Hilo liko wazi bado wapo wanachadema wengi tu ambao wanasimamia misingi ya Chadema asilia, sio hii ya Mbowe kubadili gia angani na kuuza chama.
Wagombea ubunge na udiwani wa Chadema, wengi sasa wanapigania maslai yao kwa maana ya viti wanavyoviwania.
Utashangaa baada ya uchaguzi dharau za wabunge zitavyoibuka dhidi ya Chama, ule utiifu kwa chama wote umeisha, Na mpaka sasa ndani ya Chadema hakuna wa kusimamia wala kufuatilia maendeleo ya wagombea majimboni zaidi ya wao wenyewe kukuruka.
Sasa hivi huwezi kuona umoja kama ule wa awali, wabunge kusaidiana kwenye majimbo, mbunge wa jimbo A kwenda kusaidia mgombea wa jimbo B.
Nakumbuka 2010 wabunge wengi sana kama sio wote walitembeleana majimboni, kupeana nguvu na kubadilishana uzoefu lakini leo kila mtu na lwake.
Sasa hivi hakuna vikao vya kamati kuu kujadili mwenendo wa kampeni , ila Kuna vikao vya Mbowe na Team Lowassa.
Hakuna matamko ya Chama, ila Kuna matamko ya team Lowassa, Mbatia akiwa akitangulizwa mbele kama kondoo wa kafara.
Yuko wapi John Mnyika Naibu katibu mkuu Bara, yuko wapi Tumaini Makene msemaji wa Chama, Salumu Mwalimu ni kama anaburuzwa tu , japo alizunguka Tanzania nzima na watu tukamwelewa kuwa kijana ni hazina ya chama lakini leo kapotelea wapi? hatujui pengine nafsi inamsuta kwa kutenda asiyoyaamini.
Kwa kweli bado naiota Chadema yangu ya awali, Chadema ya kujitolea, Bila kujali gharama ama muda.
Japo sijui itarudi lini lakini bado naiota, Chadema ya makamanda wa ukweli sio hao wa sasa wa plastic.
Chadema ya Silinde, Lema, Sugu , Wenje, Lisu, Mdee, Mnyika, Msigwa wakiongea utapenda uendelee kuwasikiliza.
Na ndio waliochangia vijana wengi kujikita kwenye siasa kuanzia serikali za mitaa mpaka ubunge, sasa hivi si ajabu kijana wa miaka ishirini ni mwenyekiti serikali za mitaa, Madiwani ndio kabisa vijana wadogo kabisa ndio wanawania.
Ila hii Chadema ya Sumaye, Masha, Babu duni, duh!! Mungu atunusuru.