Baadhi ya pumba za Musiba za hivi karibuni kabisa yaani leo ni hizi zifuatazo - angalia fb yake
Nimefuatilia kwa makini sakata la kijana anayedaiwa kuwa ni mwanajeshi wa kambi ya Monduli kupiga picha na wabunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Yapo mambo yanayotia mashaka juu ya magwanda hayo na tukio zima kwa ujumla.
Chadema walilenga nini kumtumia kijana huyo na gwanda lake?? Je,, kwa upande mwingine Chadema wameamua kulibip Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Watanzania? je ni kweli CHADEMA tyr wana Silaa na Sare za Jeshi nyingi wanazihifadhi Mbezi.
Hapo ndipo tutajua umakini wao. Ninavyojua na wengi tunavyojua,, wanajeshi hawaruhusiwi kuwa washabiki wa chama chochote cha siasa,, na kama kweli ni mwanajeshi mzalendo aliyeiva hawezi kukubali kuvunja sheria zinazomuongoza.
...
Kwa mujibu wa VYanzo vyangu vya habari kutoka katika chombo hicho kikubwa cha ulinzi wa nchi na mipaka yake,wamesema askari walioko kikosi cha Monduli hakuna jina kama hilo na hawajawahi kusikia wala kuona kijana kama huyo hata katika vyuo vya kijeshi hapa nchini.
Lakini kibaya zaidi kijana huyo alipoulizwa na kuhojiwa na wazee wa Amani kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama wa raia na Mali zake kwa kuanza wakianza kumuuliza yeye ni depo gani alishindwa kujibu na hata hajui maana ya depo ama inteki gani hajui kabisa,alipoendelea kuulizwa ww namba yako ya jeshi ni namba gani ama umemaliza elimu ya kijeshi lini hajui wala hajawahi kusikia habari za namba.
Lakini kibaya zaidi habari za kuaminika zinasema kijana huyu anafanya kazi pale Club Billicanas Posta Dar-es-salaam club ambayo inamilikiwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe.Freeman Alkael Mbowe na hiyo ilikuwa ni njama za kuwahadaa wananchi juu ya kwamba JWTZ wameanza kuingia ndani yake.
HABARI Za Chadema kuwa na mipango ya kuviyumbisha na kuvichafua vyombo vya Dola ni mbinu waliyopewa na Wajerumani na Waingereza katika kikao chao mwaka jana jijini Arusha ambapo pia waliwapa maagizo ya kuhakikisha kwamba wanakesha katika mitandao wakiitukana Serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ninavyojua na wengi tunavyojua,, wanajeshi hawaruhusiwi kuwa washabiki wa chama chochote cha siasa,, na kama kweli ni mwanajeshi mzalendo aliyeiva hawezi kukubali kuvunja sheria zinazomuongoza.
Je Chadema kufanya utoto huu na upuuzi huu tena kupitia vyombo vya habari ni kuvidharau vyombo vya Ulinzi ambavyo hata wao vinawalinda? je hao wazungu wanaowapa mbinu hii wanawalipa kiasi gani na huyo kijana inasemekana amepewa milioni 2 tu hata hakufikiria kama jela inamkaribia.
Kwa suala hili wale wote Lema,Nassar wanapaswa kukamatwa na kuhojiwa na vyombo vya dola lakini wajue kuwa yule kijana atasema ukweli wote haya niliyoyasema ni machache sana wataumbuka na ujanja wao utaishia pabaya.
Tafakari na chukua hatua
#########################################
Tahadhari na Angalizo kwa Wananchi na Watanzania kwa ujumla:
CHADEMA ni HATARI
...Uchaguzi wa 2010 walisambaza jumbe mbalimbali kwa sms maneno haya yalikuwe "...tuangane kumung'oa MJAHIDINA ikulu, ...mchague Dr.Slaa"
... zingine zilisomeka ...usiruhusu MJAHIDINA abaki ikulu mchague Dr. slaa"
je umeona sahizi walivyobadili mbinu umeona wanavyo shabikia migomo ya madaktari na walimu? wanasambaza SMS kwa watu juu ya Madaktari na Walimu:
Wanasambaza na Kupotosha watu ili waamini ujinga kwa kusema DK Ulimboka ametekwa na Serikali:
Najiuliza Kifo cha CHACHA WANGWE
Najiuliza Kifo cha Rejia Mtema
Mbona hatukusikia Chadema wakipotosha watu juu ya Vifo hivyo? pamoja na ukweli uliojificha juu ya vifo hivyo..
Hivi wanaosema cdm ni chama cha wakristo ni waongo? Somalia ilianza kama utani Leo hakuna Serikali..Misri na Libya walianza kama utani kwa kusaidiwa na Nchi za Magharibi kufanya Upotoshaji kama huu mwishowe nchi hizi leo hazina utulivu Tena..Angalia Syria na Nchi za Magharibi zinavyoendelea kuitafuna na leo wananchi wake wasio na Hatia hawalali wala kufanya Shughuli za Maendeleo:Kisa Madaraka na Vyeo:
Ni upungufu wa Hekima na Busara kuamini upotoshaji unaofanywa na baadhi ya watanzania wanaojiita wanauchungu na Nchi Chadema..kama mna uchungu >>Mkajifungue>>
Tudumishe Umoja Amani na Mshikamano wetu chadema wana lao jambo mwisho wake ni maafa