Msukule ni nini?

Msukule ni nini?

Msukule ni mtu anayechukuliwa kimiujiza na wachawi na kwenda kufanyishwa kazi. Msukule huwa hauna uwezo wa kuongea maana hukatwa ulimi
 
Huyu binti wa juzi inamaana hakufikia hatua ya kua msukule, sioni mkiongekea habari yake ilihali ni habari mpya kabisa ingefaa kuifanyia rejea.

Vyovyote iwavyo ni kwamba yule binti anamhusu muhusika mwenyewe kwani ingekua kinyume chake wangesha jitokeza wazazi wake kwa makelele.

©mzizimkavu
mshanajr
 
Lipo pia hili la watoto wadogo/wachanga wanafariki na kusemekana nao wamefanywa msukule angali hawana nguvu za kufanya kazi au hili nalo lipoje hili..na je hizo dawa source yake ni nini?

Binadamu ana mwili na ndani ya mwili kuna roho, roho ya mtoto, roho ya kijana na roho ya mzee zote ziko sawa, tofauti ipo kwenye mwili uliovalishwa hiyo roho. Kwa taarifa yako watoto ndio wanaotumiwa sana kwenye ulozi kuliko vijana na wazee.
 
Poneaponea ni kuwa mvivu.hawachukui wavivu.haha
 
Kariokoo yote ile wale wengine sio watu nadhani ndo sehemu inayoongoza dar kwa misekule inabeba mizigo ile pale acha tu
Hivi misukule hufanyishwa kazi wazi wazi katika macho ya binadamu wa kawaida.
 
JE MSUKULE NI NINI?

Msukule ni mtu ambaye anahesabiwa amekufa, lakini ukweli ni kuwa mtu huyo huwa amechukuliwa na Mchawi ili amtumie katika kazi zake maalum au amtumie katika mambo yake mengine anayoyataka.

Mchawi humfanya mtu huyo awe maiti au kama kitu kinachojiendesha chenyewe kikiwa kimekufa lakini hakijaoza wala hakiozi.

Mchawi kabla ya kumchukua mtu Msukule hufanya Mkataba Maalum na Jini anayeitwa “BAKAS” ili amsaidie katika kazi hiyo, na kuna Sadaka maalum ambayo hutoa kumlipa Jini huyo kama malipo ya kazi yake. Huyu Bakas ni Jini anayetawala siku ya Jumamosi.

Baada ya kukubaliana na Jini Bakas Mchawi huchagua mtu ambaye anataka kumchukua na akishampata huenda nyumbani kwa mtu huyo kinyume nyume mpaka anafika mlango wa mbele.

Anapofika mlangoni hunyonya roho ya mtu anayemtaka kwa kupitia tundu ya ufunguo na kama tundu hiyo haipo hutoboa tundu ndogo ambayo huiziba akimaliza kazi yake.

Baada ya kuipata roho anayoitaka huitia ndani ya chupa na kuziba chupa hiyo na kuondoka. Kazi hiyo hufanyika usiku wa manane kati ya saa nane na saa tisa usiku.

Siku inayofuata yule aliyechukuliwa roho yake huanza kuugua na hufa ghafla.

Baada ya Mazishi yule Mchawi huenda kaburini akiongozana na yule Jini Bakas ambaye hujigeuza kama babu kizee mwenye ndevu nyingi nyeupe ili kuuchukua ule mwili wa Marehemu.

Wanapofika makaburini yule Jini hukaa upande wa kichwani kwa maiti na mchawi hukaa upande wa miguuni na kila mmoja wao akifanya uchawi wake lakini kazi kubwa ya kumtoa maiti ndani ya kaburi kufanya na Jini.
Jini huomba kwa bidii na kunuiza Uchawi na husema maneno ya kichawi huku akimwaga juu ya kaburi majani ya Mkakaya (Acacia)

Mchawi yeye kwa upande wake husema maneno haya yafuatayo akirudia rudia “Mortoo tombo Mivi” maana yake ni kwamba “aliye ndani ya kaburi ni wangu”

Kwa nguvu za Uchawi mwili hutoka kaburini bila ya kaburi kuchimbwa na kusimama mbele yao na yule mchawi hukabidhiwa maiti huyo.

Baada ya kukabidhiwa kitu cha kwanza ambacho hufanya ni kwenda nyumbani na kumuonesha huyo ndugu zake kuona kama atawakumbuka.

Maiti huyo asipozinduka na kuwagundua ndugu zake au kutambua nyumbani kwao basi Mchawi hujua kwamba kazi imekuwa nzuri na hupelekwa nyumbani kwa mchawi.

Wakifika nyumbani Mchawi humrudishia yule Maiti roho ambayo aliiweka ndani ya chupa na kumnywesha dawa kali ambayo itamfanya asahau kabisa maisha yake yote ya nyuma yaliyopita na baada ya hapo maiti huyo atazinduka na kuwa Msukule.

Kwa hiyo Msukule ni binaadamu anayeishi lakini hana uhuru na anatumiwa kama mtumwa huku ndugu zake au jamaa zake wakijua kwamba amekufa.

Uchawi huu wa kuchukua Msukule ulianza miaka 500 na 1500 A.D. huko nchini Congo DRC na Haiti na kuenea sehemu nyingi za Dunia.
Na hapaTanzania WAPO kAA CHONJO...


Ukiwa na Shida yoyote ile unaweza kunitafuta Kwa kubonyeza hapa.Mawasiliano
Kwa nyongeza ni kwamba, msukule huwa unakufa na ukifa huwa ni chakula cha wachawi.
 
Wapo wanaokatwa ulimi na hii ndio hatua ya mwisho ya kukamilisha usukule wao...hapo hata ikitokea akarudi katika hali ya uzima wa kawaida hataweza kuongea lolote
Katika maisha yangu niliwahi kumuona msukule wa kweli (sio hawa wa kina mitume na manabii)mwaka 1984 kipindi kile cha uhujumu uchumi na ni baada ya mmiliki wake kufa, kwa mdomo wake alisema kamhifadhi fulani kwenye shamba lake kubwa la migomba


Arusha kati ya mwaka 1989 au 90 mwanzoni wakati wahindi wanakimbia uhujumu uchumi na kwenda Kenya, kuna familia ya kihindi walikimbia na kumuacha msukule muhindi mwenzao karibu wiki nzima ndani ya nyumba. Watoto walikuwa hawapiiti pale mtaani kwenda shule kuogopa kunyonywa damu. Cha kushangaza yule msukule alikuja kupotea kimaajab na mpaka leo imebaki hadithi tu.
 
Back
Top Bottom