lazima tukubali contradiction ndani ya ccm ni kubw a kuliko tatizo la ukawa, na tayari magufuli ni kama anakimbia na mpira wake mwenyewe bila kumpasia mtu wala kocha wake mkuu, ashindwe, au ashinde, ni lazima sana ccm itabadilika sana, nahisi kitu cha kwanza tutakachoona ni revolt against their chairman, muda pale uraisi utaisha, nikiingia rohoni kwa pinda, balali , profesa muhongo, mark mwandosya, warioba, hawa ni watu wana maudhi kwa sasa ya rohoni, lakini baada ya tarehe 25 octoba yatakuwa maudhi ya wazi, ni kwa mtazamo wangu, hawa ni watu wazima, amabo wamefanya uamuzi wa uvumilivu, wakiamini kuwa kwa nini tumuachie chama mwenyekiti wa mpito ( miaka kumi imepita) na aondoke ili tukichukue chama cha nyerere kutoka kwenye mitandao na uswahili uliokithiri, naamini hii itakuwa sooner than later, hapo contadictions za magufuli hatutazizungumzia, kwani kama suala ni mabadiliko, basi mabadiliko kutoka kwa kikwete, tofauti na mabadiliko ya lowassa ya kutoka CCM kwenda chadema. magufuli atataka mabadiliko ya mfumo wa utawala wa nchi, na ndani ya CCM, na pamoja na uongozi wote kutoka wilaya hadi taifa, watu wa poyoyo, jazba na matumizi mabaya ya nguvu za umma, mitandao ya watu na blind followers ( bulembo, nape, makonda etc) , kwa hiyo situation ya siasa tanzania ndani ya nchi na ndani ya ccm yenyewe, bado iko very fluid, bunge bado hapo, na contradiction za zanzibar bado hapo