Msukule ni nini?

Msukule ni nini?

Inasemekana hukatwa ulimi,hili lina ukweli wowote?
Wapo wanaokatwa ulimi na hii ndio hatua ya mwisho ya kukamilisha usukule wao...hapo hata ikitokea akarudi katika hali ya uzima wa kawaida hataweza kuongea lolote
Katika maisha yangu niliwahi kumuona msukule wa kweli (sio hawa wa kina mitume na manabii)mwaka 1984 kipindi kile cha uhujumu uchumi na ni baada ya mmiliki wake kufa, kwa mdomo wake alisema kamhifadhi fulani kwenye shamba lake kubwa la migomba
 
JE MSUKULE NI NINI?

Msukule ni mtu ambaye anahesabiwa amekufa, lakini ukweli ni kuwa mtu huyo huwa amechukuliwa na Mchawi ili amtumie katika kazi zake maalum au amtumie katika mambo yake mengine anayoyataka.

Mchawi humfanya mtu huyo awe maiti au kama kitu kinachojiendesha chenyewe kikiwa kimekufa lakini hakijaoza wala hakiozi.

Mchawi kabla ya kumchukua mtu Msukule hufanya Mkataba Maalum na Jini anayeitwa “BAKAS” ili amsaidie katika kazi hiyo, na kuna Sadaka maalum ambayo hutoa kumlipa Jini huyo kama malipo ya kazi yake. Huyu Bakas ni Jini anayetawala siku ya Jumamosi.

Baada ya kukubaliana na Jini Bakas Mchawi huchagua mtu ambaye anataka kumchukua na akishampata huenda nyumbani kwa mtu huyo kinyume nyume mpaka anafika mlango wa mbele.

Anapofika mlangoni hunyonya roho ya mtu anayemtaka kwa kupitia tundu ya ufunguo na kama tundu hiyo haipo hutoboa tundu ndogo ambayo huiziba akimaliza kazi yake.

Baada ya kuipata roho anayoitaka huitia ndani ya chupa na kuziba chupa hiyo na kuondoka. Kazi hiyo hufanyika usiku wa manane kati ya saa nane na saa tisa usiku.

Siku inayofuata yule aliyechukuliwa roho yake huanza kuugua na hufa ghafla.

Baada ya Mazishi yule Mchawi huenda kaburini akiongozana na yule Jini Bakas ambaye hujigeuza kama babu kizee mwenye ndevu nyingi nyeupe ili kuuchukua ule mwili wa Marehemu.

Wanapofika makaburini yule Jini hukaa upande wa kichwani kwa maiti na mchawi hukaa upande wa miguuni na kila mmoja wao akifanya uchawi wake lakini kazi kubwa ya kumtoa maiti ndani ya kaburi kufanya na Jini.
Jini huomba kwa bidii na kunuiza Uchawi na husema maneno ya kichawi huku akimwaga juu ya kaburi majani ya Mkakaya (Acacia)

Mchawi yeye kwa upande wake husema maneno haya yafuatayo akirudia rudia “Mortoo tombo Mivi” maana yake ni kwamba “aliye ndani ya kaburi ni wangu”

Kwa nguvu za Uchawi mwili hutoka kaburini bila ya kaburi kuchimbwa na kusimama mbele yao na yule mchawi hukabidhiwa maiti huyo.

Baada ya kukabidhiwa kitu cha kwanza ambacho hufanya ni kwenda nyumbani na kumuonesha huyo ndugu zake kuona kama atawakumbuka.

Maiti huyo asipozinduka na kuwagundua ndugu zake au kutambua nyumbani kwao basi Mchawi hujua kwamba kazi imekuwa nzuri na hupelekwa nyumbani kwa mchawi.

Wakifika nyumbani Mchawi humrudishia yule Maiti roho ambayo aliiweka ndani ya chupa na kumnywesha dawa kali ambayo itamfanya asahau kabisa maisha yake yote ya nyuma yaliyopita na baada ya hapo maiti huyo atazinduka na kuwa Msukule.

Kwa hiyo Msukule ni binaadamu anayeishi lakini hana uhuru na anatumiwa kama mtumwa huku ndugu zake au jamaa zake wakijua kwamba amekufa.

Uchawi huu wa kuchukua Msukule ulianza miaka 500 na 1500 A.D. huko nchini Congo DRC na Haiti na kuenea sehemu nyingi za Dunia.
Na hapaTanzania WAPO kAA CHONJO...


Ukiwa na Shida yoyote ile unaweza kunitafuta Kwa kubonyeza hapa.Mawasiliano
Nashukuru sana Dr. MziziMkavu kwa maelezo mazuri sana. Pamoja na majibu na maelezo hayo bado nina mambo yenye kuhitaji ufafanuzi.
Baada ya kufanywa msukule wanakula nini ?
Je akishakuwa msukule atakaa na hiyo hali kwa muda gani na mwisho wake ni nini? Je anakufa tena au anafanyaje au hatakuwa na mwisho?
Wakiwa katika hali hiyo wanaweza kufanya kazi gani ?
Asante.
 
Wapo wanaokatwa ulimi na hii ndio hatua ya mwisho ya kukamilisha usukule wao...hapo hata ikitokea akarudi katika hali ya uzima wa kawaida hataweza kuongea lolote
Katika maisha yangu niliwahi kumuona msukule wa kweli (sio hawa wa kina mitume na manabii)mwaka 1984 kipindi kile cha uhujumu uchumi na ni baada ya mmiliki wake kufa, kwa mdomo wake alisema kamhifadhi fulani kwenye shamba lake kubwa la migomba
Shukrani kwa elimu adimu mkubwa.
 
Zipo aina nyingi za kuchukua watu misukule, aina iliyozoeleka sana ni mtu kufa kisha mwili wake ukazikwa, aina ya pili ni wachawi kuondoa nafsi ya mtu akiwa hai na kuingiziwa pepo na akaendelea kuishi, aina ya tatu ni wachawi kuchukua nyota ya mtu na kuuziwa mtu mwingine.
 
Nashukuru sana Dr. MziziMkavu kwa maelezo mazuri sana. Pamoja na majibu na maelezo hayo bado nina mambo yenye kuhitaji ufafanuzi.
Baada ya kufanywa msukule wanakula nini ?
Je akishakuwa msukule atakaa na hiyo hali kwa muda gani na mwisho wake ni nini? Je anakufa tena au anafanyaje au hatakuwa na mwisho?
Wakiwa katika hali hiyo wanaweza kufanya kazi gani ?
Asante.
Baada ya kwisha kuwa wewe Msukule wanakutumia kwa kazi zao mpaka hapo utakapo kufa kifo cha kawaida wanakuzika au kukutupa porini unaliwa na wanyama fisi,simba ndio mchezo umemalizika.

 
Wapo watu huwa wanatafuta watu wa kumfanyia kazi zake bila ya malipo, watu kama hao huwaendea wachawi na kumwomba amtafutie vijana wenye nguvu kwa ajili ya kazi za shamba au kwa kazi ya kushusha nyavu za uvuvi wa samaki chini ya maji, au kwa kazi ya kwenda kuiba, au kwa kazi za kwenye viwanda n.k

Mchawi akimwona kijana mwenye sifa hizo huandaa uchawi na kuita jini kwa ajili ya kumzibiti, kwa sababu kifo chochote ni lazima kuwepo na sababu, njia wanazotumia sana ni kutumiwa jini na kijana anaumwa sana kichwa mbele ya paji la uso na baada ya muda kijana anafariki, kabila ya kifo chake wanachukuwa kipande cha mgomba, yule jini aliyetumwa anaingia ndani ya ule mgomba na kuvaa sura ya marehemu kabisa wanafana kwa kila kitu. Mchawi aliyepewa kazi ya kutafuta wafanyakazi humshika yule kijana na kumpaka madawa ya kumpumbaza na kumfanya asionekane kwa macho ya kawaida, hubaki naye ndani ya nyumba.

Ndugu mnachukua mgomba wenu na kuanza maandalizi ya mazishi, kwa kawaida vifo vya aina hii huwa vina vituko vingi sana, ndugu kutokuelewana, jambo dogo unazuka ubishi hadi watu wanapigana.

Jambo muhimu sana kwa wachawi hawa kukamilisha shughuli ni kuwafanya ndugu wakubali kuwa ndugu yao amekufa, na mbinu kubwa wanayotumia na kuhakikisha ndugu wanalia sana. Wakiona hakuna mtu anayelia, atatokea mtu hasa mwanamke atakuja analia sana na kujitupa chini kwenye vumbi, ajabu iliyoje ni kuwa huyo mwanamke atakua hajulikani kabisa kwenye hiyo familia.

Ndugu wanapoanza nao kumlilia ndugu yao, basi mjue kilio chenu ndiyo rukhusa ya wachawi kuondoka na ndugu yenu, kama ndugu wakitulia kabisa, ukweli ni kuwa hawa wachawi hawataweza kamwe kumwondoa ndugu yenu ndani ya nyumba yake.

Kama wamefanikiwa kuondoka nae, zipo dawa za kumsafisha asionekane na dawa zingine ananyweshwa ulimi unarudi ndani ya tumbo na hataweza kuongea. Misukule huwa wanalishwa sana pumba za nafaka, damu za watu na nyama za watu waliokufa.
 
Wapo watu huwa wanatafuta watu wa kumfanyia kazi zake bila ya malipo, watu kama hao huwaendea wachawi na kumwomba amtafutie vijana wenye nguvu kwa ajili ya kazi za shamba au kwa kazi ya kushusha nyavu za uvuvi wa samaki chini ya maji, au kwa kazi ya kwenda kuiba, au kwa kazi za kwenye viwanda n.k

Mchawi akimwona kijana mwenye sifa hizo huandaa uchawi na kuita jini kwa ajili ya kumzibiti, kwa sababu kifo chochote ni lazima kuwepo na sababu, njia wanazotumia sana ni kutumiwa jini na kijana anaumwa sana kichwa mbele ya paji la uso na baada ya muda kijana anafariki, kabila ya kifo chake wanachukuwa kipande cha mgomba, yule jini aliyetumwa anaingia ndani ya ule mgomba na kuvaa sura ya marehemu kabisa wanafana kwa kila kitu. Mchawi aliyepewa kazi ya kutafuta wafanyakazi humshika yule kijana na kumpaka madawa ya kumpumbaza na kumfanya asionekane kwa macho ya kawaida, hubaki naye ndani ya nyumba.

Ndugu mnachukua mgomba wenu na kuanza maandalizi ya mazishi, kwa kawaida vifo vya aina hii huwa vina vituko vingi sana, ndugu kutokuelewana, jambo dogo unazuka ubishi hadi watu wanapigana.

Jambo muhimu sana kwa wachawi hawa kukamilisha shughuli ni kuwafanya ndugu wakubali kuwa ndugu yao amekufa, na mbinu kubwa wanayotumia na kuhakikisha ndugu wanalia sana. Wakiona hakuna mtu anayelia, atatokea mtu hasa mwanamke atakuja analia sana na kujitupa chini kwenye vumbi, ajabu iliyoje ni kuwa huyo mwanamke atakua hajulikani kabisa kwenye hiyo familia.

Ndugu wanapoanza nao kumlilia ndugu yao, basi mjue kilio chenu ndiyo rukhusa ya wachawi kuondoka na ndugu yenu, kama ndugu wakitulia kabisa, ukweli ni kuwa hawa wachawi hawataweza kamwe kumwondoa ndugu yenu ndani ya nyumba yake.

Kama wamefanikiwa kuondoka nae, zipo dawa za kumsafisha asionekane na dawa zingine ananyweshwa ulimi unarudi ndani ya tumbo na hataweza kuongea. Misukule huwa wanalishwa sana pumba za nafaka, damu za watu na nyama za watu waliokufa.
Lipo pia hili la watoto wadogo/wachanga wanafariki na kusemekana nao wamefanywa msukule angali hawana nguvu za kufanya kazi au hili nalo lipoje hili..na je hizo dawa source yake ni nini?
 
Mkuu MziziMkavu nahitaji kuwa mchawi ili na mimi niweze kuwa na misukule yangu, maana kuna mdada humu ndani atongozeki, so ni bora nimtoe awe Msukule wangu ili tufanye yetu!!!
 
Wapo watu huwa wanatafuta watu wa kumfanyia kazi zake bila ya malipo, watu kama hao huwaendea wachawi na kumwomba amtafutie vijana wenye nguvu kwa ajili ya kazi za shamba au kwa kazi ya kushusha nyavu za uvuvi wa samaki chini ya maji, au kwa kazi ya kwenda kuiba, au kwa kazi za kwenye viwanda n.k

Mchawi akimwona kijana mwenye sifa hizo huandaa uchawi na kuita jini kwa ajili ya kumzibiti, kwa sababu kifo chochote ni lazima kuwepo na sababu, njia wanazotumia sana ni kutumiwa jini na kijana anaumwa sana kichwa mbele ya paji la uso na baada ya muda kijana anafariki, kabila ya kifo chake wanachukuwa kipande cha mgomba, yule jini aliyetumwa anaingia ndani ya ule mgomba na kuvaa sura ya marehemu kabisa wanafana kwa kila kitu. Mchawi aliyepewa kazi ya kutafuta wafanyakazi humshika yule kijana na kumpaka madawa ya kumpumbaza na kumfanya asionekane kwa macho ya kawaida, hubaki naye ndani ya nyumba.

Ndugu mnachukua mgomba wenu na kuanza maandalizi ya mazishi, kwa kawaida vifo vya aina hii huwa vina vituko vingi sana, ndugu kutokuelewana, jambo dogo unazuka ubishi hadi watu wanapigana.

Jambo muhimu sana kwa wachawi hawa kukamilisha shughuli ni kuwafanya ndugu wakubali kuwa ndugu yao amekufa, na mbinu kubwa wanayotumia na kuhakikisha ndugu wanalia sana. Wakiona hakuna mtu anayelia, atatokea mtu hasa mwanamke atakuja analia sana na kujitupa chini kwenye vumbi, ajabu iliyoje ni kuwa huyo mwanamke atakua hajulikani kabisa kwenye hiyo familia.

Ndugu wanapoanza nao kumlilia ndugu yao, basi mjue kilio chenu ndiyo rukhusa ya wachawi kuondoka na ndugu yenu, kama ndugu wakitulia kabisa, ukweli ni kuwa hawa wachawi hawataweza kamwe kumwondoa ndugu yenu ndani ya nyumba yake.

Kama wamefanikiwa kuondoka nae, zipo dawa za kumsafisha asionekane na dawa zingine ananyweshwa ulimi unarudi ndani ya tumbo na hataweza kuongea. Misukule huwa wanalishwa sana pumba za nafaka, damu za watu na nyama za watu waliokufa.
Duh asante sana kwa elimu hiyo. Mpaka nimeogopa sana. Kwanini ni mgomba mara nyingi. Je ni upatikanaji wake au kuna siri gani kwenye mgomba na sio mti au kitu kingine?
 
Back
Top Bottom