Mjomba, hakuna atakayekuja kutukomboa ila ni sisi wenyewe
Ni makosa kuwa na wabunge kutoka chama kimoja tu.
Hao ni wengi mno 3 wanaweza wasifike bunge zimaTulisema hapa toka mwanzo kwamba chadema itaambulia wabunge 10 tu
Ichi ndo kiliniboa sana, badala ya kupinga kisicho wanapinga kila kitu, ni kama kamtu kabishi kwa kila lifanywaloPinga pinga kila kitu ya wapinzani imewakosti sana. Ule ulikuwa ni mkakati usiozaa matunda. Wajifunze sasa kuwa na siasa zenye tija la sivyo wataendelea kupukutika.
Ichi ndo kiliniboa sana, badala ya kupinga kisicho wanapinga kila kitu, ni kama kamtu kabishi kwa kila lifanywalo
Wengi wanamtaka maguHivi kuna haja gani ya kupiga kira ilhali anayechaguliwa na wengi anachakachuliwa mnaletewa msiyemtaka?
Mkuu usihofuIkulu inaenda kukaliwa na mtu asiye na baraka ridhaa za wapiga kura, manyanyaso mateso uonevu kubambikiwa kesi kupigwa risasi, wafanyabiashara kubambikiwa kodi TRA, unyanyasaji uovu kuendelea kama awamu iliyopita
Kwani asipo pata lema au mdee au nani wa upinzani maisha yao yana athirika vipi? Wangeamua kitambo kuunga juhudi tungewafanya nn? Angalia future yako na watoto wako unao wakuza kwenye mazingira ya kidhalimu.....Tunako elekea hata watoto shule tutalipa ada kubwa wataishia kukariri na vibuti kama babu zao viongozi wa kisiasa wanavyo pitishwa pitishwa...Nakuhakikishia hawatafika labda jumlisha na viti maalum
Yaah nimepata hii kitu, nmeambiwa kwamba kamkimbiza mpinzani wake karibu kata 6 kwa kumuacha mbali sana...!Sugu anaongoza
Huu mkakati wakiendelea nao hautawafaa kabisa. Watazidi kupoteza kuungwa mkono na wananchi.Ichi ndo kiliniboa sana, badala ya kupinga kisicho wanapinga kila kitu, ni kama kamtu kabishi kwa kila lifanywalo
Hawa wenye vyombo vya habari nawasubiria kwa hamu vilio vitaendelea kuwakuta kila uchwaoKama umefatilia vizuri, nidhahiri nia ya chama tawala ni kuchukua viti vyote vya ubunge nchini.
Fatilia uzuiaji wa mikutano kwa Wapinzani kwa miaka mitano, vyombo vya habari kufungwa midomo na kuanza kus-support chama tawala, kauli za utata za NEC, wakurugenzi kupigwa mkwara endapo watatangaza wapinzani na ilihali yeye kawateua, kesi ya kupinga wakurugenzi kusimamia uchaguzi kupingwa chini, vioja vya kusimamishwa na NEC, polisi kuvuruga mikutano ya upinzani bila kusahau matukio ya leo ya kura.
Usisahau kuna wabunge 28 wamepita bila kupingwa tayari.
Hofu yangu kuna uwezekano kipindi hiki wabunge wa upinzani wasifike hata kumi kama sio watano, ngoja tuone mchezo.