Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Amavubi ww ni me au ke?itakua shega tu lazima hao wachezaji watafute majina rahisi lol
subiri kipindi cha maswali ya nyongezaAmavubi ww ni me au ke?
Hawa simba kwa kutuletea majina ya ajabu wako vzr!jina la liboro bado halijaisha wameona haitoshi wanatuletea serunkuma!
Liboro anampigia Sserunkuma pale.
Kwa hiyo hata kabila la wasukuma huwa halitaji? Kweli ujinga mwingine hauna namna ya kuulezea ukaleta mantiki.
Tatizo Wanahabari na watanzania(hasa wa BARA, afadhali WAZENJI) kwa ujumla hatufundishwi jinsi ya kutamka maneno kwa kiufasaha ,mfano Magharibi tunaitamka isivyo sahihi. Wanahabari wetu hasa wa michezo wajifunze jinsi gani watangazaji wa mpira ulaya wanavyotamka majina ya wachezaji kulingana na yanavyotakiwa kutamkwa ktk lugha za asili za wachezaji.Mfano Thierry Henry,(Henry) linatamkwa Kifaransa( Aanre) sio kienglish ,vile vile Robert Pires (Robert)linatamkwa kifaransa (Robee ) ingawaje lipo hata kwa kienglish. Kesho ukiangalia mpira au International news zingatia majina yanavyotamkwa. Kurudi katika hili jina huyo mtangaji atakuwa alidhani jina linatamkwa kwa Kiswahili badala ya lugha asili ya mwenye jina. Anyway ndiyo weakness moja ya lugha yetu kubwa ya Kiswahili matamshi yake yapo katika staili moja.Vile vile watanzania tuna ujinga wa kutozingatia jinsi neno linavyotakiwa kutamkwa bali ili mradi limekaribia na jinsi linavyotamkwa.
watangazaji wetu wengi weuoe sana na nisababu ya nepotismkuna mtangazaj wa magic fm hutangaza morning magic hawez kutamka magharibi hutamka mangaribi
Aka kanjanja............watangazaji wetu wengi weuoe sana na nisababu ya nepotism
Alianza Kumambili Keita Baadae Wakaja Libolo Ili Kuweka Mambo Sawa, Sasa Wakaona Waje Wote Kwa Pamoja Ili Mimba Ipatikane Haraka.Mboob na serunkuma,,,,,,haya majina....!!!
Katika hali isiyo ya kawaida, mtangazaji Christina Mbezi alifanya kila awezalo kukwepa kutamka jina la SSerunkuma, mshambuliaji wa Gor Mahia raia wa Uganda aliyetua nchini kufanya mazungumzo na klabu ya Simba. Mtangazaji huyo alikuwa anakwepa kutamka neno hilo wakati akisoma yaliyoandikwa magazetini katika kipindi cha Tuongee Magazetini. Mfano, alipotakiwa kusema 'SSerunkuma atua Dar', yeye alisema 'atua Dar'. Aliendelea kulikwepa neno hilo hata wakati akiisoma habari kwa undani na pia hata alipokutana na jina hilo katika magazeti mengine.
Hii itakuwa ni changamoto kwa waswahili iwapo mshambuliaji huyo atafanikiwa kusajiliwa na Simba!