Mtego wa Rais kwa CAG

Mtego wa Rais kwa CAG

Leo katika kufatilia taarifa ya habari katika kituo kimoja cha television hapa nyumbani, imeonesha Mkaguzi Mkuu wa hesabu wa Serikali amekabidhi ripoti yake kwa Mh. Rais ikulu.

Katika makabidhiano hayo, Rais ameenda mbali zaidi na kumpa kazi nyingingine, "akimtaka" Mkaguzi huyo akakague migodi ya madini na aje na ripoti ya kuonesha taifa/serikali ina nufaika vipi na mchanga unaosafirishwa kwenda nje.

Mbali na kumuagiza huko, Rais kasema kwamba, ataunda tume nyingine ichunguze suala hili hilo, na ataunda "timu" nyingine hisiyojulikana (invisible team) kuchunguza jambo hilo hilo pia.

Sasa hapa najiuliza, kuna ulazima gani tena Rais aunde tume na invisible team, wakati ameishamwagiza CAG kufanya jambo hilo?

What if, kama hiyo tume na team zikaja na majibu tofauti na ya CAG?

Je Kazi anayofanya CAG haiaminiki kwa serikali au Rais ndio hana imani na CAG?

Hiyo ni kawaida sana kwenye masuala ya kiuchumi.

Ndiyo maana kuna kitu kinaitwa intelligence.

Nnafurahi sana kusikia Rais kuyasema hayo.

Hilo ni dongo kwa wale wanaosema "anakurupuka".

Hongera Magufuli, hivyo ndiyo sahihi, lazima upate information kutoka sehemu tofauti kwa miono tofauti ili ufanye maamuzi sahihi.

Ndiyo maana ulipomtunbua Anne Kilango nikasema yule mwanamke ni bogus kabisa kutokuelewa kuwa Rais anapokutuma kazi ana njia nyingi nyingine za kupata taarifa.

Mleta mada usiwe kama Anne Kilango. Tumia kichwa chako kufikiri japo kiduchu na usikiwache kuwa ni mzigo tu juu ya mabega yako.
 
Binafsi, naona ni sawa kabisa, nchi zote zilizoendelea hakuna siku hata moja utafanya kazi pekee ni lazima kuna taasisi nyingi sana zinakufatilia kuona unachofanya kama kipo sahihi/ repoti zinakuwa sahihi.

Na pia , Rais amefanya vizuri sana kumwambia wazi kuwa kuna timu za watu wengine pia wanaofanya utafiti juu ya hicho kitu.

Na hii itasaidia sana watu kuwa waadilifu.

Labda, ushauri sasa Rais, wakati mwingine na kazi zitakazofuatia usiseme kuwa anawafatilia .
Alifanye kwa siri kisha alinganishe na majibu yanayoletwa na tume au wataalamu au hao invisibles.

Na hili litaipatia akili hata bunge ili lisiwe kundi la vibwagizo vya ndiyoooooooo na kiitikio cha siyoo.

Lazima, tufike mahala pazuri kama watu watamuelewa JPM.
 
Si kwamba hamwan CAG la hasha!! Bali kiuahalisia nikutaka report yenye uhakika kwa kua ktk nyanja zinazo ipa taifa fedha ni madin na uwezekano upo wa kufanywa figisu figisu ikatengenezwa report isiyo sahihi na ndyo maana amempa mkwara huo.
 
mtu analalamika pesa haitoshi kukagua hesabu zote za serekali utamwamini vipi wakati anaweza hongwa raisi yuko sahihi kimtizamo wahasibu walikagua mahesabu miaka kumi hawakuwahi kuleta hasara iliotokana na wafanyakazi hewa leo tuwaamini vipi jpm hadanganyiki
 
Hatuwezi kuota. Magufuli kaweka kodi mpaka ya ndoto tunabana matumizi.


Si kweli.

Magufuli hawezi kuweka sheria mpya bila kuipitisha hiyo sheria bungeni. Sijaona kodi yoyote mpya.

Sema upinzani hamna hoja ya siasa mlichobaki nacho ni hoja za kurukia, mnataza wapi kuna uoenyo ndiyo mnabwabwaja.

Nnashangaa sana pale nnapoona upinzani unakosa mawazo mapya (ideas), unakosa hata kuongolea matukio (events) unabaki kuongelea watu.

Hoi.
 
Inaweza kuwa mbinu nzuri, ila inategemea inatumika Je, na wakati gani?
Kwa hili mpaka kumuambia moja kwa moja kuwa kafanye hivi ila na mimi nitafanya hivi kujua nilichokuambia ukafanye kuona kama kipo sawa, sidhani kama ni sahihi. Kwanza unaonesha wazi pengine huna imani na ninachofanya au nifanye iwapo ikitokea nimekosea sehemu basi ndio itumike kama sehemu ya kunisemea.
mkuu upo sahihi inaonyesha dhahiri kuwa mwenye nchi hana mahusiano mazuri na mkaguzi mkuu wa serikali (hana imani nae).
 
Hivi sheria inasemaje? CAG ana haki ya kufanya auditing kwenye taasisi/kampuni binafsi? Au ni pale tu kunapokuwa na maelekezo maalum?
 
Si kweli.

Magufuli hawezi kuweka sheria mpya bila kuipitisha hiyo sheria bungeni. Sijaona kodi yoyote mpya.

Sema upinzani hamna hoja ya siasa mlichobaki nacho ni hoja za kurukia, mnataza wapi kuna uoenyo ndiyo mnabwabwaja.

Nnashangaa sana pale nnapoona upinzani unakosa mawazo mapya (ideas), unakosa hata kuongolea matukio (events) unabaki kuongelea watu.

Hoi.
Magufuli yeye ni bunge, mahakama, serikali ya mitaa na mpaka kanisa.

Sijui unaongelea bunge gani wakati kashaliamrisha bunge litunie fedha za tafrija yake kwenye habari za hospitali.

Utaongelea mahakama gani wakati Magufuli kahutubia Mahakama na kuipangia kazi.

Utaongelea serikali za mitaa gani wakati Magufuli kaenda kwa Mzee wa Upako na kuaguza barabara itengenezwe.

Anaenda kanisani na kutoa hotuba ya kisiasa mbele ya kanisa.

Na juzi kaingikia mpaka wasanii anaaanza kuwapangia mistari ya kuandika kwenye nyimbo zao.

Sasa hivi ataomba atoe single na Ney wa Mitego.
 
Inaweza kuwa mbinu nzuri, ila inategemea inatumika Je, na wakati gani?
Kwa hili mpaka kumuambia moja kwa moja kuwa kafanye hivi ila na mimi nitafanya hivi kujua nilichokuambia ukafanye kuona kama kipo sawa, sidhani kama ni sahihi. Kwanza unaonesha wazi pengine huna imani na ninachofanya au nifanye iwapo ikitokea nimekosea sehemu basi ndio itumike kama sehemu ya kunisemea.
Only in God we trust...
 
Rais makini wakati wote huweka msisitizo kuonesha kazi hiyo ni muhimu. Hapa sio issue ya kuaminiana bali ni kulinda maslahi ya Taifa. Na kama CAG yupo tentative lazima atakwenda kufanya kazi bora zaidi. Mazoea ya kuaminiana ndiyo yamefanya nchi imekuwa na ulaji na walaji kila kona. Ni mjinga pekee anayeweza kuhoji ubora wa Rais tuliyenaye Tanzania kwasasa. Ukifuatilia kwa makini utaona wanaohoji ni wale waliokuwa kwenye mtandao wa kuifanyia maovu nchi yetu Tanzania. Either wapiga deals haramu au wauza unga. You are no more. Go to hell. Leave our country alone.

Bahati mbaya tuliyonayo ni hao ambao ndiyo wenye access kwenye key boards...Watanzania average wana akili zao ila kwasababu tu ya hawa waovu wachache walinyimwa haki ya kupata elimu na nafasi zenye kuwawezesha kutoa maoni yao kama hawa waliokosa uzakendo kwakua tu mkate wao sasa umepunguzwa ukubwa kwakugawia wenzao...
 
Magufuli yeye ni bunge, mahakama, serikali ya mitaa na mpaka kanisa.

Sijui unaongelea bunge gani wakati kashaliamrisha bunge litunie fedha za tafrija yake kwenye habari za hospitali.

Utaongelea mahakama gani wakati Magufuli kahutubia Mahakama na kuipangia kazi.

Utaongelea serikali za mitaa gani wakati Magufuli kaenda kwa Mzee wa Upako na kuaguza barabara itengenezwe.

Anaenda kanisani na kutoa hotuba ya kisiasa mbele ya kanisa.

Na juzi kaingikia mpaka wasanii anaaanza kuwapangia mistari ya kuandika kwenye nyimbo zao.

Sasa hivi ataomba atoe single na Ney wa Mitego.


Naam, wakati watu wanalia vitanda hamna mahospitalini wewe unafanya sherehe ya mamilioni? Inaingia akilini hiyo?

Kuhusu mzee wa upako, ni safi sana. Hebu soma hiki kipande "...wenye mahitaji ya kuabudu waabudu...".

Ukitaka "context" ya hicho kipande, pitia hapa: Siasa, Uchumi, Dhahabu, Neema na Laana zake
 
Back
Top Bottom