Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 305
- Thread starter
- #161
Rev. KishokaJe tofuauti yao ya ki-Itikadi na mfumo na CCM ni ipi?
It is 2010, mambo yanabidi kwenda kisayansi na si kienyeji enyeji.
Kwa nchi kama Tanzania kuanza kufikilia mifumo ya kisayansi ni vigumu sana, mifumo ya kisayansi inatengemea mipango ya nchi na mipango inategemea uchumi na uchumi unategemea discipline kwenye ukusanyaji wa kodi. Kama huna discipline kwenye kodi ni ndoto kufikilia mifumo ya kisayansi.
Nchi zilizoendelea kama Canada uliko wamefanikiwa kwa sababu discipline ya kodi ni ya hali ya juu mtu huwezi kukwepa kulipa kodi, nilibahatika kufanya kazi kwenye Borough Council moja ya nchi zilizoendelea utaona ni jinsi gani watu wanavyokimbilia kulipa kodi na ukimchelewesha mlipa kodi ana haki ya kukushitaki watu wote wamejengewa tabia hivyo.
Tukirudi kwetu leo ukiwauliza TRA projection ya mapato ya mwaka ujao ikoje utakuwa unawaonea bure, kwa sababu hawajui wana vyanzo gani vya mapato vyenye uhakika, kwa hiyo nchi haiwezi kuwa na mipango scientific au mradi mkubwa bila kuwa na uhakika wa mapato zaidi ya kutegemea wahisani.
Leo ukimuuliza waziri wa elimu dropouts ya wanafunzi mwaka kesho ni ngapi atakuambia hajui maana yake nini mbali ya kutojua dropouts hana hata mpango wa kuwasaidia.
Tukija kwenye vyama vya siasa ukisema vijiendeshe kisayansi itakuwa ngumu sana ndugu yangu Rev. ukiwauliza hata hao CCM watafanya nini siku 100 za mwanzo zaidi ya kukuambia watatekeleza ilani ya chama watakuambia hata wao hawajui kwa sababu hilo fungu na hayo mapato ya kutekeleza hawayajui sembuse Chadema au CUF ambao nafikiri kwenye hizo siku 100 za mwanzo watakuwa bado wanagombania vyeo na wizara.
Naweza kusema kuwa mawazo yako ni mazuri lakini kwa tanzania ya leo itakuwa vigumu sana kutekelezeka, Tanzania haijawa na mfumo endelevu unaoeleweka hata hao CCM hawana mfumo unaojulikana, kwa hiyo kutaka vyama vingine kwanza viunde mifumo yao ndipo vipewe ridhaa ya kuongoza utakuwa unavionea bure, viache viingie kwenye system ndipo vitakapopata fulsa ya kujenga na kuendeleza mifumo wanayoitaka.