Msuya aionya serikali ya JK

Kwa kweli msuya amekosea sana kutoa hiyo kauli kwa sababu kwa yeye kuwa waziri mkuu katika moja ya tawala za nchi hii ni wazi kwamba hawezi kutenganishwa na matatizo lukuki yanoikumba nchi yetu tangu mwaka 1961.

Alipaswa yeye binafsi akiri makosa yake aliyotenda wakati akiwa mtawala then atuombe radhi, baada ya hapo ndio akituhumu na chama chake na serikali ya JK. Vingenevyo atakuwa amekengeuka.
tafadhali sana ndugu yangu usijenisababishia nipigwe ban na mod. Hivi una umri wa miaka mingapi wewe? Je reli ya Tazara ni wewe umejenga tena wakati nchi inatoka vitani.! usiwe mshabiki wa vyama vya siasa kuwa mshabiki mkereketwa wa tanzania. Hata yeye anaona mambo hayaendi sawa ndio maana anakemea. hata salimu ahmed salimu , joseph warioba wanakemea hayo hayo mzee msuya anayokemea we vipi!
 
Msuya naye pia ni fisadi. Anamiliki eneo kubwa sana Wilaya ya Mwanga. Amehamisha watu kibabe. Hana lolote.
 
Kwa kweli msuya amekosea sana kutoa hiyo kauli kwa sababu kwa yeye kuwa waziri mkuu katika moja ya tawala za nchi hii ni wazi kwamba hawezi kutenganishwa na matatizo lukuki yanoikumba nchi yetu tangu mwaka 1961.<br />
Alipaswa yeye binafsi akiri makosa yake aliyotenda wakati akiwa mtawala then atuombe radhi, baada ya hapo ndio akituhumu na chama chake na serikali ya JK. Vingenevyo atakuwa amekengeuka.


Wewe vipi bwana? Msuya wakati wao walihakikisha nchi ina umeme unaolingana au kuzidi kidogo na matumizi ya nchi. Sasa tuwaulinze ni mradi gani serikali za awamu zote tatu baada ya ile ya kwanza umejengwa? hamkujua mahitaji yanaongezeka? hamkujua vyanzo hivyo vinazidi kupungua uwezo ama kwa mitambo kuchakaa au mabwawa kudhofishwa na siltation process.
&lt;br /&gt;<br />
Ni upumbavu na ujinga kuhalalisha matatizo ya leo eti kwa sababu historia ya nchi imepinda. Kwani muliomba uongozi mkawafanyie nini Watanzania kama si pamoja na kurekebisha yale ambayo awamu zingine hazikufanikiwa kurekebisha au kuyafanya vizuri.
&lt;br /&gt;<br />
Kwa kweli niliwahi kusikia kiongozi mmoja akisema wenzake wote waliomtangulia hawakuyamaliza matatizo ya watanzania na kwamba na yeye kipindi chake kitapita atakuja mwingine maana yake eti matatizo haya hayatakwisha nilisikitika sana na kwa kufikiri kwangu nilihisi kiongozi yule alighafirika na kwamba ipo siku atawaomba msamaha wananchi. Kwa kifupi historia ya nchi inatusaidia kuindaa nchi kukabili chanagamoto za sasa. hatuwezi kuwalaumu wenzetu waliotutangulia kwa kushindwa kufikia malengo yao au kufikia matumaini yetu. Lakini tutawalaumu pale tu ambapo rasilimali tulizowakabidhi hazikutumika ipasavyo katika kusaidia kuleta maendeleo ya Mtanzania.
&lt;br /&gt;<br />
Hivi Nyerere angekuwa mlafi na rasilimali asilia za nchi hii katika kipindi cha miaka 25 awamu zilifuata baada yake zingekuwa zinategemea nini? Kama unachimba madini huwezi kujenga miundo mbinu ya kuzalisha umeme uweze kuwauzia majirani zako unategemea nini kama si kuiletea umasikini.
Unawezaje kuuza nyumba ya urithi na usijenge ingine, unawezaje kuuza nyumba uliyojenga na pesa zake ukazitumbua. Ndugu watanzania huko ni kuleta umaskini. Msuya aliyefunguka macho na masikio na kuamua kusimama kidete leo kutoa kauli zinazoitayarisha serikali kujirekebisha ni bora kuliko mamuliki 100 wanaonyamaza nyuma ya blanketi la UCCM. Mkapa, Mwinyi, na wengineo wafanye hima kuongoza msimamo bora wa kuishauri serikali ifanye hima kurebisha kero hizi namshukuru Msuya na kuwakemea wote watakao ona mzee huyo amekosea leo.
 
ccm na serikali zake inajitahdi kutatua matatizo ya wananchi wa nchi hii ikiwemo hayo yalioainishwa na kabla a 2015 mambo ya akuwa historia
I hope you are right. I remember in 2007 Kikwete told us that by December the electricity problem will be history. Only it has gotten worse. So I hope you are right for sanity's sake.
 
MBONA HUYU MZEE HAJAELEZA KITU GANI KIFANYIKE. ANATAKIWA AELEZE yeye angekuwa raisi kipindi hiki angefanya nini.Huyu si miongoni wa wale wanaopata pensheni kubwa kuliko. Hana jipya.

Yeye ametoa ujumbe kitu gani kifanyike hiyo sio kazi yake. Ngeleja na wahuni wanzake wanajua nini wanapaswa kufanya ili kuhakikisha Tanzania inapata umeme.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Yeye ametoa ujumbe kitu gani kifanyike hiyo sio kazi yake. Ngeleja na wahuni wanzake wanajua nini wanapaswa kufanya ili kuhakikisha Tanzania inapata umeme.

Chama
Gongo la Mboto DSM

Well said. Nimefurahishwa sana na statement yako hasa hapo penye red. Walioajiriwa kufanya kazi hiyo ndio wanawajibu wakutafuta soln sio Msuya unless Msuya ajitolee kufanya hivyo.
 
Msuya sema.
Sema Usiogope sema
sisi ni watanzania hatuogopi magamba sema


Nimeukumbuka wimbo tuliokuwa tukiimba enzi hizo (nime u edit)
 
Kwa kweli mie nashangaa sana hawa waliowahi kushika nafasi za juu ndani ya CCM au Serikali kutomwambia ukweli Kikwete kwamba nchi imemshinda. Hili siyo siri kabisa na sijui hawa Vingunge wanaogopa nini kuwambia ukweli. Mara nyingi wakisema machache hapo hapo wanapulizia na kumfagilia Kikwete ambaye kwa maoni yangu hastahili kufagiliwa kwenye lolote lile kwani ameshindwa kila idara. Watu kama akina SAS, Warioba na wengineo wasikae kimya au kuongea machache na huku kumfagilia Kikwete.

Waanze sasa kuwa kama CD Msuya na kumuanika hadharani Kikwete ambaye anaipeleka nchi mrama kwa mwaka wa sita sasa, kwa kufanya hivyo labda utendaji wake utabadilika katika hii miaka minne iliyobaki katika awamu yake au kama hawezi kubadilika basi ajiuzulu ili kuwe na Serikali itakayokaimu kwa Mwaka 1 kabla ya uchaguzi mkuu mwingine. Hakuna sababu yoyote ya kusubiri mpaka mwaka 2015 wakati ambapo hali ya nchi itakuwa mbaya zaidi kuliko ilivyo sasa.
 
Back
Top Bottom