Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,238
Hata kama tuna hasira namna gani dhidi ya CCM ni lazima tukiangalie chama hicho kwa mtazamo wa chama kinachoongoza nchi kwa sasa. Tatizo letu tunaombea CCM idhoofike yenyewe (Naturally) ili vyama vyetu viimarike kwa udhaifu wa CCM. Mtazamo wangu tuimarishe vyama vyetu ili uimara wake uidhoofishe CCM na kama nchi tufaidike.
Kama kuna mtu anadhani mapinduzi aliyofanyiwa Thabo Mbeki na Jacob Zuma ndani ya ANC umeiletea mafanikio Afrika Kusini anajidanganya!! Hawa hawa kina Julius Malema ndiiyo waliongoza mapinduzi haya na aliyekuwa mfadhili wa shughuli yenyewe Jacob Zuma naye tena anatishiwa na wanamapinduzi "wenzake" kupinduliwa.
Kama hasimu wa Kikwete ndiye atakuwa Mwenyekiti na tunakoelekea inaonekana kwa mara nyingine wanasiasa wanaamini Rais ajaye atatoka tena CCM Urais wa Kikwete tunataka kuuweka rehani na inavyoonekana hakuna nguvu ya kuhimili (Shock Absorb) dhoruba ya kuuweka rehani Urais wa Kikwete. Mwaka 1994 wakati Urais wa Mwinyi unatashiwa na kina Malecela na Kolimba alikuwepo Nyerere, leo yupo nani?
Kama kuna mtu anadhani mapinduzi aliyofanyiwa Thabo Mbeki na Jacob Zuma ndani ya ANC umeiletea mafanikio Afrika Kusini anajidanganya!! Hawa hawa kina Julius Malema ndiiyo waliongoza mapinduzi haya na aliyekuwa mfadhili wa shughuli yenyewe Jacob Zuma naye tena anatishiwa na wanamapinduzi "wenzake" kupinduliwa.
Kama hasimu wa Kikwete ndiye atakuwa Mwenyekiti na tunakoelekea inaonekana kwa mara nyingine wanasiasa wanaamini Rais ajaye atatoka tena CCM Urais wa Kikwete tunataka kuuweka rehani na inavyoonekana hakuna nguvu ya kuhimili (Shock Absorb) dhoruba ya kuuweka rehani Urais wa Kikwete. Mwaka 1994 wakati Urais wa Mwinyi unatashiwa na kina Malecela na Kolimba alikuwepo Nyerere, leo yupo nani?