"Hivi wewe jamaa una akili timamu kweli au unaishi kwa shemeji yako mpaka akili zako zimebaki kuwa za kitoto? Unakuja hapa kuwadharau wanaume wanaopambana asubuhi kwenye daladala kutafuta riziki ya familia zao, huku ukisahau kuwa wewe mwenyewe juzi umepanda hiyo daladala kwa sababu tu gari la shemeji yako liliharibika! Yaani unaringia dudu na jasho la mume wa dada yako kiasi cha kuona watu wanaovuja jasho lao wenyewe hawana akili? Huu ni ushamba na ulimbukeni wa kiwango cha lami.
Bandiko lako linaonyesha wazi kuwa wewe ndiye mfano halisi wa man-child (baba zima zuzu) unayewasingizia wenzako. Mtu mzima aliyekomaa kifikra hawezi kuwa na shobo ya kwenda kupanda usafiri wa umma 'just for fun' ili akawacheke wapambanaji. Hiyo ni tabia ya chawa na watu tegemezi waliopata nafasi ya kukaa kwenye kiti cha gari la kuazima wakajihisi wamefika mbinguni. Umekariri maisha kwamba kufanikiwa ni kununua kimeo cha milioni 6 ili kuwaringishia watu barabarani? Huko ni kudumaa kiakili.
Watu wazima unaowaona hapo kituoni wana vipaumbele vya maisha; wanasomesha watoto shule za maana, wanajenga nyumba, na wanatunza wazazi wao kwa pesa ya jasho la halali. Hawana muda wa kuishi maisha ya maigizo ya mtandaoni kama wewe. Mwanaume anayegombania daladala saa kumi na moja asubuhi ana heshima na utu mara mia moja kuliko tegemezi mnyanyasa makalio anayeishi kwa shemeji yake lakini ana dharau kwa wanaume wenzake. Shuka kwenye mgongo na tege la shemeji yako, pambana na maisha yako binafsi kwanza ndipo uje uongee na watu wazima wanaojielewa. Umekalia umbeya na dharau wakati mfuko wako umetoboka, nyoo!
Jiangalie sana yasije yakukuta yaliyomkuta Mwijaku aliyekuwa anatupigia kelele kama wewe mpaka alipoachika na mkewe, ambaye ndiye alikuwa mmiliki halali wa ghorofa, akabaki mweupe peee mpaka kupewa gari na Silent Ocean. Tupo tunakusubiri hapa jamvini pale Shemeji yako atakapo muacha dada yako na wewe uanze kuayaona maisha ya kweli!"