inadhihirisha uvivu wa kufikiri alionao.Lwetama mbali na kuwa na focus ya kutamani CCM ife ata Leo lakini inaonyesha njia ya CCM kufa haioni zaidi ya kutanguliza chuki binafsi na wala si " strategy".Dr. Lwetama akiwa anajinadi kama Mwanachama mfu wa CCM ,hii pia inaongeza changamoto ya kutokukubalika kwa hoja yake kwani ni dhahiri anaonyesha ushabiki wake kisiasa ni katika mlengo wa "opportunistic".Maoni yake ya kudai ushindani wa kimaadili (kutokutumia mbinu ya kudhoofishana) ila CCM ife hapa ndio njia na mbinu ya Lwetama inaposhindwa.CCM haiwezi kufa bila kudhoofika,ajali kwa binadamu ni sawa lakini si mfano wa CCM kufa kama ajali ya basi.
CDM imeonyesha ku-survive kwa makosa ya CCM,hii inamaana CCM ikijirekebisha kutokana na makosa yake CDM haipo.Mwanakijiji anapata wasiwasi kwani mwazoni CDM ilikuwa inampa nguvu na kuona kifo cha CCM kinakaribia sasa wasiwasi unatanda baada ya kuona CDM imempa kikombe CCM (adui) sasa karudi kazini na dhana za kummaliza mtoa kikombe.
Mwanakijiji hajakosea kwani anajua CCM si chama cha kawaida kama CDM inavyodhani.Anatambua na kusifu katika mada yake kuwa hawa ni watu wa siasa za Kisayansi na mbinu za kimafia kwa maana ya ubingwa wa kuuwa vyama pinzani.Ni kweli CCM inauwezo huo na kama CDM haitofikiri njia mbadala za kujiimalisha (kuachana na nyimbo za list of shame,remix etc.) ambazo CCM imeisha zirekodi kwa jina lake itakufa kabla ya 2015.
CCM haitanii na ndio kwanza safari imeanza na wanakwambia si nguvu ya soda.Kumbuka uzoefu wa CDM kisiasa ni mdogo kulinganisha na CCM hivyo na adui CCM ameishatambua silaa ilizonazo CDM sasa kilichobaki ni mchakato wa kukimaliza kisayansi.
Changamoto anayotoa Mwanakijiji kwa CDM ni kubwa kutokana na maswali haya.
Je!CDM watauweza mziki wa CCM?Je! CDM wanauwezo wa kucheza bila kusikiliza mziki wa CCM?.Ikumbukwe kuwa Watanzania watampigia kura Yule mwenye uwezo wa kumiliki Jukwaa.