Msukule ni nini?

Msukule ni nini?

Zipo aina nyingi za kuchukua watu misukule, aina iliyozoeleka sana ni mtu kufa kisha mwili wake ukazikwa, aina ya pili ni wachawi kuondoa nafsi ya mtu akiwa hai na kuingiziwa pepo na akaendelea kuishi, aina ya tatu ni wachawi kuchukua nyota ya mtu na kuuziwa mtu mwingine.

Huyu Gwajima ni Mwizi tu.
Hakuna mtu anaweza kurudisha mfu hatta siku moja.
Acheni kudanganya watu nyie.
Mtapigwa laana.
 
Majimoto mshana jr
Unatakiwa ufanye nini ili wasikuchukue msukule? Na wanakua wanaangalia vigezo gani mpk wanaona flan anafaa kuwa msukule? Wanaishi sehemu gani exactly /wanapohifadhiwa?
 
Mkuu tomjelly, Majimoto sidhani Kama anamrithi mshana jr nenda jukwaa la biashara kuna Uzi stick unaitwa biashara ya uchawi ni ya 2011, majimoto alikuwa anamwaga nondo za kuogofya kuhusu uchawi, nimeusoma ule Uzi two days ago hapa nalala taa inawaka.
Uzi noma ule niliusoma sikulala siku mbili had nikawa sijielewi nahisi nimezungukwa ña vtu visivo vya kawaida kutetetemeka na baridi juu
 
Zipo aina nyingi za kuchukua watu misukule, aina iliyozoeleka sana ni mtu kufa kisha mwili wake ukazikwa, aina ya pili ni wachawi kuondoa nafsi ya mtu akiwa hai na kuingiziwa pepo na akaendelea kuishi, aina ya tatu ni wachawi kuchukua nyota ya mtu na kuuziwa mtu mwingine.
mkuu naomba kufahamu kuhusu aina hiyo ya pili na ya tatu namna wanavyochukuliwa na wanavyofanyishwa kazi
 
Habari wanajukwaa.
Natambua uwepo wa watu wenye ufahamu na uzoefu katika mambo mbalimbali nami nikaona nipate kufahamishwa jambo hili.
Tangu nikiwa mdogo hadi zama hizi nimesikia na ninaendelea kusikia kuwa mtu fulani hakufa bali amechukuliwa na kufanywa msukule. Hii taaluma ya uchukuaji watu na kuwafanya misukule ipo au ni hadithi tu za kufariji watu? Kama ipo inafanyaje kazi? Nani amewahi kushuhudia msukule na uko katika hali gani?
Mwisho wa msukule (kama upo) ni nini, je atakufa tena kwa mara nyingine au anafanyaje maana hadithi zilizopo ni kuwa lazima mtu afe kwanza kwenye macho ya watu kabla ya kufanywa msukule.

Langu ni hilo tu karibuni sana.

Napenda nikufamishe kuwa misukule ipo, tena kwa idadi kubwa sana, idadi kubwa ya kwanza ni watu waliochukuliwa ufahamu wao na wapo barabarani na majumbani wanatembea vizuri kabisa, wachawi huwanyofoa ufahamu wao, maisha yao yote wanakuwa kwenye himaya yao na wanachotaka ukifanye ndicho utakachokifanya, inakuwa kama vile unavyotumia tv yako kwa kutumia kitufe kinachojulikana kama remote kubadilisha station au vipindi mbalimbali kwenye tv yako. Aina hii ya misukule hapa nchini Tanzania idadi yao inakaribia asilimia 75(%) ya Watanzania wote.

Aina ya pili ya misukule ni wale ambao wamekufa kabisa na wakazikwa, hawa wamegawanyika sehemu tatu.

Wapo misukule kwa ajili ya kufanya kazi za nguvu kama kilimo, uvuvi, kupasua mbao, kulea watoto (house girls), kazi za viwandani n.k. kundi hili pia lina idadi kubwa ya watu, unakuta mchawi mmoja anakuwa na misukule hadi 1,000 na biashara ya misukule ni jambo la kawaida, kama wewe siyo mchawi na unahitaji misukule kwa ajili ya shamba au uvuvi kushusha nyavu chini ya bahari unaenda kwa wachawi na wanakuuzia kwa kiasi unachotaka. Misukule siku yao ya kufa ikifika huwa wanakufa, tofauti ni kuwa wakifa hawazikwi, miili yao hukatwa katwa vipande vipande na siku hiyo huandaliwa karamu ya nyama ya mtu kwa misukule waliobaki, chakula kikuu cha misukule ni pumba za nafaka zilizolowekwa kwenye maji, damu na nyama za watu.

Kundi la pili ni misukule ambao ni watalamu katika fani mbalimbali, kundi hili huwa wanashushwa moja kwa moja shimoni (kuzimu), kazi yao kubwa ni kufanya reserch kwenye maabara, kutengeneza magonjwa yasiyo na tiba, kuvumbua technologya mpya za machine, magari, silaha, ndege, meli, music nk. Kwa taarifa yako vitu vyote vinavyotumika duniani leo hii, technologya hiyo imeasisiwa na kuzimu inapoibuliwa duniani inakuwa kwa ajili ya kuimarisha tu. Mataifa mengi ya Asia, China na Japan huenda kuzimu kununua utaalamu, kila mwezi matajiri wote wa mataifa hayo huchanga fedha nyingi ambazo hushushwa shimoni kununua technologya mpya.

Wachawi wanayo majini ambayo akitupiwa mtu hubana pumzi yake, na anaonekana kama amekufa, watu wanaokufa kifo cha namna hii mazishi yao hufanyika kwa haraka sana, kama kafa usiku, usiku huo huo anazikwa. Mazishi yakiisha fanyika wachawi huenda kwenye kaburi lake, wanavifaa na dua wanazoomba mwili wa marehemu hutoka ardhi na kuinukia juu, wachawi humpulizia madawa ya kichawi na lile jini humwachia, kisha kumpulizia dawa zingine za kumpumbaza na kuondoka naye.

Maisha ya usukule ni matatizo makubwa kila wakati ni vipigo, kupuliziwa madawa na kulishwa kama nguruwe, ukiingia na afya nzuri ukiyamudu sana maisha hayo unaweza kuishi miaka kati ya 5 hadi 10
 
Zipo aina nyingi za kuchukua watu misukule, aina iliyozoeleka sana ni mtu kufa kisha mwili wake ukazikwa, aina ya pili ni wachawi kuondoa nafsi ya mtu akiwa hai na kuingiziwa pepo na akaendelea kuishi, aina ya tatu ni wachawi kuchukua nyota ya mtu na kuuziwa mtu mwingine.

Hizi naona ni habari za watu wasioamini (au hawaamini kabisa kuwa ndg au rafiki yao anaweza kufa hivihivi tu). Kwa kutoamini huko ndg wa wafiwa huendelea kutafuta (kwa waganga) nini sababu ya kifo.
Mganga kwa kuelewa upungufu wa imani yao wengi huambiwa ndg yao bado mzima ila amewekwa msukule, na mara nyingi mganga huyo huwaambia kuwa ana uwezo wa kumrudisha. Na baada ya kula pesa zao huanza tabia ya kuwachosha na mwisho ndg hukata tama.
 
mkuu naomba kufahamu kuhusu aina hiyo ya pili na ya tatu namna wanavyochukuliwa na wanavyofanyishwa kazi

Kila mtu anayo nyota yake ya mafanikio katika maisha yake, bahati mbaya nyota hizi huwa zinaonekana kwa macho ya wachawi (wanajimu). Wachawi hawa wanao uwezo wa kuchukua nyota za watu na kuziuza kwa watu wengine, watu wanaoadhirika sana na tatizo hili ni wanafunzi, utakuta mtoto wako anafanya vizuri sana kwenye masomo, anashika namba ya kwanza darasani, ndani ya darasa hilo hilo anakuwepo kijana ambaye kimasomo haelewi chochote, wazazi wake wanamchukua kwa mganga, mganga anampa kitu chochote cha kutafuna anamwambia ampe yule kijana anayeongoza darasani, yule kijana atakapokula lile tunda/pipi kichwa kinaanza kumuuma sana, anatibiwa hospitali zote bila ya kupata nafuu yoyote, inafika wakati mtoto anasahau hata chumba chake cha kulala, huku mkihangaika na tiba ya mtoto wenu kijana mwezie atakuwa ndiye anayeongoza darasani. Uwezekano wa kurudisha nyota iliyoibiwa upo sana, na nyota inaporudishwa maisha ya ushindi yanachanua tena. Mtu anakuwa na nyota ya biashara, uongozi, kupendwa, siku wachawi wanapochukua hizi nyota shughuli zako zinadorora biashara inakufa na baadaye kupotea kabisa, ukiwahi kurudisha nyota yako maisha yanarudi kama mwazo na wale waliokuwa wanazitumia wanabaki mazezeta.

Nilishuhudia kiongozi fulani alikuwa anatembelea nyota ya kununua, ikafika siku mwenye nyota yake akaenda mahali nyota yake ikarudishwa yule jamaa hadi leo ni zezeta kabisa.

Umewahi kuona watoto mazezeta hasa katika familia zenye ukwasi wa fedha wa kutosha, kinachofanyika kwa baadhi yao ni kumtoa kafara mtoto wake, wachawi wanahamisha ufahamu wa mtoto na kushushwa kuzimu, mtoto anawekwa eneo la biashara au nyumbani kwa uangalizi wa juu sana, kinachofanyika katika ulimwengu wa roho wa kishetani ni kuwa ule ufahamu wa mtoto kuzimu ndio unaowezesha biashara yako ikuwe na kunawiri, kuna ishara anazofanya yule mtoto zezeta, mwenye mtoto anazijua maana ya hizo ishara, kuna ishara zingine utaona duka linafungwa haraka na kuanza kuchoma ubani. Huyu mtoto kitu chochote atakachokitaka ni lazima kitafutwe kwa gharama yoyote na apewe.

Ipo siku nilifika kwa rafiki yangu tuliyesoma naye, ana biashara kubwa ya malori mengi ya mafuta na mizigo, yeye nae alikuwa na kijana wake zezeta, wakati tukiwa tunaongea, yule kijana akafanya ishara kama anaendesha gari na kubadilisha gia na kupiga honi, mimi niliona kitendo kile kama jambo la kawaida, lakini baba yake alisimama ghafula na kuingia ndani mara nikasikia harufu ya ubani na makokoro mengine yanachomwa, kwa hali ile sikuweza tena kuendelea kukaa pale nikaanga kijana wake wa kazi na kuondoka. Kesho yake tukapata habari kuwa mmoja ya lori lake lililokuwa na mizigo ya kwenda Congo limeanguka na mali yote kupotea.

Siku zote biashara za kichawi huishia kubaya
 
Majimoto mshana jr
Unatakiwa ufanye nini ili wasikuchukue msukule? Na wanakua wanaangalia vigezo gani mpk wanaona flan anafaa kuwa msukule? Wanaishi sehemu gani exactly /wanapohifadhiwa?
Hakuna formula na mara nyingi haya ni mambo ya vijijini misukule huhifadhiwa vichakani porini na kwenye Mashamba mbali na vijiji
 
JE MSUKULE NI NINI?

Msukule ni mtu ambaye anahesabiwa amekufa, lakini ukweli ni kuwa mtu huyo huwa amechukuliwa na Mchawi ili amtumie katika kazi zake maalum au amtumie katika mambo yake mengine anayoyataka.

Mchawi humfanya mtu huyo awe maiti au kama kitu kinachojiendesha chenyewe kikiwa kimekufa lakini hakijaoza wala hakiozi.

Mchawi kabla ya kumchukua mtu Msukule hufanya Mkataba Maalum na Jini anayeitwa “BAKAS” ili amsaidie katika kazi hiyo, na kuna Sadaka maalum ambayo hutoa kumlipa Jini huyo kama malipo ya kazi yake. Huyu Bakas ni Jini anayetawala siku ya Jumamosi.

Baada ya kukubaliana na Jini Bakas Mchawi huchagua mtu ambaye anataka kumchukua na akishampata huenda nyumbani kwa mtu huyo kinyume nyume mpaka anafika mlango wa mbele.

Anapofika mlangoni hunyonya roho ya mtu anayemtaka kwa kupitia tundu ya ufunguo na kama tundu hiyo haipo hutoboa tundu ndogo ambayo huiziba akimaliza kazi yake.

Baada ya kuipata roho anayoitaka huitia ndani ya chupa na kuziba chupa hiyo na kuondoka. Kazi hiyo hufanyika usiku wa manane kati ya saa nane na saa tisa usiku.

Siku inayofuata yule aliyechukuliwa roho yake huanza kuugua na hufa ghafla.

Baada ya Mazishi yule Mchawi huenda kaburini akiongozana na yule Jini Bakas ambaye hujigeuza kama babu kizee mwenye ndevu nyingi nyeupe ili kuuchukua ule mwili wa Marehemu.

Wanapofika makaburini yule Jini hukaa upande wa kichwani kwa maiti na mchawi hukaa upande wa miguuni na kila mmoja wao akifanya uchawi wake lakini kazi kubwa ya kumtoa maiti ndani ya kaburi kufanya na Jini.
Jini huomba kwa bidii na kunuiza Uchawi na husema maneno ya kichawi huku akimwaga juu ya kaburi majani ya Mkakaya (Acacia)

Mchawi yeye kwa upande wake husema maneno haya yafuatayo akirudia rudia “Mortoo tombo Mivi” maana yake ni kwamba “aliye ndani ya kaburi ni wangu”

Kwa nguvu za Uchawi mwili hutoka kaburini bila ya kaburi kuchimbwa na kusimama mbele yao na yule mchawi hukabidhiwa maiti huyo.

Baada ya kukabidhiwa kitu cha kwanza ambacho hufanya ni kwenda nyumbani na kumuonesha huyo ndugu zake kuona kama atawakumbuka.

Maiti huyo asipozinduka na kuwagundua ndugu zake au kutambua nyumbani kwao basi Mchawi hujua kwamba kazi imekuwa nzuri na hupelekwa nyumbani kwa mchawi.

Wakifika nyumbani Mchawi humrudishia yule Maiti roho ambayo aliiweka ndani ya chupa na kumnywesha dawa kali ambayo itamfanya asahau kabisa maisha yake yote ya nyuma yaliyopita na baada ya hapo maiti huyo atazinduka na kuwa Msukule.

Kwa hiyo Msukule ni binaadamu anayeishi lakini hana uhuru na anatumiwa kama mtumwa huku ndugu zake au jamaa zake wakijua kwamba amekufa.

Uchawi huu wa kuchukua Msukule ulianza miaka 500 na 1500 A.D. huko nchini Congo DRC na Haiti na kuenea sehemu nyingi za Dunia.
Na hapaTanzania WAPO kAA CHONJO...


Ukiwa na Shida yoyote ile unaweza kunitafuta Kwa kubonyeza hapa.Mawasiliano
Duuh hii mbona hataree..!!
 
Kila mtu anayo nyota yake ya mafanikio katika maisha yake, bahati mbaya nyota hizi huwa zinaonekana kwa macho ya wachawi (wanajimu). Wachawi hawa wanao uwezo wa kuchukua nyota za watu na kuziuza kwa watu wengine, watu wanaoadhirika sana na tatizo hili ni wanafunzi, utakuta mtoto wako anafanya vizuri sana kwenye masomo, anashika namba ya kwanza darasani, ndani ya darasa hilo hilo anakuwepo kijana ambaye kimasomo haelewi chochote, wazazi wake wanamchukua kwa mganga, mganga anampa kitu chochote cha kutafuna anamwambia ampe yule kijana anayeongoza darasani, yule kijana atakapokula lile tunda/pipi kichwa kinaanza kumuuma sana, anatibiwa hospitali zote bila ya kupata nafuu yoyote, inafika wakati mtoto anasahau hata chumba chake cha kulala, huku mkihangaika na tiba ya mtoto wenu kijana mwezie atakuwa ndiye anayeongoza darasani. Uwezekano wa kurudisha nyota iliyoibiwa upo sana, na nyota inaporudishwa maisha ya ushindi yanachanua tena. Mtu anakuwa na nyota ya biashara, uongozi, kupendwa, siku wachawi wanapochukua hizi nyota shughuli zako zinadorora biashara inakufa na baadaye kupotea kabisa, ukiwahi kurudisha nyota yako maisha yanarudi kama mwazo na wale waliokuwa wanazitumia wanabaki mazezeta.

Nilishuhudia kiongozi fulani alikuwa anatembelea nyota ya kununua, ikafika siku mwenye nyota yake akaenda mahali nyota yake ikarudishwa yule jamaa hadi leo ni zezeta kabisa.

Umewahi kuona watoto mazezeta hasa katika familia zenye ukwasi wa fedha wa kutosha, kinachofanyika kwa baadhi yao ni kumtoa kafara mtoto wake, wachawi wanahamisha ufahamu wa mtoto na kushushwa kuzimu, mtoto anawekwa eneo la biashara au nyumbani kwa uangalizi wa juu sana, kinachofanyika katika ulimwengu wa roho wa kishetani ni kuwa ule ufahamu wa mtoto kuzimu ndio unaowezesha biashara yako ikuwe na kunawiri, kuna ishara anazofanya yule mtoto zezeta, mwenye mtoto anazijua maana ya hizo ishara, kuna ishara zingine utaona duka linafungwa haraka na kuanza kuchoma ubani. Huyu mtoto kitu chochote atakachokitaka ni lazima kitafutwe kwa gharama yoyote na apewe.

Ipo siku nilifika kwa rafiki yangu tuliyesoma naye, ana biashara kubwa ya malori mengi ya mafuta na mizigo, yeye nae alikuwa na kijana wake zezeta, wakati tukiwa tunaongea, yule kijana akafanya ishara kama anaendesha gari na kubadilisha gia na kupiga honi, mimi niliona kitendo kile kama jambo la kawaida, lakini baba yake alisimama ghafula na kuingia ndani mara nikasikia harufu ya ubani na makokoro mengine yanachomwa, kwa hali ile sikuweza tena kuendelea kukaa pale nikaanga kijana wake wa kazi na kuondoka. Kesho yake tukapata habari kuwa mmoja ya lori lake lililokuwa na mizigo ya kwenda Congo limeanguka na mali yote kupotea.

Siku zote biashara za kichawi huishia kubaya
duu hii ni hatari zaidi yaani kumbe mtu uko mzima unatembea lakini ni msukule na nyota yako inatumiwa na wengine hii hatari sana
 
Aisee kumbe elimu tuliyonayo haifiki hata 1/10 ya elimu yote duniani.
 
Majimoto mshana jr
Unatakiwa ufanye nini ili wasikuchukue msukule? Na wanakua wanaangalia vigezo gani mpk wanaona flan anafaa kuwa msukule? Wanaishi sehemu gani exactly /wanapohifadhiwa?

Mwamini MUNGU na ishi maisha ya utakatifu, hawatakusogelea.

Kama mwajiri anavyotafuta mfanyakazi mwenye sifa fulani, wachawi/kuzimu nao wanatumia vigezo hivyo hivyo kutafuta wafanyakazi, elimu, uzoefu, nguvu nk. Sifa ya kipekee asiwe mcha MUNGU.
 
Back
Top Bottom