CHIEFMANGU
JF-Expert Member
- Dec 19, 2016
- 654
- 1,070
Mtoto wangu anasoma shule ya sekondari MGULASI, iliyopo kata ya CHAMWINO, MANISPAA YA MOROGORO. (Anaingia kidato cha pili) Wakitumia mtaala mpya, ukianza rasmi mwaka 2025.
Mtoto wangu alichagua mkondo WA biashara, baada ya kupewa elimu ya kuchagua Masomo na wanataka nini wakiwa wakubwa.
Mwaka mzima (kidato cha Kwanza) HAKUWAHI kusoma somo la BIOLOJIA kwa sababu si somo la lazima kwa MUJIBU wa mwongozo WA mtaala mpya
Katika Hali isiyo ya kawaida, kijana wangu amekuja ananiambia wamwambie wamesajiliwa kufanya mtihani WA TAIFA kwa somo la BIOLOJIA.
Namuuliza imekuwaje? Anasema mwalimu wao amewaambia MFUMO WA USAJILI WA BARAZA LA MITIHANI, ndiyo sababu.
Nimeenda shule, kupata ufafanuzi, nimeamgiwa NI KWELI WAMEWASAJILI WATOTO WOTE KATIKA SOMO LA BIOLOJIA KWA SABABU MFUMO WA NECTA UNAKATAA KUSAJILI MASOMO KWA KUFUATA MTAALA MPYA!
Najiuliza, hii si kuwafelisha watoto kwa makusudi? Yaani mtoto ambaye HAKUWAHI kusoma somo Hilo kwa mwaka mzima, analazimishwa kusoma kidato cha mtihani na bila utayari wake.
Je, ni vigumu kwa NECTA kurekebisha mfumo ili uendane na matakwa ya mtaala mpya, na badala yake ni rahisi kumuumiza mwanafunzi kwa kumharibia Kesho yake?
Baraza la MITIHANI (NECTA) tunaomba ufafanuzi wa Jambo hili nyeti kabisa!
Mzazi WA mwanafunzi,
Kata ya CHAMWINO
Manispaa ya Morogoro.
Mtoto wangu alichagua mkondo WA biashara, baada ya kupewa elimu ya kuchagua Masomo na wanataka nini wakiwa wakubwa.
Mwaka mzima (kidato cha Kwanza) HAKUWAHI kusoma somo la BIOLOJIA kwa sababu si somo la lazima kwa MUJIBU wa mwongozo WA mtaala mpya
Katika Hali isiyo ya kawaida, kijana wangu amekuja ananiambia wamwambie wamesajiliwa kufanya mtihani WA TAIFA kwa somo la BIOLOJIA.
Namuuliza imekuwaje? Anasema mwalimu wao amewaambia MFUMO WA USAJILI WA BARAZA LA MITIHANI, ndiyo sababu.
Nimeenda shule, kupata ufafanuzi, nimeamgiwa NI KWELI WAMEWASAJILI WATOTO WOTE KATIKA SOMO LA BIOLOJIA KWA SABABU MFUMO WA NECTA UNAKATAA KUSAJILI MASOMO KWA KUFUATA MTAALA MPYA!
Najiuliza, hii si kuwafelisha watoto kwa makusudi? Yaani mtoto ambaye HAKUWAHI kusoma somo Hilo kwa mwaka mzima, analazimishwa kusoma kidato cha mtihani na bila utayari wake.
Je, ni vigumu kwa NECTA kurekebisha mfumo ili uendane na matakwa ya mtaala mpya, na badala yake ni rahisi kumuumiza mwanafunzi kwa kumharibia Kesho yake?
Baraza la MITIHANI (NECTA) tunaomba ufafanuzi wa Jambo hili nyeti kabisa!
Mzazi WA mwanafunzi,
Kata ya CHAMWINO
Manispaa ya Morogoro.